Mambo ya Walawi 18:1-30

  • Ngono haramu (1-30)

    • Msiwaige Wakanaani (3)

    • Ngono mbalimbali kati ya watu wa ukoo (6-18)

    • Wakati wa hedhi (19)

    • Ngono kati ya watu wa jinsia moja (22)

    • Ngono na wanyama (23)

    • ‘Msijichafue, kama sivyo, nchi itawatapika’ (24-30)

18  Yehova akaendelea kumwambia Musa:  “Waambie Waisraeli hivi: ‘Mimi ni Yehova Mungu wenu.+  Msifanye kama wanavyofanya katika nchi ya Misri ambako mliishi, wala msifanye kama wanavyofanya katika nchi ya Kanaani ambako nawapeleka.+ Msifuate sheria zao.  Mnapaswa kutekeleza sheria zangu,* nanyi mnapaswa kutii amri zangu na kuzifuata.+ Mimi ni Yehova Mungu wenu.  Ni lazima mshike amri zangu na sheria zangu;* yeyote anayefanya hivyo ataishi kupitia hizo.+ Mimi ni Yehova.  “‘Hakuna mtu yeyote kati yenu anayepaswa kumkaribia mtu wake wa karibu wa ukoo ili kufanya naye ngono.*+ Mimi ni Yehova.  Usifanye ngono na baba yako wala mama yako. Yeye ni mama yako, usifanye naye ngono.  “‘Usifanye ngono na mke wa baba yako.+ Utamwaibisha baba yako.*  “‘Usifanye ngono na dada yako, awe ni binti ya baba yako au binti ya mama yako, awe amezaliwa katika nyumba ileile au amezaliwa nje.+ 10  “‘Usifanye ngono na binti ya mwana wako au binti ya binti yako, kwa sababu ni uchi wako mwenyewe. 11  “‘Usifanye ngono na binti ya mke wa baba yako, mtoto wa baba yako, kwa sababu ni dada yako. 12  “‘Usifanye ngono na dada ya baba yako. Ana uhusiano wa damu na baba yako.+ 13  “‘Usifanye ngono na dada ya mama yako, kwa sababu ana uhusiano wa damu na mama yako. 14  “‘Usimwaibishe* ndugu ya baba yako kwa kufanya ngono na mke wake. Mke huyo ni shangazi yako.+ 15  “‘Usifanye ngono na binti mkwe wako.+ Yeye ni mke wa mwana wako, usifanye naye ngono. 16  “‘Usifanye ngono na mke wa ndugu yako,+ kwa sababu utamwaibisha ndugu yako.* 17  “‘Usifanye ngono na mwanamke na binti yake.+ Usimchukue binti ya mwana wa mwanamke huyo na binti ya binti yake ili kufanya nao ngono. Wao ni watu wake wa karibu wa ukoo; hilo ni tendo chafu linalochukiza.* 18  “‘Usimchukue dada ya mke wako ili awe mke mwenza+ na kufanya naye ngono wakati mke wako angali hai. 19  “‘Usimkaribie mwanamke wakati wa hedhi anapokuwa si safi ili kufanya naye ngono.+ 20  “‘Usifanye ngono na mke wa jirani yako* na hivyo kujichafua.+ 21  “‘Usikubali mtoto wako yeyote atolewe dhabihu kwa Moleki.+ Usilichafue jina la Mungu wako kwa njia hiyo.+ Mimi ni Yehova. 22  “‘Usilale na mwanamume kama vile unavyolala na mwanamke.+ Ni tendo linalochukiza. 23  “‘Mwanamume hapaswi kujichafua kwa kufanya ngono na mnyama; wala mwanamke hapaswi kwenda kufanya ngono na mnyama.+ Kufanya hivyo kunakiuka sheria ya asili. 24  “‘Msijichafue kwa kufanya jambo lolote kati ya mambo hayo, kwa maana mataifa ninayoyafukuza kutoka mbele yenu yamejichafua kwa mambo hayo yote.+ 25  Kwa hiyo nchi si safi, nami nitaiadhibu kwa sababu ya dhambi yake, nayo nchi itawatapika wakaaji wake.+ 26  Lakini ni lazima ninyi mzishike amri zangu na sheria zangu,*+ msifanye jambo lolote kati ya mambo hayo yenye kuchukiza, awe ni mwenyeji au mgeni anayeishi miongoni mwenu.+ 27  Kwa maana mambo hayo yote yenye kuchukiza yalifanywa na watu walioishi katika nchi hiyo kabla yenu,+ na sasa nchi si safi. 28  Msifanye mambo hayo ili nchi isiwatapike kwa sababu ya kuichafua kama itakavyoyatapika mataifa yaliyowatangulia. 29  Mtu yeyote akifanya jambo lolote kati ya mambo hayo yenye kuchukiza, wote wanaofanya mambo hayo ni lazima wauawe watoke miongoni mwa watu wao. 30  Ni lazima mtimize wajibu wenu kwangu kwa kutofuata desturi yoyote kati ya desturi zenye kuchukiza zilizofuatwa kabla yenu,+ ili msijichafue kwa desturi hizo. Mimi ni Yehova Mungu wenu.’”

Maelezo ya Chini

Tnn., “maamuzi yangu ya hukumu.”
Tnn., “maamuzi yangu ya hukumu.”
Tnn., “kufunua uchi wake.”
Tnn., “Ni uchi wa baba yako.”
Tnn., “Usifunue uchi wa.”
Tnn., “ni uchi wa ndugu yako.”
Au “ni mwenendo wa aibu; mwenendo mchafu uliopotoka.”
Au “rafiki yako.”
Tnn., “maamuzi yangu ya hukumu.”