Mambo ya Walawi 6:1-30

  • Habari zaidi kuhusu dhabihu ya hatia (1-7)

  • Maagizo kuhusu dhabihu (8-30)

    • Dhabihu ya kuteketezwa (8-13)

    • Toleo la nafaka (14-23)

    • Dhabihu ya dhambi (24-30)

6  Yehova akaendelea kumwambia Musa:  “Mtu akitenda dhambi na kukosa uaminifu kwa Yehova+ kwa kumdanganya jirani yake kuhusu kitu fulani alichokabidhiwa atunze,+ au alichoachiwa kama dhamana, au akimwibia au kumlaghai jirani yake,  au akipata kitu kilichopotea na kudanganya kwamba hajakipata, naye akiapa kwa uwongo kuhusu dhambi yoyote kama hiyo ambayo huenda akatenda,+ anapaswa kufanya hivi:  Ikiwa ametenda dhambi naye ana hatia, ni lazima arudishe kitu alichoiba, kitu alichochukua kwa nguvu, kitu alichochukua kwa ulaghai, kitu alichokabidhiwa atunze, au kitu kilichopotea akakipata,  au chochote alichoapia kwa uwongo, ni lazima alipe kitu hicho kikamili+ na kuongeza sehemu ya tano ya thamani yake. Atamrudishia mwenyewe kitu hicho siku ambayo hatia yake itajulikana.  Naye atamletea kuhani kondoo dume asiye na kasoro kutoka kundini ili amtolee Yehova dhabihu ya hatia kulingana na thamani iliyokadiriwa ya dhabihu ya hatia.+  Kuhani atamtolea dhabihu ya kufunika dhambi yake mbele za Yehova, naye atasamehewa kosa lolote ambalo lilifanya awe na hatia.”+  Yehova akaendelea kumwambia Musa:  “Mwamuru hivi Haruni na wanawe: ‘Hii ndiyo sheria kuhusu dhabihu ya kuteketezwa:+ Dhabihu ya kuteketezwa itakaa usiku kucha motoni juu ya madhabahu mpaka asubuhi, hakikisheni kwamba moto wa madhabahu unaendelea kuwaka. 10  Kuhani atavaa vazi lake rasmi la kitani+ na suruali fupi ya kitani.*+ Kisha ataondoa majivu*+ ya dhabihu iliyoteketezwa kwenye madhabahu na kuyaweka kando ya madhabahu. 11  Halafu atavua mavazi hayo+ na kuvaa mengine, naye atapeleka majivu hayo mahali safi nje ya kambi.+ 12  Ni lazima moto wa madhabahu uendelee kuwaka. Haupaswi kuzimika. Kila asubuhi kuhani ataongeza kuni+ kwenye moto huo na kupanga dhabihu ya kuteketezwa juu yake, naye atateketeza mafuta ya dhabihu za ushirika ili yafuke moshi.+ 13  Hakikisheni kwamba moto unaendelea kuwaka daima kwenye madhabahu. Haupaswi kuzimika. 14  “‘Hii ndiyo sheria kuhusu toleo la nafaka:+ Ninyi wana wa Haruni mtamtolea Yehova toleo hilo mbele ya madhabahu. 15  Mmoja wenu atachukua mkono mmoja wa unga laini wa toleo la nafaka na kiasi fulani cha mafuta yake na ubani wote ulio katika toleo la nafaka, naye atauteketeza ili ufuke moshi kwenye madhabahu kama harufu ya kupendeza* ya dhabihu ya kumbukumbu* kwa Yehova.+ 16  Haruni na wanawe watatumia unga unaobaki+ kuoka mikate isiyo na chachu, nao watakula mikate hiyo mahali patakatifu. Wataila katika ua wa hema la mkutano.+ 17  Haipaswi kuokwa pamoja na kitu chochote chenye chachu.+ Nimewapa liwe fungu lao kutoka katika matoleo yangu yanayochomwa kwa moto.+ Ni toleo takatifu kabisa,+ kama ilivyo dhabihu ya dhambi na dhabihu ya hatia. 18  Kila mzao wa kiume wa Haruni ataila.+ Ni posho yao ya kudumu katika vizazi vyenu vyote kutoka kwa matoleo ya Yehova yanayochomwa kwa moto.+ Chochote kinachogusa matoleo hayo kitakuwa kitakatifu.’” 19  Yehova akaendelea kumwambia Musa: 20  “Hivi ndivyo vitu ambavyo Haruni na wanawe watamtolea Yehova siku ambayo Haruni atatiwa mafuta:+ sehemu ya kumi ya kipimo cha efa moja*+ ya unga laini kama toleo la kawaida la nafaka,+ nusu ya unga huo asubuhi na nusu nyingine jioni. 21  Utachanganywa na mafuta na kuokwa kwenye kiokeo.+ Mtaukanda vizuri kabisa kwa mafuta na kuuleta ukiwa vitumbua vya toleo la nafaka lenye harufu inayompendeza* Yehova. 22  Mwana wa Haruni atakayetiwa mafuta ili kuwa kuhani baada yake+ atatoa toleo hilo. Ni sheria ya kudumu: Kwa kuwa toleo hilo linatolewa kwa Yehova likiwa zima litateketezwa ili moshi ufuke mbele zake. 23  Kila toleo la nafaka la kuhani linapaswa kuwa toleo zima. Halipaswi kuliwa.” 24  Yehova akaendelea kumwambia Musa: 25  “Mwambie hivi Haruni na wanawe: ‘Hii ndiyo sheria kuhusu dhabihu ya dhambi:+ Mnyama wa dhabihu ya dhambi atachinjiwa+ mahali ambapo mnyama wa dhabihu ya kuteketezwa huchinjwa mbele za Yehova. Ni dhabihu takatifu kabisa. 26  Kuhani anayetoa dhabihu hiyo kwa ajili ya dhambi ataila.+ Ataila mahali patakatifu katika ua wa hema la mkutano.+ 27  “‘Kila kitu kinachogusa nyama hiyo kitakuwa kitakatifu, na vazi la mtu yeyote likidondokewa na damu ya mnyama huyo, mtalifua vazi hilo mahali patakatifu. 28  Chombo cha udongo kilichotumiwa kuchemshia nyama hiyo kitavunjwavunjwa. Lakini ikiwa ilichemshiwa katika chombo cha shaba, basi lazima chombo hicho kisuguliwe na kusafishwa kwa maji. 29  “‘Kila mwanamume kuhani ataila.+ Ni takatifu kabisa.+ 30  Lakini kila dhabihu ya dhambi ambayo kiasi fulani cha damu yake kimeletwa mahali patakatifu kwenye hema la mkutano ili kufunika dhambi, haitaliwa.+ Itateketezwa.

Maelezo ya Chini

Au “majivu yenye mafuta,” yaani, majivu yaliyojaa mafuta ya dhabihu.
Au “suruali ya ndani.”
Au “inayotuliza.”
Au “ukiwa sehemu ya ukumbusho (uwakilishi) wake.”
Sehemu ya kumi ya efa ilikuwa sawa na lita 2.2 au kilogramu 1.3 hivi. Angalia Nyongeza B14.
Au “inayomtuliza.”