Mambo ya Walawi 22:1-33

  • Utakatifu wa makuhani na ulaji wa vitu vitakatifu (1-16)

  • Dhabihu zisizo na kasoro ndizo zinazokubaliwa (17-33)

22  Yehova akaendelea kumwambia Musa:   “Mwambie Haruni na wanawe kwamba wanapaswa kuwa waangalifu kuhusu wanavyoshughulikia* vitu vitakatifu vya Waisraeli, nao wasichafue jina langu takatifu+ kuhusu vitu wanavyotakasa kwa ajili yangu.+ Mimi ni Yehova.  Waambie, ‘Katika vizazi vyenu vyote, mzao wenu yeyote asiye safi atakayekaribia vitu vitakatifu ambavyo Waisraeli wanavitakasa kwa ajili yangu, mimi, Yehova, ataangamizwa kutoka mbele zangu.+ Mimi ni Yehova.  Mzao yeyote wa Haruni mwenye ukoma+ au anayetokwa na umajimaji+ asile vitu vitakatifu mpaka atakapokuwa safi,+ wala mtu anayemgusa mtu yeyote aliyejichafua kwa kugusa mtu aliyekufa,*+ wala mtu anayetokwa na shahawa,+  wala mtu anayemgusa kiumbe asiye safi anayeishi kwenye makundi makubwa+ wala mtu anayemgusa mtu asiye safi kwa sababu yoyote ile ambaye anaweza kumchafua.+  Mtu anayegusa kitu chochote kati ya vitu hivyo hatakuwa safi mpaka jioni, naye hapaswi kula kitu chochote kitakatifu, badala yake anapaswa kuoga kwenye maji.+  Baada ya jua kutua, atakuwa safi, kisha anaweza kula baadhi ya vitu vitakatifu kwa sababu ni chakula chake.+  Pia, hapaswi kujichafua kwa kula mnyama yeyote aliyepatikana amekufa au kiumbe yeyote aliyeraruliwa na mnyama wa mwituni.+ Mimi ni Yehova.  “‘Ni lazima watimize wajibu wao mbele zangu, wasije wakatenda dhambi kwa kukosa kutimiza wajibu huo na hivyo kufa kwa sababu walikuwa wakiuchafua. Mimi ni Yehova, ninayewatakasa. 10  “‘Mtu asiye na idhini* haruhusiwi kula vitu vitakatifu.+ Hakuna mgeni wa kuhani au kibarua anayepaswa kula kitu chochote kitakatifu. 11  Lakini kuhani akimnunua mtu kwa pesa zake, mtu huyo anaweza kula vitu hivyo. Vilevile watumwa waliozaliwa katika nyumba yake wanaweza kula chakula chake.+ 12  Binti ya kuhani akiolewa na mwanamume ambaye si kuhani,* hapaswi kula vitu vitakatifu vilivyotolewa mchango. 13  Lakini binti ya kuhani akiwa mjane au akitalikiwa na hana mtoto, naye arudi nyumbani kwa baba yake alikoishi kabla hajaolewa, anaweza kula kiasi fulani cha chakula cha baba yake;+ lakini mtu yeyote asiye na idhini* hapaswi kula chakula hicho. 14  “‘Mtu akila kitu kitakatifu bila kujua, ni lazima alipie kitu hicho na kuongeza sehemu ya tano ya thamani yake na kumpa kuhani.+ 15  Kwa hiyo makuhani hawapaswi kuchafua vitu vitakatifu ambavyo Waisraeli wanamtolea Yehova mchango+ 16  na hivyo kufanya Waisraeli waadhibiwe kwa sababu ya hatia ya kula vitu vyao vitakatifu; kwa maana mimi ni Yehova, ninayewatakasa.’” 17  Yehova akaendelea kumwambia Musa: 18  “Waambie hivi Haruni na wanawe na Waisraeli wote: ‘Mwanamume Mwisraeli au mgeni katika Israeli anapomtolea Yehova dhabihu ya kuteketezwa+ ili kutimiza nadhiri zake au kutoa toleo la hiari,+ 19  anapaswa kutoa ng’ombe dume asiye na kasoro,+ wanakondoo dume, au mbuzi ili apate kibali. 20  Hampaswi kutoa kitu chochote chenye kasoro,+ kwa sababu hamtapata kibali mkifanya hivyo. 21  “‘Mtu akimtolea Yehova dhabihu ya ushirika+ ili kutimiza nadhiri au akiitoa ikiwa toleo la hiari, anapaswa kutoa mnyama asiye na kasoro kutoka katika mifugo yake au kundi lake, ili apate kibali. Mnyama huyo hapaswi kuwa na kasoro yoyote. 22  Hampaswi kumtoa dhabihu mnyama yeyote aliye kipofu, aliyevunjika, aliyekatwa, aliyejeruhiwa, mwenye uvimbe, vipele, au mba; hampaswi kumtolea Yehova yeyote kati ya wanyama hao au kumtolea Yehova dhabihu za aina hiyo kwenye madhabahu yake. 23  Mnaweza kumtoa ng’ombe dume au kondoo mwenye kiungo kimoja kirefu zaidi au kifupi sana kuwa toleo la hiari, lakini hatakubaliwa mkimtoa kuwa dhabihu ya nadhiri. 24  Hampaswi kumtolea Yehova mnyama mwenye mapumbu yaliyominywa au kupondwa au kung’olewa au kukatwa; hampaswi kuwatoa dhabihu wanyama wa aina hiyo katika nchi yenu. 25  Nanyi hampaswi kupokea wanyama wa aina hiyo kutoka kwa mgeni na kuwatoa kuwa dhabihu kwa* Mungu wenu, kwa sababu wana kasoro na ni walemavu. Hawatakubaliwa.’” 26  Yehova akaendelea kumwambia Musa: 27  “Ng’ombe dume au mwanakondoo dume au mbuzi akizaliwa, atakaa na mama yake kwa siku saba,+ lakini kuanzia siku ya nane atapokewa kwa kibali kuwa dhabihu, dhabihu kwa Yehova inayochomwa kwa moto. 28  Lakini hampaswi kumchinja ng’ombe dume au kondoo pamoja na watoto wake siku ileile.+ 29  “Mkimtolea Yehova dhabihu ya shukrani,+ mnapaswa kuitoa dhabihu hiyo ili mpate kibali chake. 30  Inapaswa kuliwa siku hiyohiyo. Hampaswi kuacha sehemu yoyote mpaka asubuhi.+ Mimi ni Yehova. 31  “Ni lazima mshike amri zangu na kuzifuata.+ Mimi ni Yehova. 32  Msilichafue jina langu takatifu,+ ni lazima nitakaswe miongoni mwa Waisraeli.+ Mimi ni Yehova, ninayewatakasa,+ 33  ninayewatoa katika nchi ya Misri ili nijithibitishe kuwa Mungu wenu.+ Mimi ni Yehova.”

Maelezo ya Chini

Tnn., “kuhusu jinsi wanavyopaswa kujitenga na.”
Au “nafsi iliyokufa.”
Tnn., “Mgeni,” yaani, mtu ambaye si wa familia ya Haruni.
Au “ni mgeni.”
Tnn., “mgeni yeyote,” yaani, mtu ambaye si wa familia ya Haruni.
Tnn., “mkate wa.”