Maombolezo 3:1-66

  • Yeremia aeleza hisia na matumaini yake

    • “Nitaonyesha mtazamo wa kungojea” (21)

    • Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi (22, 23)

    • Mungu ni mwema kwa wale wanaomtumaini (25)

    • Ni jambo jema kwa vijana kubeba nira (27)

    • Mungu aziba kwa wingu njia ya kumkaribia (43, 44)

א [Aleph] 3  Mimi ndiye mwanamume aliyepata mateso kwa sababu ya fimbo ya ghadhabu yake.   Amenifukuza, naye hunifanya nitembee gizani, si nuruni.+   Kwa kweli, yeye huniadhibu tena na tena kwa mkono wake mchana kutwa.+ ב [Beth]   Ameudhoofisha mwili wangu na ngozi yangu;Ameivunja mifupa yangu.   Amenizingira; amenizungushia sumu+ kali na taabu.   Amenilazimisha niketi katika sehemu zenye giza, kama watu waliokufa zamani za kale. ג [Gimel]   Amenizungushia ukuta, hivi kwamba siwezi kutoroka;Amenifunga kwa pingu nzito za shaba.+   Na ninapolilia sana msaada, yeye hukataa* sala yangu.+   Ameviziba vijia vyangu kwa mawe yaliyochongwa;Amezifanya barabara zangu zipinde.+ ד [Daleth] 10  Anangojea kunivizia kama dubu, kama simba aliye mafichoni.+ 11  Amenisukuma kutoka kwenye vijia na kunirarua vipandevipande;*Amenifanya nibaki ukiwa.+ 12  Ameukunja* upinde wake, naye hunifanya niwe shabaha ya mshale wake. ה [He] 13  Amezichoma figo zangu kwa mishale ya* podo lake. 14  Nimekuwa kichekesho kwa mataifa yote, kichwa cha wimbo wao mchana kutwa. 15  Amenijaza mambo machungu na kunikoleza kwa pakanga.+ ו [Waw] 16  Huyavunja meno yangu kwa changarawe;Hunifanya nijikunyate kwa woga katika majivu.+ 17  Unaninyima amani; nimesahau lililo jema. 18  Kwa hiyo ninasema: “Fahari yangu imetoweka, na pia matarajio yangu kwa Yehova.” ז [Zayin] 19  Kumbuka mateso yangu na hali yangu ya kukosa makao,+ pakanga na sumu kali.+ 20  Kwa hakika utakumbuka na kuinama juu yangu.+ 21  Ninakumbuka hili moyoni mwangu; ndiyo sababu nitaonyesha mtazamo wa kungojea.+ ח [Heth] 22  Hatujaangamia kwa sababu ya upendo mshikamanifu wa Yehova,+Kwa maana rehema zake hazikomi kamwe.+ 23  Ni mpya kila asubuhi;+ uaminifu wako ni mwingi sana.+ 24  Nimesema,* “Yehova ni fungu langu+ ndiyo sababu nitaonyesha mtazamo wa kumngojea yeye.”+ ט [Teth] 25  Yehova ni mwema kwa yule anayemtumaini,+ kwa mtu anayeendelea kumtafuta.+ 26  Ni jambo jema kuungojea kimyakimya*+ wokovu wa Yehova.+ 27  Ni jambo jema kwa mwanamume kubeba nira wakati wa ujana.+ י [Yod] 28  Acha akae peke yake na kunyamaza Mungu anapoiweka juu yake.+ 29  Acha atie kinywa chake mavumbini;+ huenda ikawa bado kuna tumaini.+ 30  Acha ampe shavu lake yule anayempiga; acha atukanwe vya kutosha. כ [Kaph] 31  Kwa maana Yehova hatatutupa mbali milele.+ 32  Ingawa amesababisha huzuni, ataonyesha pia rehema kulingana na upendo wake mwingi sana mshikamanifu.