Mambo ya Walawi 3:1-17

  • Dhabihu ya ushirika (1-17)

    • Msile mafuta wala damu (17)

3  “‘Ikiwa mtu anatoa dhabihu ya ushirika*+ na dhabihu hiyo inatoka kati ya mifugo, awe ni mnyama dume au jike, anapaswa kumtolea Yehova mnyama asiye na kasoro.  Anapaswa kuweka mkono wake juu ya kichwa cha mnyama huyo, naye atachinjwa kwenye mlango wa hema la mkutano; kisha wana wa Haruni, makuhani, watanyunyiza damu yake pande zote za madhabahu.  Atatoa sehemu ya dhabihu hiyo ya ushirika kuwa dhabihu kwa Yehova+ inayochomwa kwa moto, yaani, mafuta+ yanayofunika matumbo, naam, mafuta yote yaliyo juu ya matumbo,  na figo zake mbili pamoja na mafuta yake yaliyo karibu na kiuno. Ataondoa pia figo pamoja na mafuta yaliyo juu ya ini.+  Wana wa Haruni watateketeza vitu hivyo kwenye madhabahu juu ya dhabihu ya kuteketezwa iliyo kwenye kuni zinazowaka moto ili vifuke moshi;+ ni dhabihu inayochomwa kwa moto yenye harufu inayompendeza* Yehova.+  “‘Ikiwa mtu anamtolea Yehova dhabihu ya ushirika kutoka kati ya kundi lake, anapaswa kutoa mnyama dume au jike asiye na kasoro.+  Ikiwa anatoa kondoo dume mchanga, atamtoa mbele za Yehova.  Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha mnyama huyo, naye atachinjwa mbele ya hema la mkutano. Kisha wana wa Haruni, makuhani, watanyunyiza damu yake pande zote za madhabahu.  Atayatoa mafuta kutoka kwenye dhabihu ya ushirika yawe dhabihu kwa Yehova inayochomwa kwa moto.+ Atakata mkia wote wenye mafuta karibu na uti wa mgongo, ataondoa mafuta yanayofunika matumbo, naam, mafuta yote yaliyo juu ya matumbo, 10  na figo zake mbili pamoja na mafuta yake yaliyo karibu na kiuno. Ataondoa pia figo pamoja na mafuta yaliyo juu ya ini.+ 11  Naye kuhani ataviteketeza vitu hivyo kwenye madhabahu kama chakula* ili vifuke moshi. Ni dhabihu kwa Yehova inayochomwa kwa moto.+ 12  “‘Ikiwa mtu anatoa mbuzi, atamtoa mbele za Yehova. 13  Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha mbuzi huyo, naye atachinjwa mbele ya hema la mkutano, nao wana wa Haruni watanyunyiza damu yake pande zote za madhabahu. 14  Atamtolea Yehova mafuta yanayofunika matumbo, naam, mafuta yote yaliyo juu ya matumbo kuwa dhabihu inayochomwa kwa moto,+ 15  pamoja na figo zake mbili na mafuta yake yaliyo karibu na kiuno. Ataondoa pia figo pamoja na mafuta yaliyo juu ya ini. 16  Kuhani ataviteketeza vitu hivyo kwenye madhabahu kama chakula* ili vifuke moshi, ni dhabihu inayochomwa kwa moto yenye harufu inayopendeza.* Mafuta yote ni ya Yehova.+ 17  “‘Ni sheria ya kudumu kwa vizazi vyenu, katika makao yenu yote: Msile mafuta yoyote wala damu+ yoyote.’”

Maelezo ya Chini

Au “dhabihu ya matoleo ya amani.”
Au “inayomtuliza.”
Tnn., “mkate,” yaani, sehemu ya Mungu ya dhabihu ya ushirika.
Tnn., “mkate,” yaani, sehemu ya Mungu ya dhabihu ya ushirika.
Au “inayotuliza.”