Mambo ya Walawi 26:1-46

  • Epukeni ibada ya sanamu (1, 2)

  • Baraka za kuwa mtiifu (3-13)

  • Adhabu ya kukosa kutii (14-46)

26  “‘Msijitengenezee miungu ya ubatili+ wala sanamu ya kuchongwa+ au nguzo takatifu, nanyi msichonge sanamu ya mawe+ katika nchi yenu na kuiinamia;+ kwa maana mimi ni Yehova Mungu wenu.  Mnapaswa kushika sabato zangu na kuheshimu* mahali pangu patakatifu. Mimi ni Yehova.  “‘Mkiendelea kufuata sheria zangu na kushika amri zangu na kuzitekeleza,+  nitawaletea mvua katika majira yanayofaa,+ nayo nchi itazaa kwa wingi,+ na miti ya matunda itazaa matunda mengi.  Majira yenu ya kupura nafaka yataendelea mpaka wakati wa kuvuna zabibu, na wakati wa kuvuna zabibu utaendelea mpaka wakati wa kupanda; nanyi mtakula mkate na kushiba na kuishi kwa usalama katika nchi yenu.+  Nitaleta amani nchini,+ nanyi mtalala na hakuna yeyote atakayewaogopesha;+ nami nitawaondoa nchini wanyama wote wakali wa mwituni, na hakuna mtu yeyote atakayewashambulia kwa upanga katika nchi yenu.  Nanyi hakika mtawakimbiza maadui wenu na kuwaua kwa upanga.  Watu watano kati yenu watawakimbiza maadui 100, na 100 watawakimbiza 10,000; mtawaua maadui wenu kwa upanga.+  “‘Nitawabariki* na kuwafanya mzaane na kuongezeka,+ nami nitatimiza agano nililofanya pamoja nanyi.+ 10  Wakati wa mavuno mtakuwa bado mnakula mavuno ya zamani ya mwaka uliotangulia, mtahitaji kuondoa mavuno hayo ya zamani ili mpate nafasi ya mavuno mapya. 11  Nami nitaweka hema langu la ibada kati yenu,+ nami sitawakataa. 12  Nitatembea kati yenu na kuwa Mungu wenu,+ nanyi mtakuwa watu wangu.+ 13  Mimi ni Yehova Mungu wenu, niliyewatoa katika nchi ya Misri ili msiendelee kuwa watumwa wao, nami nikavunja nira yenu na kuwafanya mtembee vichwa vyenu vikiwa vimeinuliwa.* 14  “‘Lakini msiponisikiliza au kushika amri hizo zote,+ 15  mkikataa masharti yangu,+ mkichukia sheria zangu,* na kuvunja agano langu kwa kuacha kushika amri zangu zote,+ 16  basi, mimi nitawatendea mambo haya: nitawaadhibu kwa taabu, kwa kifua kikuu na homa kali, na kufanya macho yenu yadhoofike na uhai wenu uzorote.* Mtapanda mbegu zenu bure, kwa maana maadui wenu watazila.+ 17  Nitawakataa,* nanyi mtashindwa na maadui wenu;+ na wale wanaowachukia ninyi watawakanyaga-kanyaga,+ nanyi mtakimbia bila kukimbizwa na mtu.+ 18  “‘Hata mambo hayo yasipowafanya mnisikilize, nitalazimika kuwaadhibu mara saba zaidi kwa sababu ya dhambi zenu. 19  Nitakivunja kiburi chenu cha ukaidi na kufanya mbingu zenu ziwe kama chuma+ na nchi yenu kama shaba. 20  Mtapoteza nguvu zenu bure, kwa maana nchi yenu haitazaa mazao yake,+ na miti iliyo nchini haitazaa matunda. 21  “‘Lakini mkiendelea kunipinga na kukataa kunisikiliza, ndipo mimi nitalazimika kuwapiga mara saba zaidi, kulingana na dhambi zenu. 22  Nitaleta wanyama wa mwituni kati yenu,+ nao watawaua watoto wenu,+ wataangamiza mifugo yenu na kupunguza idadi yenu, na barabara zenu hazitakuwa na watu.+ 23  “‘Msipokubali nidhamu yangu+ licha ya mambo hayo, nanyi kwa ushupavu mtembee kwa kunipinga, 24  basi mimi pia nitawapinga, nami mwenyewe nitawapiga mara saba kwa sababu ya dhambi zenu. 25  Nitaleta dhidi yenu upanga unaolipiza kisasi kwa sababu ya kulivunja agano langu.+ Hata mkikusanyika katika majiji yenu, nitaleta magonjwa katikati yenu+ na kuwatia mikononi mwa adui.