Matendo ya Mitume 16:1-40

  • Paulo amchagua Timotheo (1-5)

  • Maono kuhusu mwanamume Mmakedonia (6-10)

  • Lidia awa mwamini huko Filipi (11-15)

  • Paulo na Sila wafungwa gerezani (16-24)

  • Mlinzi wa jela na nyumba yake wabatizwa (25-34)

  • Paulo ataka ombi rasmi la msamaha (35-40)

16  Kwa hiyo akafika Derbe na pia Listra.+ Huko kulikuwa na mwanafunzi aliyeitwa Timotheo,+ mama yake alikuwa Myahudi aliyekuwa mwamini, lakini baba yake alikuwa Mgiriki,  na alishuhudiwa vema na akina ndugu huko Listra na Ikoniamu.  Paulo alitamani Timotheo aende pamoja naye, basi akamchukua na kumtahiri kwa sababu ya Wayahudi waliokuwa katika sehemu hizo,+ kwa maana wote walijua kwamba baba yake ni Mgiriki.  Walipokuwa wakipita katika majiji, walikuwa wakiwapa maagizo yaliyokuwa yameamuliwa na mitume na wazee waliokuwa Yerusalemu ili wayashike.+  Ndipo kwa kweli makutaniko yakaendelea kuimarishwa katika imani na kuongezeka idadi siku baada ya siku.  Zaidi ya hayo, wakapitia Frigia na nchi ya Galatia,+ kwa sababu roho takatifu iliwakataza kuhubiri lile neno katika mkoa wa Asia.  Vilevile, walipofika Misia wakajaribu kuingia Bithinia,+ lakini roho ya Yesu haikuwaruhusu.  Basi wakapita* Misia na kushuka mpaka Troa.  Naye Paulo akaona maono usiku—mwanamume Mmakedonia alikuwa amesimama hapo akimsihi: “Vuka uingie Makedonia utusaidie.” 10  Mara tu alipoona maono hayo, tukajaribu kuingia Makedonia, tukikata kauli kwamba Mungu alikuwa ametuita tuwatangazie habari njema. 11  Basi tukatoka Troa na kusafiri moja kwa moja baharini hadi Samothrake, lakini kesho yake tukafika Neapoli; 12  na kutoka huko tukaenda Filipi,+ koloni ambalo ni jiji kuu la wilaya ya Makedonia. Tukakaa katika jiji hilo siku kadhaa. 13  Siku ya Sabato tukatoka nje ya lango kando ya mto, ambako tulifikiri kuna mahali pa sala, tukaketi na kuanza kuzungumza na wanawake waliokuwa wamekusanyika. 14  Na mwanamke aliyeitwa Lidia, muuzaji wa nguo za rangi ya zambarau, wa jiji la Thiatira+ aliyekuwa mwabudu wa Mungu, alikuwa akisikiliza, na Yehova* akaufungua moyo wake wazi ili asikilize kwa makini mambo ambayo Paulo alikuwa akisema. 15  Basi yeye na watu wa nyumbani mwake walipobatizwa,+ akatusihi: “Ikiwa mmeniona kuwa mwaminifu kwa Yehova,* njooni mkae nyumbani kwangu.” Naye akatuhimiza sana twende. 16  Ikatukia kwamba tulipokuwa tukienda mahali pale pa kusali, tulikutana na kijakazi fulani mwenye roho, roho mwovu wa uaguzi.+ Aliwapatia mabwana zake faida nyingi kwa kubashiri.* 17  Msichana huyo alikuwa akimfuata Paulo na sisi akisema kwa sauti kubwa: “Watu hawa ni watumwa wa Mungu Aliye Juu Zaidi+ nao wanawatangazia ninyi njia ya wokovu.” 18  Akaendelea kufanya hivyo kwa siku nyingi. Mwishowe Paulo akachoshwa, akageuka na kumwambia huyo roho: “Ninakuamuru katika jina la Yesu Kristo umtoke.” Naye akatoka saa hiyohiyo.