Kulingana na Marko 9:1-50

  • Yesu ageuka sura (1-13)

  • Mvulana aliyekuwa na roho mwovu aponywa (14-29)

    • Mambo yote yanawezekana kwa mtu mwenye imani (23)

  • Kifo cha Yesu chatabiriwa tena (30-32)

  • Wanafunzi wabishana kuhusu aliye mkuu zaidi (33-37)

  • Mtu asiyetupinga yuko upande wetu (38-41)

  • Vikwazo (42-48)

  • “Iweni na chumvi ndani yenu” (49, 50)

9  Yesu akaendelea kusema: “Kwa kweli ninawaambia kwamba kuna baadhi ya wale waliosimama hapa ambao hawataonja kifo kamwe kabla ya kuona Ufalme wa Mungu ukiwa tayari umekuja katika nguvu.”+  Siku sita baadaye Yesu akaenda pamoja na Petro, Yakobo, na Yohana kwenye mlima mrefu wakiwa peke yao. Sura yake ikageuka mbele yao;+  mavazi yake ya nje yakaanza kumetameta, yakawa meupe kuliko vile mfuaji nguo yeyote duniani angeweza kuyasafisha.  Pia, wakaona Eliya na Musa, wakizungumza na Yesu.  Kisha Petro akamwambia Yesu: “Rabi, ni vizuri sisi tuwe hapa. Basi, tutasimamisha mahema matatu, moja lako, moja la Musa, na moja la Eliya.”  Kwa kweli, hakujua afanye nini, kwa maana walikuwa wameogopa sana.  Wingu likatokea na kuwafunika, na sauti+ ikasikika kutoka katika lile wingu ikisema: “Huyu ni Mwanangu, mpendwa.+ Msikilizeni.”+  Kisha ghafla wakatazama huku na huku na hawakumwona tena mtu yeyote isipokuwa Yesu.  Walipokuwa wakishuka kutoka mlimani, akawaamuru wasimwambie mtu yeyote kile walichoona,+ hadi Mwana wa binadamu atakapofufuliwa kutoka kwa wafu.+ 10  Wakayaweka maneno hayo moyoni,* lakini wakazungumza kati yao wenyewe kuhusu maana ya huko kufufuliwa kutoka kwa wafu. 11  Wakaanza kumuuliza: “Kwa nini waandishi husema kwamba lazima Eliya+ aje kwanza?”+ 12  Akawaambia: “Eliya anakuja kwanza na kurudisha mambo yote;+ lakini kwa nini imeandikwa kwamba lazima Mwana wa binadamu apatwe na mateso mengi+ na atendewe kwa dharau?+ 13  Lakini ninawaambia kwamba kwa kweli, Eliya+ amekuja nao walimtendea kama walivyotaka, kama ilivyoandikwa kumhusu.”+ 14  Walipowakaribia wale wanafunzi wengine, wakaona umati mkubwa umewazunguka, na kulikuwa na waandishi waliokuwa wakibishana nao.+ 15  Lakini mara tu umati wote ulipomwona, ukashangaa, ukamkimbilia ili kumsalimu. 16  Basi akawauliza: “Mnabishania nini?” 17  Mtu mmoja katika umati akamjibu: “Mwalimu, nilimleta mwanangu kwako kwa sababu ana roho anayemfanya awe bubu.+ 18  Kila mara anapomshambulia humwangusha chini, naye hutoa povu mdomoni na kusaga meno yake na kuishiwa nguvu. Niliwaambia wanafunzi wako wamfukuze, lakini hawakuweza.” 19  Yesu akajibu: “Enyi kizazi kisicho na imani,+ nitaendelea kuwa pamoja nanyi mpaka lini? Nitawavumilia mpaka lini? Mleteni hapa.”+ 20  Basi wakamleta yule mvulana kwa Yesu, lakini yule roho mwovu alipomwona, mara moja akamfanya yule mtoto agaegae. Baada ya kuanguka chini, akaendelea kujiviringisha, akitoa povu mdomoni. 21  Yesu akamuuliza baba yake: “Jambo hili limekuwa likitokea kwa muda gani?” Akasema: “Tangu utotoni, 22  naye humwangusha ndani ya moto na ndani ya maji ili amuue. Lakini ikiwa unaweza kufanya chochote, tuhurumie na utusaidie.” 23  Yesu akamwambia: “Maneno hayo, ‘Ikiwa unaweza’! Mambo yote yanawezekana kwa mtu mwenye imani.”