Maombolezo 2:1-22

  • Hasira ya Yehova dhidi ya Yerusalemu

    • Hakulihurumia (2)

    • Yehova ni kama adui yake (5)

    • Machozi yamwagwa kwa ajili ya Sayuni (11-13)

    • Wapita njia walidharau jiji lililokuwa maridadi awali (15)

    • Maadui washangilia kuanguka kwa Sayuni (17)

א [Aleph] 2  Jinsi Yehova alivyomfunika binti ya Sayuni katika wingu la hasira yake! Ameutupa chini urembo wa Israeli kutoka mbinguni mpaka duniani.+ Hajakumbuka kiti cha miguu yake+ katika siku ya hasira yake. ב [Beth]   Yehova ameyameza makao yote ya Yakobo bila huruma. Katika hasira yake amebomoa ngome za binti ya Yuda.+ Ameushusha chini ardhini na kuuchafua ufalme+ na wakuu wake.+ ג [Gimel]   Kwa hasira kali amezikata nguvu zote za* Israeli. Aliuondoa mkono wake wa kuume adui alipokaribia,+Na katika Yakobo aliendelea kuwaka kama moto ulioteketeza kila kitu kilicho karibu.+ ד [Daleth]   Ameukunja* upinde wake kama adui; mkono wake wa kuume uko tayari kama adui;+Aliendelea kuwaua wote wanaotamanika machoni.+ Naye aliimwaga ghadhabu yake kama moto+ katika hema la binti ya Sayuni.+ ה [He]   Yehova amekuwa kama adui;+Ameimeza Israeli. Ameimeza minara yake yote;Ameziharibu ngome zake zote. Na katika binti ya Yuda anafanya maombolezo na kilio kiwe kingi. ו [Waw]   Anakitendea kwa ukatili kibanda chake,+ kama kibanda kilicho katika bustani. Amekomesha* sherehe yake.+ Yehova amesababisha sherehe na sabato zisahauliwe Sayuni,Na kwa ghadhabu yake kali hamheshimu mfalme na kuhani.+ ז [Zayin]   Yehova ameikataa madhabahu yake;Amedharau mahali pake patakatifu.+ Amesalimisha kuta za minara yake yenye ngome mikononi mwa adui.+ Wameinua sauti yao ndani ya nyumba ya Yehova,+ kama inavyokuwa siku ya sherehe. ח [Heth]   Yehova ameazimia kuuharibu ukuta wa binti ya Sayuni.+ Ameinyoosha kamba ya kupimia.+ Hajauzuia mkono wake usilete maangamizi.* Naye husababisha maboma na kuta ziomboleze. Zote pamoja zimedhoofishwa. ט [Teth]   Malango yake yamezama chini ardhini.+ Ameyaharibu na kuyavunja makomeo yake. Mfalme wake na wakuu wake wako miongoni mwa mataifa.+ Hakuna sheria;* hata manabii wake hawapati maono kutoka kwa Yehova.+ י [Yod] 10  Wazee wa binti ya Sayuni wanaketi ardhini wakiwa kimya.+ Wanarusha mavumbi vichwani mwao na kuvaa nguo za magunia.+ Mabikira wa Yerusalemu wameinamisha vichwa vyao mpaka ardhini. כ [Kaph] 11  Macho yangu yamechoka kabisa kwa sababu ya kumwaga machozi.+ Matumbo yangu yanasukasuka. Ini langu limemwagika ardhini, kwa sababu ya kuanguka kwa binti ya* watu wangu,+Kwa sababu ya watoto wadogo na watoto wanaonyonya wanaozimia kwenye viwanja vya mji.+ ל [Lamed] 12  Wanaendelea kuwauliza mama zao, “Iko wapi nafaka na divai?”+ Wanapozimia kama mtu aliyejeruhiwa katika viwanja vya mji,Huku uhai wao ukitoka polepole wakiwa mikononi mwa mama zao. מ [Mem] 13  Ninaweza kutumia nini kama ushahidi,Au ninaweza kukufananisha na nini, Ee binti ya Yerusalemu? Ninaweza kukulinganisha na nini, ili nikufariji, Ee bikira binti ya Sayuni? Kwa maana jeraha lako* ni kubwa kama bahari.+ Ni nani anayeweza kukuponya?+ נ [Nun] 14  Maono ambayo manabii wako waliona kwa ajili yako yalikuwa ya uwongo na yasiyofaa kitu,+Nao hawakufunua kosa lako ili kuzuia usipelekwe utekwani,+Bali waliendelea kukupa maono yenye ujumbe wa uwongo na unaopotosha.+ ס [Samekh] 15  Wote wanaopita barabarani wanakupigia makofi kwa dharau.+ Wanapiga mluzi kwa mshangao+ na kumtikisia vichwa vyao binti ya Yerusalemu, wakisema: “Je, hili ndilo jiji walilosema hivi kulihusu: ‘Lina urembo mkamilifu, ni shangwe ya dunia yote’?”+ פ [Pe] 16  Maadui wako wote wamefungua kinywa chao dhidi yako. Wanapiga mluzi na kusaga meno yao wakisema: “Tumemmeza.+ Hii ndiyo siku tuliyokuwa tukiingojea!+ Imefika, nasi tumeiona!”+ ע [Ayin] 17  Yehova ametenda alilokusudia;+ ametekeleza neno lake,+Aliloamuru zamani za kale.+ Amebomoa bila huruma.+ Amemruhusu adui ashangilie msiba wako; amezikweza nguvu za* wapinzani wako. צ [Tsade] 18  Moyo wao unamlilia Yehova kwa sauti, Ee ukuta wa binti ya Sayuni. Machozi na yatiririke kama mto mchana na usiku. Usipumzike, macho yako yasiache kulia.* ק [Qoph] 19  Inuka! Lia kwa sauti wakati wa usiku, mwanzoni mwa makesha ya usiku. Umwage moyo wako kama maji mbele za uso wa Yehova. Mwinulie mikono yako kwa ajili ya uhai wa* watoto wako,Wanaozimia kwenye kila pembe ya barabara kwa sababu ya njaa kali.+ ר [Resh] 20  Tazama, Ee Yehova, umwone yule uliyemtesa vikali. Je, wanawake wanapaswa kuendelea kula uzao wao wenyewe, watoto wao wenyewe waliokomaa,+Au, je, makuhani na manabii wanapaswa kuuawa mahali patakatifu pa Yehova?+ ש [Shin] 21  Mvulana na mwanamume mzee wamelala chini barabarani wakiwa wamekufa.+ Mabikira* wangu na vijana wangu wa kiume wameuawa kwa upanga.+ Umeua katika siku ya hasira yako; umechinja bila huruma.+ ת [Taw] 22  Unakusanya vitisho kutoka kila upande kana kwamba ni siku ya sherehe.+ Katika siku ya ghadhabu ya Yehova, hakuna yeyote aliyeponyoka wala kuokoka;+Wale niliowazaa* na kuwalea, adui yangu aliwaangamiza kabisa.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “ameikata kila pembe ya.”
Tnn., “Ameukanyaga.”
Au “Ameharibu.”
Tnn., “usimeze.”
Au “mafundisho.”
Mfano wa kishairi ambao huenda unaonyesha huruma au sikitiko.
Au “jeraha lako la kuvunjika.”
Tnn., “ameikweza pembe ya.”
Tnn., “binti ya jicho lako asipumzike.”
Au “nafsi za.”
Au “Wanawali.”
Au “niliowazaa wakiwa na afya.”