+ 19  Basi, mabwana zake walipoona kwamba wamepoteza tumaini lao la kupata faida,+ wakawakamata Paulo na Sila wakawakokota hadi sokoni kwa watawala.+ 20  Wakawapeleka kwa mahakimu wa raia, na kusema: “Watu hawa wanasumbua sana jiji letu.+ Wao ni Wayahudi, 21  nao wanatangaza desturi ambazo si halali kwetu kuzikubali au kuzifuata, kwa kuwa sisi ni Waroma.” 22  Umati ukasimama pamoja dhidi yao, nao wale mahakimu wa raia, baada ya kuyararua mavazi yao, wakaamuru wapigwe kwa fimbo.+ 23  Baada ya kuwapiga sana, wakawatupa gerezani na kumwagiza mlinzi wa jela awalinde.+ 24  Kwa sababu alipewa agizo hilo, akawatupa katika gereza la ndani zaidi na kuifunga miguu yao katika mikatale. 25  Lakini karibu katikati ya usiku, Paulo na Sila walikuwa wakisali na kumsifu Mungu kwa wimbo,+ nao wafungwa walikuwa wakiwasikiliza. 26  Ghafla tetemeko kubwa la ardhi likatokea na misingi ya jela ikatikiswa. Isitoshe, milango yote ikafunguliwa mara moja, na vifungo vyao wote vikafunguka.+ 27  Mlinzi wa jela alipoamka na kuona milango ya gereza imefunguka, akauchomoa upanga wake naye karibu ajiue, akidhani wafungwa walikuwa wametoroka.+ 28  Lakini Paulo akamwambia kwa sauti kubwa: “Usijiumize, kwa maana sisi sote tupo hapa!” 29  Kwa hiyo akaomba taa akakimbia ndani, akitetemeka, akaanguka chini mbele ya Paulo na Sila. 30  Akawaleta nje na kusema: “Mabwana zangu, nifanye nini ili niokolewe?” 31  Wakajibu: “Mwamini Bwana Yesu, nawe utaokolewa, wewe na watu wa nyumba yako.”+ 32  Nao wakamhubiria neno la Yehova* yeye pamoja na wote waliokuwa katika nyumba yake. 33  Naye akawachukua saa hiyo ya usiku, akaosha vidonda vyao. Kisha yeye na watu wote wa nyumba yake wakabatizwa bila kukawia.+ 34  Akawaleta nyumbani kwake akaandaa meza mbele yao, naye akashangilia sana pamoja na watu wote wa nyumba yake kwa kuwa sasa alikuwa amemwamini Mungu. 35  Ilipofika mchana, mahakimu wa raia wakawatuma maofisa wa polisi wakaseme: “Wafungueni wale watu.” 36  Mlinzi wa jela akamweleza Paulo maneno yao: “Mahakimu wa raia wamewatuma watu ili ninyi wawili mfunguliwe. Basi tokeni sasa mwende zenu kwa amani.” 37  Lakini Paulo akawaambia: “Walitupiga viboko hadharani bila kutuhukumu,* ingawa sisi ni Waroma,+ na wakatutupa gerezani. Je, sasa wanatufukuza kwa siri? Hapana, haiwezekani! Acha waje watutoe nje wao wenyewe.” 38  Wale maofisa wa polisi wakawaeleza mahakimu wa raia maneno hayo. Nao wakaogopa waliposikia kwamba watu hao walikuwa Waroma.+ 39  Basi wakaja na kuwasihi na baada ya kuwatoa nje, wakawaomba waondoke katika jiji hilo. 40  Lakini wakatoka gerezani na kwenda nyumbani kwa Lidia; na walipowaona akina ndugu, wakawatia moyo+ kisha wakaondoka.

Maelezo ya Chini

Au “wakapitia.”
Au “kupiga ramli.”
Au “bila uamuzi wa mahakama.”