Mambo ya Walawi 7:1-38

  • Maagizo kuhusu dhabihu (1-21)

    • Dhabihu ya hatia (1-10)

    • Dhabihu ya ushirika (11-21)

  • Wakatazwa kula mafuta au damu (22-27)

  • Fungu la kuhani (28-36)

  • Orodha ya dhabihu mbalimbali (37, 38)

7  “‘Hii ndiyo sheria kuhusu dhabihu ya hatia:+ Ni dhabihu takatifu kabisa.  Mnyama wa dhabihu ya hatia atachinjiwa mahali ambapo dhabihu za kuteketezwa huchinjwa, na damu yake+ itanyunyizwa pande zote za madhabahu.+  Kuhani atatoa mafuta yote+ ya mnyama huyo pamoja na mkia wake wenye mafuta, mafuta yanayofunika matumbo,  na figo zake mbili pamoja na mafuta yake yaliyo karibu na kiuno. Ataondoa pia figo pamoja na mafuta yaliyo juu ya ini.+  Kuhani ataviteketeza vitu hivyo kwenye madhabahu ili vifuke moshi vikiwa dhabihu kwa Yehova inayochomwa kwa moto.+ Ni dhabihu ya hatia.  Kila mwanamume kuhani ataila,+ nayo inapaswa kuliwa mahali patakatifu. Ni dhabihu takatifu kabisa.+  Sheria kuhusu dhabihu ya dhambi ni sawa na sheria kuhusu dhabihu ya hatia; dhabihu hiyo ni ya kuhani aliyeitoa kufunika dhambi.+  “‘Kuhani akitoa dhabihu ya kuteketezwa kwa ajili ya mtu, ngozi+ ya mnyama aliyeletwa kwa ajili ya dhabihu ya kuteketezwa itakuwa ya kuhani huyo.  “‘Kila toleo la nafaka linalookwa kwenye jiko au kikaangio au kiokeo+ ni la kuhani anayelitoa. Litakuwa lake.+ 10  Lakini kila toleo la nafaka linalochanganywa na mafuta+ au lililo kavu+ litakuwa la wana wote wa Haruni; kila mmoja wao atapokea kiasi kilekile. 11  “‘Sasa hii ndio sheria ya dhabihu ya ushirika+ ambayo mtu yeyote anaweza kumtolea Yehova: 12  Ikiwa anaitoa ili kuonyesha shukrani,+ ataitoa dhabihu hiyo ya shukrani pamoja na mikate ya mviringo isiyo na chachu na iliyokandwa kwa mafuta, mikate myembamba isiyo na chachu na ambayo imepakwa mafuta, na mikate ya mviringo iliyookwa kwa unga laini uliochanganywa vizuri kabisa na kukandwa kwa mafuta. 13  Atatoa dhabihu yake pamoja na mikate ya mviringo iliyotiwa chachu na dhabihu ya shukrani ya dhabihu zake za ushirika. 14  Atatoa mkate mmoja kutoka katika kila toleo kuwa fungu takatifu kwa Yehova; litakuwa la kuhani anayenyunyiza damu ya dhabihu za ushirika.+ 15  Nyama za dhabihu za ushirika zinazotolewa ili kuonyesha shukrani zinapaswa kuliwa siku ambayo dhabihu hiyo ya shukrani inatolewa. Nyama yoyote ya dhabihu hiyo haipaswi kuachwa mpaka asubuhi.+ 16  “‘Ikiwa dhabihu anayotoa ni kwa ajili ya nadhiri+ au ni toleo la hiari,+ inapaswa kuliwa siku ambayo anatoa dhabihu hiyo, na nyama inayobaki inaweza pia kuliwa siku inayofuata. 17  Lakini nyama yoyote inayobaki ya dhabihu hiyo inapaswa kuteketezwa siku ya tatu.+ 18  Hata hivyo, nyama yoyote ya dhabihu ya ushirika ikiliwa siku ya tatu, yule anayeitoa hatapata kibali. Haitamnufaisha; ni dhabihu inayochukiza, na mtu anayeila ataadhibiwa kwa sababu ya kosa lake.