Matendo ya Mitume 18:1-28

  • Huduma ya Paulo huko Korintho (1-17)

  • Kurudi Antiokia ya Siria (18-22)

  • Paulo aenda Galatia na Frigia (23)

  • Apolo mwenye ufasaha asaidiwa (24-28)

18  Baada ya hayo, akatoka Athene na kwenda Korintho.  Naye akamkuta Myahudi aliyeitwa Akila,+ mzaliwa wa Ponto aliyekuwa amekuja hivi karibuni kutoka Italia na Prisila mke wake, kwa sababu Klaudio alikuwa ameagiza Wayahudi wote waondoke Roma. Basi akaenda kwao,  na kwa sababu walifanya kazi ileile, akakaa nyumbani kwao na kufanya kazi pamoja nao,+ kwa maana kazi yao ilikuwa ya kutengeneza mahema.  Alikuwa akitoa hotuba* katika sinagogi+ kila sabato+ na kuwashawishi Wayahudi na Wagiriki.  Basi, Sila+ na Timotheo+ waliposhuka kutoka Makedonia, Paulo akaanza kushughulika sana na lile neno, akiwatolea Wayahudi ushahidi ili kuthibitisha kwamba Yesu ndiye Kristo.+  Lakini walipoendelea kumpinga na kumtukana, akayakung’uta mavazi yake+ na kuwaambia: “Damu yenu na iwe juu ya vichwa vyenu wenyewe.+ Mimi ni safi.+ Kuanzia sasa nitaenda kwa watu wa mataifa.”+  Basi akatoka humo* na kuingia katika nyumba ya mwanamume aliyeitwa Titio Yusto, mwabudu wa Mungu, ambaye nyumba yake ilikuwa imeshikana na sinagogi.  Lakini Krispo,+ ofisa msimamizi wa sinagogi akamwamini Bwana, yeye pamoja na watu wote wa nyumba yake. Na Wakorintho wengi waliosikia wakaanza kuamini na kubatizwa.  Isitoshe, Bwana akamwambia Paulo katika maono usiku: “Usiogope, bali endelea kusema na usinyamaze, 10  kwa sababu niko pamoja nawe+ na hakuna mtu atakayekushambulia ili kukudhuru; kwa maana nina watu wengi katika jiji hili.” 11  Basi akakaa huko kwa mwaka mmoja na miezi sita, akifundisha neno la Mungu kati yao. 12  Galio alipokuwa liwali* wa Akaya, Wayahudi wakaungana, wakamshambulia Paulo na kumpeleka kwenye kiti cha hukumu, 13  wakisema: “Mtu huyu anawashawishi watu wamwabudu Mungu kwa njia iliyo kinyume cha sheria.” 14  Lakini Paulo alipokuwa karibu kuzungumza, Galio akawaambia Wayahudi: “Enyi Wayahudi, kama kweli lingekuwa kosa fulani au uhalifu mkubwa, ningekuwa na sababu ya kuwasikiliza kwa subira. 15  Lakini kama mnabishania maneno na majina na sheria yenu,+ amueni wenyewe. Mimi sitaki kuwa mwamuzi wa mambo hayo.” 16  Ndipo akawafukuza kutoka mbele ya kiti cha hukumu. 17  Basi wote wakamkamata Sosthene,+ ofisa msimamizi wa sinagogi na kuanza kumpiga mbele ya kiti cha hukumu. Lakini Galio hakujihusisha kamwe na mambo hayo. 18  Hata hivyo, baada ya kukaa siku kadhaa, Paulo aliwaaga akina ndugu naye akasafiri baharini kwenda Siria, pamoja na Prisila na Akila. Alikuwa amekata nywele zake huko Kenkrea,+ kwa sababu alikuwa ameweka nadhiri. 19  Basi wakafika Efeso, akawaacha huko; lakini yeye akaingia ndani ya sinagogi na kujadiliana na Wayahudi.+ 20  Ingawa waliendelea kumsihi akae kwa muda mrefu zaidi, hakukubali 21  bali aliwaaga na kuwaambia: “Nitarudi kwenu tena, Yehova* akipenda.” Naye akasafiri baharini kutoka Efeso 22  na kushuka mpaka Kaisaria. Akapanda kwenda na kulisalimia kutaniko,* kisha akashuka kwenda Antiokia.+ 23  Baada ya kukaa huko kwa muda fulani, akaondoka na kwenda sehemu mbalimbali katika nchi ya Galatia na Frigia,+ akiwaimarisha wanafunzi wote.+ 24  Sasa Myahudi aliyeitwa Apolo,+ mzaliwa wa Aleksandria akafika Efeso; alikuwa mwanamume mwenye ufasaha na ujuzi mwingi wa Maandiko. 25  Mwanamume huyu alikuwa amefundishwa* njia ya Yehova,* na akiwa amewaka roho, alikuwa akizungumza na kufundisha kwa usahihi kumhusu Yesu, lakini alifahamu ubatizo wa Yohana tu. 26  Akaanza kuzungumza kwa ujasiri katika sinagogi, nao Prisila na Akila+ walipomsikia, wakamchukua na kumfafanulia kwa usahihi zaidi njia ya Mungu. 27  Pia, kwa sababu alitaka kuvuka kwenda Akaya, akina ndugu wakawaandikia wanafunzi wakiwahimiza wamkaribishe kwa fadhili. Basi alipofika huko, akawasaidia sana wale ambao kupitia fadhili zisizostahiliwa za Mungu walikuwa wameamini; 28  kwa maana alithibitisha kikamili hadharani na kwa juhudi nyingi kwamba Wayahudi walikuwa wamekosea, na kuwaonyesha kwa Maandiko kuwa Yesu ndiye Kristo.+

Maelezo ya Chini

Au “Alikuwa akijadiliana nao.”
Yaani, sinagogi.
Gavana Mroma aliyetawala mkoa. Angalia Kamusi.
Inaonekana alienda Yerusalemu.
Au “amefundishwa kwa mdomo.”