Kulingana na Marko 16:1-8

  • Yesu afufuliwa (1-8)

16  Baada ya Sabato+ kupita, Maria Magdalene, Maria+ mama ya Yakobo, na Salome wakanunua manukato ili wakaupake mwili wa Yesu.+  Asubuhi na mapema siku ya kwanza ya juma, jua lilipokuwa limechomoza, wakaenda kwenye kaburi.*+  Walikuwa wakiulizana: “Ni nani atakayetuviringishia lile jiwe kutoka kwenye mwingilio wa kaburi?”  Lakini walipotazama, wakaona lile jiwe lilikuwa limeondolewa, ingawa lilikuwa kubwa sana.+  Walipoingia ndani ya kaburi, wakaona mwanamume kijana akiwa ameketi upande wa kulia akiwa amevaa kanzu nyeupe, nao wakashtuka.  Akawaambia: “Msishtuke.+ Mnamtafuta Yesu Mnazareti, aliyeuawa kwenye mti. Amefufuliwa.+ Hayupo hapa. Tazama, hapa ndipo walipomlaza.+  Lakini nendeni mkawaambie wanafunzi wake na Petro, ‘Yesu anawatangulia kwenda Galilaya.+ Mtamwona huko, kama vile alivyowaambia.’”+  Basi walipotoka kaburini, wakakimbia wakitetemeka huku wakiwa wamelemewa na hisia. Nao hawakumwambia mtu yeyote jambo lolote, kwa sababu waliogopa.*+

Maelezo ya Chini

Au “kwenye kaburi la ukumbusho.”
Kulingana na hati za kale zinazotegemeka, Injili ya Marko inafikia mwisho kwa maneno yaliyo kwenye mstari wa 8. Angalia Nyongeza A3..