Mambo ya Walawi 21:1-24

  • Makuhani wawe watakatifu, wasiwe wachafu (1-9)

  • Kuhani mkuu asijichafue (10-15)

  • Makuhani wasiwe na kasoro yoyote mwilini (16-24)

21  Yehova akaendelea kumwambia Musa: “Waambie hivi wana wa Haruni, makuhani: ‘Mtu yeyote kati yenu asijichafue kwa kumgusa mtu aliyekufa* miongoni mwa watu wake.+  Lakini anaweza kufanya hivyo kwa ajili ya mtu wa karibu wa ukoo aliye na uhusiano wa damu naye, mama yake, baba yake, mwana wake, binti yake, ndugu yake,  na anaweza kujichafua kwa kumgusa dada yake wa karibu ikiwa ni bikira na hajaolewa.  Hapaswi kujichafua na kujitia unajisi kwa kumgusa mke wa mwanamume anayetoka katika ukoo wake.  Hawapaswi kunyoa upara+ au kukata ncha za ndevu zao au kujikatakata mwilini.+  Wanapaswa kuwa watakatifu mbele za Mungu wao,+ nao hawapaswi kulichafua jina la Mungu wao,+ kwa sababu wanatoa dhabihu za Yehova zinazochomwa kwa moto, mkate wa* Mungu wao, lazima wawe watakatifu.+  Hawapaswi kumwoa kahaba,+ mwanamke aliyenajisiwa, au mwanamke aliyetalikiwa na mume wake,+ kwa sababu kuhani ni mtakatifu mbele za Mungu wake.  Ni lazima umtakase kuhani,+ kwa sababu ndiye anayetoa mkate wa Mungu wenu. Mnapaswa kumwona kuwa mtakatifu, kwa sababu mimi, Yehova, ninayewatakasa ninyi, ni mtakatifu.+  “‘Sasa binti ya kuhani akijichafua kwa kufanya ukahaba, anamchafua baba yake. Binti huyo anapaswa kuchomwa moto.+ 10  “‘Kuhani mkuu miongoni mwa ndugu zake, aliyetiwa mafuta kichwani+ na kuwekwa rasmi ili avae mavazi ya kuhani,+ anapaswa kutunza nywele zake na hapaswi kurarua mavazi yake.+ 11  Hapaswi kumkaribia mtu yeyote aliyekufa;*+ hapaswi hata kujichafua kwa kumgusa baba yake au mama yake ambaye amekufa. 12  Hapaswi kuondoka mahali patakatifu wala kuchafua mahali patakatifu pa Mungu wake,+ kwa sababu ishara ya wakfu, yale mafuta ya Mungu wake yanayotumiwa kutia mafuta+ yako juu yake. Mimi ni Yehova. 13  “‘Ni lazima amwoe mwanamke ambaye ni bikira.+ 14  Hapaswi kuoa mwanamke mjane, mwanamke aliyetalikiwa, aliyenajisiwa, au kahaba; anapaswa kuoa mwanamke bikira miongoni mwa watu wake. 15  Hapaswi kuchafua uzao wake* kati ya watu wake,+ kwa sababu mimi ni Yehova, ninayemtakasa.’” 16  Yehova akaendelea kumwambia Musa: 17  “Mwambie hivi Haruni: ‘Mtu yeyote wa uzao wako* katika vizazi vyako vyote ambaye ana kasoro asikaribie mahali patakatifu ili kutoa mkate wa Mungu wake. 18  Mtu yeyote mwenye kasoro hapaswi kukaribia mahali patakatifu: mtu aliye kipofu au mlemavu au mwenye majeraha usoni* au mwenye kiungo kimoja kirefu zaidi, 19  au mtu aliyevunjika mguu au aliyevunjika mkono, 20  au kibyongo au mbilikimo,* au mtu mwenye jicho lililo na kasoro au mwenye ukurutu wa ngozi au mba au mwenye mapumbu yaliyoharibika.+ 21  Mtu yeyote wa uzao wa* kuhani Haruni ambaye ana kasoro hatakaribia mahali patakatifu ili kutoa dhabihu za Yehova zinazochomwa kwa moto. Kwa sababu ana kasoro, hapaswi kupakaribia ili kutoa mkate wa Mungu wake. 22  Anaweza kula mkate wa Mungu wake kutoka kati ya vitu vitakatifu kabisa+ na kutoka kati ya vitu vitakatifu.+ 23  Hata hivyo, hapaswi kukaribia pazia+ wala madhabahu,+ kwa sababu ana kasoro mwilini; naye hapaswi kuchafua mahali pangu patakatifu,+ kwa kuwa mimi ni Yehova, ninayewatakasa.’”+ 24  Basi Musa akawaambia Haruni na wanawe, na Waisraeli wote mambo hayo.

Maelezo ya Chini

Au “kuigusa nafsi iliyokufa.”
Au “chakula cha,” yaani, dhabihu.
Au “kuikaribia nafsi yoyote iliyokufa.”
Tnn., “mbegu yake.”
Tnn., “mbegu yako.”
Tnn., “pua iliyokatika.”
Au labda, “aliyekonda na kudhoofika.”
Tnn., “mbegu ya.”