Mambo ya Walawi 5:1-19

  • Dhambi hususa na dhabihu zilizohitaji kutolewa (1-6)

    • Kutoa habari kuhusu dhambi za wengine (1)

  • Dhabihu ambazo zingeweza kutolewa na maskini (7-13)

  • Dhabihu ya hatia kwa ajili ya dhambi zilizotendwa bila kukusudia (14-19)

5  “‘Ikiwa mtu amesikia mwito wa hadharani wa kutoa ushahidi*+ kuhusu jambo ambalo amejionea au kusikia au kujua, lakini amekataa kutoa habari, basi ametenda dhambi, naye atawajibika kwa sababu ya kosa lake.  “‘Au mtu akigusa kitu chochote kisicho safi, iwe ni mzoga wa mnyama wa mwituni, mzoga wa mnyama wa kufugwa, au viumbe wanaoishi katika makundi makubwa,+ hatakuwa safi na atakuwa na hatia hata kama hajui jambo hilo.  Au mtu akigusa uchafu wa mwanadamu bila kujua+—kitu chochote kisicho safi kinachoweza kumchafua—atakuwa na hatia atakapojua jambo hilo.  “‘Au mtu akiapa kufanya jambo fulani bila kufikiri—jambo lolote lile, jema au baya—lakini baadaye atambue kwamba ameapa bila kufikiri, atakuwa na hatia atakapojua jambo hilo.*+  “‘Ikiwa ana hatia katika jambo lolote kati ya mambo hayo, basi ni lazima aungame+ dhambi aliyotenda.  Pia atamletea Yehova dhabihu ya hatia kwa ajili ya dhambi aliyotenda;+ ataleta mnyama jike kutoka katika kundi, yaani, mwanakondoo jike au mwanambuzi jike, ili awe dhabihu ya dhambi. Kisha kuhani atamtolea dhabihu ya kufunika dhambi yake.  “‘Hata hivyo, ikiwa hawezi kutoa kondoo, atamletea Yehova njiwa tetere wawili au hua wawili wachanga+ wawe dhabihu ya hatia kwa ajili ya dhambi yake, ndege mmoja kwa ajili ya dhabihu ya dhambi, na mwingine kwa ajili ya dhabihu ya kuteketezwa.+  Atawaleta kwa kuhani, naye kuhani atatoa ndege mmoja kwanza kwa ajili ya dhabihu ya dhambi, atamvunja shingo na kuacha kichwa kikining’inia.  Atanyunyiza kiasi kidogo cha damu ya dhabihu hiyo ya dhambi kando ya madhabahu, lakini damu inayobaki itamwagwa kwenye msingi wa madhabahu.+ Ni dhabihu ya dhambi. 10  Atamtoa ndege wa pili kuwa dhabihu ya kuteketezwa akifuata utaratibu wa kawaida;+ naye kuhani atamtolea dhabihu ya kufunika dhambi aliyotenda, naye atasamehewa.+ 11  “‘Ikiwa hawezi kutoa njiwa tetere wawili au hua wawili wachanga, basi atatoa sehemu ya kumi ya kipimo cha efa moja*+ ya unga laini ili kuwa dhabihu ya dhambi. Hapaswi kuutia mafuta au ubani kwa sababu ni dhabihu ya dhambi. 12  Atauleta kwa kuhani, naye kuhani atachukua mkono mmoja wa unga huo ukiwa dhabihu ya kumbukumbu* naye atauweka kwenye madhabahu juu ya dhabihu za Yehova zinazochomwa kwa moto ili ufuke moshi. Ni dhabihu ya dhambi. 13  Kuhani atamtolea dhabihu ya kufunika dhambi aliyotenda, yoyote kati ya dhambi hizo, naye atasamehewa.+ Sehemu inayobaki ya dhabihu hiyo itakuwa ya kuhani,+ sawa na sehemu inayobaki ya toleo la nafaka.’”+ 14  Yehova akaendelea kumwambia Musa: 15  “Mtu akikosa uaminifu kwa kutenda dhambi bila kukusudia kwa kuvunja sheria kuhusu vitu vitakatifu vya Yehova,+ anapaswa kumletea Yehova kondoo dume asiye na kasoro kutoka kundini ili awe dhabihu ya hatia;+ thamani yake itapimwa kwa shekeli za fedha* kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu.*+ 16  Naye atalipia dhambi aliyotenda dhidi ya mahali patakatifu na pia ataongeza sehemu ya tano ya thamani ya vitu hivyo.+ Atampa kuhani, ili kuhani amtolee dhabihu ya kufunika dhambi+ yake akitumia kondoo dume wa dhabihu ya hatia, naye atasamehewa.+ 17  “Mtu akitenda dhambi kwa kufanya jambo lolote ambalo Yehova ameamuru lisifanywe, hata kama hajui, bado ana hatia naye atawajibika kwa sababu ya kosa lake.+ 18  Anapaswa kumletea kuhani kondoo dume asiye na kasoro kutoka kundini kulingana na thamani iliyokadiriwa, kwa ajili ya dhabihu ya hatia.+ Kisha kuhani atamtolea dhabihu ya kufunika kosa alilofanya bila kukusudia na bila kujua, naye atasamehewa. 19  Ni dhabihu ya hatia. Bila shaka ana hatia ya kumtendea dhambi Yehova.”

Maelezo ya Chini

Tnn., “amesikia laana (kiapo).” Labda anasikia tangazo kuhusu kosa lililofanywa na laana itakayompata mkosaji au shahidi yeyote anayekataa kutoa ushahidi.
Inaonekana mtu huyo hatimizi kiapo chake.
Sehemu ya kumi ya efa ilikuwa sawa na lita 2.2 au kilogramu 1.3 hivi. Angalia Nyongeza B14.
Au “ukiwa sehemu ya ukumbusho (uwakilishi) wake.”
Shekeli moja ilikuwa na uzito wa gramu 11.4. Angalia Nyongeza B14.
Au “shekeli takatifu.”