+ 26  Nitakapoharibu hifadhi yenu ya* mikate,+ wanawake kumi wataoka mikate kwenye jiko moja tu na kuwapimia mikate kwa mizani;+ nanyi mtakula lakini hamtashiba.+ 27  “‘Na ikiwa hamtanisikiliza, nanyi mkinipinga kwa ushupavu licha ya mambo hayo, 28  nitazidisha upinzani wangu dhidi yenu,+ na mimi mwenyewe nitawaadhibu mara saba kwa sababu ya dhambi zenu. 29  Basi mtalazimika kula nyama ya wana wenu na nyama ya mabinti wenu.+ 30  Nitaharibu mahali penu patakatifu palipo juu+ na kuvikatakata vinara vyenu vya uvumba, nami nitarundika mizoga yenu juu ya mizoga ya sanamu zenu zenye kuchukiza,*+ nami nitawachukia na kuwaacha.+ 31  Nitayaangamiza majiji yenu kwa upanga+ na kuharibu mahali penu patakatifu, nami sitasikia harufu inayopendeza* ya dhabihu zenu. 32  Mimi mwenyewe nitaifanya nchi yenu iwe ukiwa,+ na maadui wenu watakaoishi humo watashangazwa na hali yake.+ 33  Nitawatawanya miongoni mwa mataifa,+ nitachomoa upanga nanyi mtakimbizwa;+ na nchi yenu itaharibiwa, na majiji yenu yatabaki ukiwa.+ 34  “‘Wakati huo nchi italipa sabato zake siku zote itakapokuwa ukiwa, mtakapokuwa katika nchi ya maadui wenu. Wakati huo nchi itapumzika,* kwa maana ni lazima ilipe sabato zake.+ 35  Siku zote itakapokuwa ukiwa itapumzika, kwa sababu haikupumzika wakati wa sabato zenu mlipokuwa mkiishi humo. 36  “‘Nitajaza hisia ya kukata tamaa mioyoni mwa wale watakaobaki+ katika nchi za maadui wao; na sauti ya jani linalopeperushwa na upepo itawafanya wakimbie, nao watakimbia kama mtu anayeukimbia upanga na kuanguka bila kukimbizwa na yeyote.+ 37  Watajikwaa na kuangukiana kama watu wanaokimbia upanga, hata ingawa hakuna anayewakimbiza. Hamtaweza kuwashinda maadui wenu.+ 38  Mtaangamia miongoni mwa mataifa,+ na nchi ya maadui wenu itawala. 39  Wale watakaobaki wataachwa waoze katika nchi za maadui wenu+ kwa sababu ya dhambi zenu. Naam, wataozea huko kwa sababu ya dhambi za baba zao.+ 40  Kisha wataungama dhambi zao,+ wataungama pia dhambi na ukosefu wa uaminifu wa baba zao, nao watakiri kwamba hawakuwa waaminifu waliponipinga mimi.+ 41  Basi nikalazimika kuwapinga+ kwa kuwapeleka katika nchi ya maadui wao.+ “‘Nilifanya hivyo ili mioyo yao mikaidi* inyenyekee,+ na ili walipie dhambi zao. 42  Nitakumbuka agano langu na Yakobo,+ na agano langu na Isaka,+ na pia agano langu na Abrahamu,+ nami nitaikumbuka nchi yao. 43  Walipokuwa wameiacha nchi yao, ilikuwa ikilipa sabato zake+ na kukaa ukiwa bila mtu yeyote, nao walikuwa wakilipia dhambi zao, kwa sababu walikataa amri zangu na kuchukia sheria zangu.+ 44  Lakini licha ya hayo yote, wakiwa katika nchi ya maadui wao, sitawakataa kabisa+ wala sitawatupa na kuwaangamiza kabisa na hivyo kulivunja agano nililofanya+ pamoja nao; kwa maana mimi ni Yehova Mungu wao. 45  Kwa ajili yao nitalikumbuka agano nililofanya na mababu zao+ niliowatoa nchini Misri mataifa yakishuhudia,+ ili nijithibitishe mwenyewe kuwa Mungu wao. Mimi ni Yehova.’” 46  Hayo ndiyo masharti, amri, na sheria ambazo Yehova aliwapa Waisraeli kwenye Mlima Sinai kupitia Musa.+

Maelezo ya Chini

Au “kuogopa.”
Au “Nitawakazia fikira.”
Tnn., “mtembee wima.”
Tnn., “maamuzi yangu ya hukumu.”
Au “nafsi yenu izorote.”
Tnn., “Nitaukaza uso wangu dhidi yenu.”
Tnn., “fito zenu za.” Labda ni fito zilizotumiwa kuhifadhia mikate.
Huenda neno la Kiebrania linahusiana na neno “mavi,” nalo hutumiwa kuonyesha dharau.
Au “inayotuliza.”
Au “itashika sabato.”
Tnn., “mioyo yao ambayo haijatahiriwa.”