+ 33  Kwa maana moyo wake haupendi kuwatesa au kuwahuzunisha wanadamu.+ ל [Lamed] 34  Kuwaponda chini ya nyayo wafungwa wote wa dunia,+ 35  Kumnyima mtu haki yake mbele za Aliye Juu Zaidi,+ 36  Kumlaghai mtu katika kesi yake—Yehova havumilii mambo kama hayo. מ [Mem] 37  Kwa hiyo basi, ni nani anayeweza kusema na jambo likatendeka Yehova asipoamuru? 38  Kutoka katika kinywa cha Aliye Juu Zaidi,Mambo mabaya na mema hayatoki pamoja. 39  Kwa nini mtu aliye hai alalamike kuhusu matokeo ya dhambi yake?+ נ [Nun] 40  Acheni tuzikague na kuzichunguza kwa makini njia zetu,+ na acheni tumrudie Yehova.+ 41  Acheni tuinue mioyo yetu pamoja na mikono yetu kwa Mungu mbinguni:+ 42  “Tumetenda dhambi na kuasi,+ nawe hujatusamehe.+ ס [Samekh] 43  Kwa hasira umeziba njia tusikukaribie;+Umetufuatia na kutuua bila huruma.+ 44  Umeziba kwa wingu njia ya kukukaribia, ili sala yetu isipenye.+ 45  Unatufanya kuwa takataka na uchafu miongoni mwa mataifa.” פ [Pe] 46  Maadui wetu wote wanafungua vinywa vyao dhidi yetu.+ 47  Hofu na mitego vimekuwa fungu letu,+ ukiwa na maangamizi.+ 48  Vijito vya maji vinatiririka kutoka katika macho yangu kwa sababu ya maangamizi ya binti ya watu wangu.+ ע [Ayin] 49  Macho yangu yanamwaga machozi bila kikomo, hayapumziki,+ 50  Mpaka Yehova atakapoangalia na kuona kutoka mbinguni.+ 51  Macho yangu yameniletea huzuni kwa sababu ya mabinti wote wa jiji langu.+ צ [Tsade] 52  Maadui wangu wameniwinda sana kama ndege bila sababu. 53  Wameunyamazisha uhai wangu shimoni; waliendelea kunitupia mawe. 54  Maji yalitiririka juu ya kichwa changu, nami nikasema: “Nimekwisha!” ק [Qoph] 55  Nililiita jina lako kwa sauti, Ee Yehova, kutoka chini shimoni.+ 56  Isikie sauti yangu; usizibe sikio lako ninapolilia msaada, ninapoomba kitulizo. 57  Ulinikaribia siku niliyokuita. Ulisema: “Usiogope.” ר [Resh] 58  Umenitetea,* Ee Yehova, umeukomboa uhai wangu.+ 59  Umeona, Ee Yehova, uovu niliotendewa; tafadhali nitendee haki.+ 60  Umeona kisasi chao chote, njama zao zote walizopanga dhidi yangu. ש [Sin] au [Shin] 61  Umesikia dhihaka zao, Ee Yehova, njama zao zote walizopanga dhidi yangu,+ 62  Midomo ya wapinzani wangu na mambo wanayonong’ona dhidi yangu mchana kutwa. 63  Watazame; wananidhihaki kwa nyimbo zao wakiwa wameketi au wamesimama! ת [Taw] 64  Utawalipa, Ee Yehova, kulingana na matendo yao. 65  Utaifanya mioyo yao kuwa migumu, kama laana kwao. 66  Utawafuatia kwa hasira yako na kuwaangamiza chini ya mbingu zako, Ee Yehova.

Maelezo ya Chini

Au “huizuia; huifungia nje.”
Au labda, “ananiacha kama shamba ambalo halijapandwa mbegu.”
Tnn., “Ameukanyaga.”
Tnn., “wana wa.”
Au “Nafsi yangu inasema.”
Au “kuungojea kwa subira.”
Au “Umezitetea kesi za nafsi yangu.”