+ 24  Mara moja baba ya yule mtoto akasema kwa sauti kubwa: “Nina imani! Nisaidie mahali ambapo ninahitaji imani!”+ 25  Yesu alipoona umati ukikusanyika haraka, akamkemea yule roho mwovu, akamwambia: “Wewe roho bubu na kiziwi, ninakuagiza umtoke mtoto huyu na usimwingie tena!”+ 26  Baada ya kupaza sauti na kugaagaa sana, roho huyo akamtoka, na yule mtoto akaonekana ni kama amekufa, hivi kwamba watu wengi wakasema: “Amekufa!” 27  Lakini Yesu akamshika mkono na kumwinua, naye akasimama. 28  Baada ya kuingia ndani ya nyumba, wanafunzi wake wakamuuliza faraghani: “Kwa nini tulishindwa kumfukuza?”+ 29  Akawaambia: “Roho wa aina hii hawezi kutoka isipokuwa kwa sala.” 30  Wakatoka huko wakapitia Galilaya, lakini hakutaka mtu yeyote ajue. 31  Kwa sababu alikuwa akiwafundisha wanafunzi wake na kuwaambia: “Mwana wa binadamu atasalitiwa mikononi mwa watu, nao watamuua,+ na ingawa atauawa, atafufuka baada ya siku tatu.”+ 32  Hata hivyo, hawakuelewa maneno aliyosema, nao waliogopa kumuuliza. 33  Nao wakaingia Kapernaumu. Alipokuwa ndani ya nyumba akawauliza: “Mlikuwa mkibishania nini barabarani?”+ 34  Wakakaa kimya, kwa maana barabarani walikuwa wakibishana kuhusu aliye mkuu kati yao. 35  Basi akaketi na kuwaita wale 12 akawaambia: “Yeyote anayetaka kuwa wa kwanza, lazima awe wa mwisho kati ya wote na mhudumu wa wote.”+ 36  Kisha akamchukua mtoto mdogo, akamsimamisha katikati yao; akamkumbatia na kuwaambia: 37  “Yeyote anayempokea mtoto mdogo+ kama huyu kwa msingi wa jina langu ananipokea mimi pia; na yeyote anayenipokea mimi hanipokei mimi tu, bali pia Yule aliyenituma.”+ 38  Yohana akamwambia: “Mwalimu, tulimwona mtu fulani akifukuza roho waovu kwa kutumia jina lako, tukajaribu kumzuia, kwa sababu hakuwa akitufuata.”+ 39  Lakini Yesu akasema: “Msijaribu kumzuia, kwa maana hakuna yeyote atakayefanya matendo yenye nguvu kwa msingi wa jina langu atakayeweza kusema mambo mabaya kunihusu. 40  Kwa maana yeyote ambaye hatupingi yuko upande wetu.+ 41  Na yeyote anayewapa kikombe cha maji ya kunywa kwa sababu ninyi ni wa Kristo,+ kwa kweli ninawaambia hatapoteza kamwe thawabu yake.+ 42  Lakini yeyote anayemkwaza mmoja wa hawa wadogo walio na imani, ingekuwa afadhali ikiwa jiwe la kusagia ambalo huzungushwa na punda lingefungwa shingoni mwake kisha atupwe baharini.+ 43  “Ikiwa mkono wako unakufanya ukwazike, ukate. Ni afadhali uingie katika uzima ukiwa kilema kuliko kuingia ukiwa na mikono miwili katika Gehena,* katika moto usioweza kuzimwa.+ 44 * —— 45  Na ikiwa mguu wako unakufanya ukwazike, ukate. Ni afadhali uingie katika uzima ukiwa kilema kuliko kutupwa katika Gehena* ukiwa na miguu miwili.+ 46 * —— 47  Na ikiwa jicho lako linakufanya ukwazike, litupe mbali.+ Ni afadhali uingie katika Ufalme wa Mungu ukiwa na jicho moja kuliko kutupwa katika Gehena ukiwa na macho mawili,*+ 48  mahali ambapo funza hawafi na moto hauzimwi.+ 49  “Kwa maana kila mtu lazima atiwe chumvi kwa moto.+ 50  Chumvi ni nzuri, lakini ikipoteza ladha yake, mtaikoleza na nini?+ Iweni na chumvi ndani yenu,+ na mdumishe amani kati yenu.”+

Maelezo ya Chini

Au labda, “hawakumwambia mtu yeyote.”
Angalia Kamusi.
Angalia Kamusi.
Angalia Kamusi.