+ 19  Nyama inayogusa kitu chochote kisicho safi haipaswi kuliwa. Itateketezwa kwa moto. Mtu yeyote aliye safi anaweza kula nyama iliyo safi. 20  “‘Lakini mtu yeyote asiye safi akila nyama ya dhabihu ya ushirika, ambayo ni ya Yehova, ni lazima auawe.+ 21  Mtu yeyote akigusa kitu chochote kisicho safi, iwe ni uchafu wa mwanadamu+ au mnyama asiye safi+ au kitu chochote chenye kuchukiza kisicho safi,+ kisha ale nyama ya dhabihu ya ushirika, ambayo ni ya Yehova, ni lazima auawe.’” 22  Yehova akaendelea kumwambia Musa: 23  “Waambie Waisraeli, ‘Hampaswi kula mafuta yoyote+ ya ng’ombe dume au ya mwanakondoo dume au ya mbuzi. 24  Mafuta ya mnyama aliyepatikana amekufa na mafuta ya mnyama aliyeuawa na mnyama mwingine, yanaweza kutumiwa kwa kusudi lingine lolote, lakini hampaswi kamwe kuyala.+ 25  Kwa maana mtu yeyote anayekula mafuta ya mnyama anayemtoa kuwa dhabihu kwa Yehova inayochomwa kwa moto, ni lazima auawe. 26  “‘Hampaswi kula damu yoyote+ mahali popote mnapoishi, iwe ni damu ya ndege au ya mnyama. 27  Mtu yeyote anayekula damu ni lazima auawe.’”+ 28  Yehova akaendelea kumwambia Musa: 29  “Waambie Waisraeli, ‘Mtu yeyote anayemletea Yehova dhabihu yake ya ushirika atamtolea Yehova sehemu ya dhabihu hiyo.+ 30  Ataleta mafuta+ pamoja na kidari kwa mikono yake mwenyewe ili vitu hivyo viwe dhabihu kwa Yehova inayochomwa kwa moto, naye atavitikisa kwenda mbele na nyuma vikiwa toleo la kutikiswa+ mbele za Yehova. 31  Kuhani atayateketeza mafuta hayo kwenye madhabahu ili yafuke moshi,+ lakini kidari kitakuwa cha Haruni na wanawe.+ 32  “‘Mtampa kuhani mguu wa kulia kutoka katika dhabihu zenu za ushirika ukiwa fungu takatifu.+ 33  Mguu wa kulia utakuwa fungu la mwana wa Haruni atakayetoa damu ya dhabihu za ushirika na mafuta.+ 34  Kwa maana nachukua kidari cha toleo la kutikiswa na mguu wa lile fungu takatifu kutoka kwa dhabihu za ushirika za Waisraeli na kumpa kuhani Haruni na wanawe. Ni sheria ya kudumu kwa Waisraeli.+ 35  “‘Hilo ndilo fungu lililotengwa kwa ajili ya makuhani, yaani, Haruni na wanawe, kutoka katika dhabihu za Yehova zinazochomwa kwa moto, fungu lililotengwa kwa ajili yao siku waliyowekwa rasmi kumtumikia Yehova wakiwa makuhani.+ 36  Yehova aliwaamuru Waisraeli wawape makuhani fungu hilo siku alipowatia mafuta.+ Ni sheria ya kudumu katika vizazi vyao.’” 37  Hizo ndizo sheria kuhusu dhabihu ya kuteketezwa,+ toleo la nafaka,+ dhabihu ya dhambi,+ dhabihu ya hatia,+ dhabihu ya kuwaweka rasmi makuhani,+ na dhabihu ya ushirika,+ 38  kama Yehova alivyomwamuru Musa kwenye Mlima Sinai+ siku aliyowaamuru Waisraeli wamtolee Yehova dhabihu zao katika nyika ya Sinai.+

Maelezo ya Chini