Mambo ya Walawi 17:1-16

  • Hema la ibada, mahali pa kutoa dhabihu (1-9)

  • Wakatazwa kula damu (10-14)

  • Sheria kuhusu wanyama waliokufa (15, 16)

17  Yehova akaendelea kumwambia Musa:   “Mwambie Haruni na wanawe na Waisraeli wote, ‘Yehova ameamuru hivi:  “‘“Mwisraeli yeyote akimchinja ng’ombe dume au mwanakondoo dume au mbuzi ndani au nje ya kambi,  na kukosa kumleta kwenye mlango wa hema la mkutano ili kumtolea Yehova dhabihu mbele ya hema la Yehova la ibada, mtu huyo atakuwa na hatia ya damu. Ameua,* naye ni lazima auawe.  Itakuwa hivyo ili Waisraeli wamletee Yehova dhabihu wanazotolea mashambani, wamletee kuhani dhabihu hizo kwenye mlango wa hema la mkutano. Wanapaswa kumtolea Yehova dhabihu hizo zikiwa dhabihu za ushirika.+  Naye kuhani atainyunyizia madhabahu ya Yehova damu ya dhabihu hizo kwenye mlango wa hema la mkutano na kuteketeza mafuta yake ili yafuke moshi yakiwa harufu inayompendeza* Yehova.+  Kwa hiyo hawapaswi tena kutoa dhabihu zao kwa roho waovu wenye umbo la mbuzi,*+ wanaofanya nao ukahaba.+ Hiyo itakuwa sheria ya kudumu kwa ajili yenu katika vizazi vyenu vyote.”’  “Waambie hivi: ‘Mwisraeli yeyote au mgeni yeyote anayeishi miongoni mwenu atakayetoa dhabihu ya kuteketezwa au dhabihu yoyote  na kukosa kuileta kwenye mlango wa hema la mkutano ili kumtolea Yehova ni lazima auawe.+ 10  “‘Mwisraeli yeyote au mgeni yeyote anayeishi miongoni mwenu akila damu yoyote ile,+ kwa hakika nitamkataa* mtu anayekula damu, nami nitamwangamiza atoke miongoni mwa watu wake. 11  Kwa maana uhai wa kiumbe umo* katika damu,+ nami nimeitoa kwenye madhabahu+ ili mwitumie kufunika dhambi zenu, kwa maana damu ndiyo inayofunika dhambi+ kupitia uhai ulio ndani yake. 12  Ndiyo sababu nimewaambia Waisraeli hivi: “Hakuna yeyote kati yenu anayepaswa kula damu, na hakuna mgeni yeyote anayeishi miongoni mwenu+ anayepaswa kula damu.”+ 13  “‘Mwisraeli yeyote au mgeni yeyote anayeishi miongoni mwenu akiwinda na kumkamata mnyama wa mwituni au ndege anayeweza kuliwa, ni lazima amwage damu yake+ chini na kuifunika kwa udongo. 14  Kwa maana uhai wa* kila kiumbe ni damu yake, kwa sababu uhai umo* ndani ya damu. Kwa hiyo, niliwaambia Waisraeli: “Hampaswi kula damu ya kiumbe yeyote kwa sababu uhai wa kila kiumbe umo katika damu yake. Mtu yeyote anayekula damu atauawa.”+ 15  Mtu yeyote, awe ni mwenyeji au mgeni, akila mnyama aliyepatikana amekufa au aliyeraruliwa na mnyama wa mwituni,+ basi ni lazima afue mavazi yake na kuoga kwenye maji,+ naye hatakuwa safi mpaka jioni. 16  Lakini asipofua mavazi yake na kuoga, atawajibika kwa sababu ya kosa lake.’”+

Maelezo ya Chini

Tnn., “Amemwaga damu.”
Au “inayomtuliza.”
Tnn., “kwa wale mbuzi.”
Tnn., “nitaukaza uso wangu dhidi ya.”
Au “nafsi ya kiumbe imo.”
Au “nafsi ya.”
Au “nafsi imo.”