Kulingana na Marko 7:1-37

  • Yesu afunua mapokeo ya wanadamu (1-13)

  • Mtu huchafuliwa na kile kinachotoka moyoni (14-23)

  • Imani ya mwanamke wa Sirofoinike (24-30)

  • Mwanamume aliyekuwa kiziwi aponywa (31-37)

7  Sasa Mafarisayo na baadhi ya waandishi waliotoka Yerusalemu wakakusanyika kumzunguka Yesu.+  Wakaona baadhi ya wanafunzi wake wakila chakula kwa mikono isiyo safi, yaani, bila kunawa.*  (Kwa maana kabla ya kula, Mafarisayo na Wayahudi wote hunawa mikono yao mpaka kwenye kiwiko, kwa kuyashika mapokeo ya mababu zao,  na wanapotoka sokoni, hawali chakula kabla ya kujisafisha. Kuna mapokeo mengine mengi ambayo wamepokea na kuyashika, kama vile kubatiza* vikombe, mitungi, na vyombo vya shaba.)+  Basi Mafarisayo na waandishi hao wakamuuliza: “Kwa nini wanafunzi wako hawafuati mapokeo ya mababu zetu, bali wanakula kwa mikono isiyo safi?”+  Akawaambia: “Isaya kwa kufaa alitoa unabii kuwahusu ninyi wanafiki, kama ilivyoandikwa, ‘Watu hawa huniheshimu kwa midomo yao, lakini mioyo yao iko mbali nami.+  Wao huniabudu bure, kwa maana wanafundisha amri za wanadamu kuwa mafundisho.’+  Mnaiacha amri ya Mungu, na kuyashika mapokeo ya wanadamu.”+  Akaendelea kuwaambia: “Mnapuuza amri ya Mungu kwa ujanja ili mfuate mapokeo yenu.+ 10  Kwa mfano, Musa alisema, ‘Mheshimu baba yako na mama yako,’+ na, ‘Yeyote anayemtukana* baba yake au mama yake anapaswa kuuawa.’+ 11  Lakini ninyi mnasema, ‘Mtu akimwambia baba yake au mama yake: “Chochote nilicho nacho ambacho kingekusaidia ni korbani, (yaani, zawadi iliyowekwa wakfu kwa Mungu),”’ 12  hivyo mnamzuia kumsaidia kwa chochote baba yake au mama yake.+ 13  Kwa hiyo, mnalibatilisha neno la Mungu kwa mapokeo yenu ambayo mlipewa.+ Nanyi mnafanya mambo mengine mengi kama hayo.”+ 14  Basi Yesu akauita tena umati, akawaambia: “Nisikilizeni, ninyi nyote, na mwelewe maana yake.+ 15  Mtu hawezi kuchafuliwa na kitu kinachoingia ndani yake; bali huchafuliwa na mambo yanayotoka ndani yake.”+ 16 * —— 17  Alipouacha umati, Yesu aliingia ndani ya nyumba, na wanafunzi wake wakaanza kumuuliza kuhusu mfano huo.+ 18  Basi akawaambia: “Je, ninyi pia hamwelewi kama wao? Je, hamjui kwamba mtu hawezi kuchafuliwa na kitu kinachoingia ndani yake, 19  kwa kuwa hakiingii moyoni mwake bali huingia tumboni, kisha hutoka na kuingia chooni?” Kwa hiyo akatangaza vyakula vyote kuwa safi. 20  Tena akasema: “Kile kinachotoka ndani ya mtu ndicho humchafua.+ 21  Kwa maana kutoka ndani, moyoni mwa watu,+ hutoka mawazo mabaya: uasherati,* wizi, mauaji, 22  uzinzi, pupa, uovu, udanganyifu, mwenendo mpotovu,* jicho lenye wivu, makufuru, majivuno, na ukosefu wa akili. 23  Mambo hayo yote maovu hutoka ndani, nayo humchafua mtu.” 24  Akatoka huko na kwenda kwenye maeneo ya Tiro na Sidoni.+ Akaingia katika nyumba na hakutaka mtu yeyote ajue, lakini hakuweza kuepuka kutambuliwa. 25  Mara moja mwanamke ambaye binti yake mdogo alikuwa na roho mwovu akasikia kumhusu Yesu, akaja na kuanguka miguuni pake.+ 26  Mwanamke huyo alikuwa Mgiriki, wa taifa la* Sirofoinike; naye aliendelea kumsihi sana Yesu amfukuze roho mwovu aliyekuwa ndani ya binti yake. 27  Lakini Yesu akamwambia: “Kwanza acha watoto washibe, kwa maana haifai kuchukua mkate wa watoto na kuwatupia mbwa wadogo.”+ 28  Hata hivyo, yule mwanamke akamjibu: “Ndiyo, bwana, lakini hao mbwa wadogo walio chini ya meza hula makombo ya watoto wadogo.” 29  Ndipo Yesu akamwambia: “Kwa sababu umesema hivyo, nenda; yule roho mwovu amemtoka binti yako.”+ 30  Basi akaenda nyumbani akamkuta yule mtoto akiwa amelala kitandani, na yule roho mwovu alikuwa amemtoka.+ 31  Yesu aliporudi kutoka eneo la Tiro akapitia Sidoni, Dekapoli,* na kufika Bahari ya Galilaya.+ 32  Basi wakamletea mtu aliye kiziwi na mwenye tatizo la kuzungumza,+ nao wakamsihi aweke mkono juu yake. 33  Kisha akampeleka faraghani, mbali na umati. Halafu akamtia vidole masikioni, baada ya kutema mate, akamgusa ulimi.+ 34  Yesu akatazama mbinguni, akavuta pumzi kwa nguvu na kumwambia: “Efatha,” yaani, “Funguka.” 35  Ndipo masikio yake yakafunguliwa,+ na tatizo lake la kuzungumza likaisha, naye akaanza kuzungumza vizuri. 36  Kisha akawaamuru wasimwambie mtu yeyote,+ lakini kadiri alivyowakataza, ndivyo walivyozidi kutangaza jambo hilo.+ 37  Kwa kweli, walishangaa sana+ wakasema: “Amefanya mambo yote vema. Hata anafanya viziwi wasikie na wasio na uwezo wa kusema, wazungumze.”+

Maelezo ya Chini

Yaani, haikuwa imesafishwa kisherehe.
Au “kuzamisha.”
Au “Anayesema vibaya kumhusu.”
Wingi wa neno la Kigiriki, por·neiʹa. Angalia Kamusi.
Au “ufidhuli; matendo ya kuchukiza yanayofanywa bila aibu.” Kigiriki, a·selʹgei·a. Angalia Kamusi.
Au “aliyezaliwa huko.”
Au “Eneo lenye Majiji Kumi.”