Matendo ya Mitume 3:1-26

  • Petro amponya kilema aliyekuwa akiombaomba (1-10)

  • Hotuba ya Petro kwenye Safu ya Nguzo za Sulemani (11-26)

    • “Kurudishwa kwa mambo yote” (21)

    • Nabii kama Musa (22)

3  Basi Petro na Yohana walikuwa wakipanda kwenda hekaluni wakati wa saa ya sala, yaani, saa tisa,*  na mwanamume fulani aliyekuwa kilema tangu kuzaliwa alikuwa amebebwa. Kila siku walimweka karibu na lango la hekalu lililoitwa Lango Zuri, ili aombe zawadi za rehema kutoka kwa wale waliokuwa wakiingia hekaluni.  Alipowaona Petro na Yohana wakiwa karibu kuingia hekaluni, akaanza kuomba zawadi za rehema.  Lakini Petro, pamoja na Yohana, wakamtazama moja kwa moja na kumwambia: “Tuangalie.”  Kwa hiyo akawaangalia, akitarajia kupata kitu kutoka kwao.  Hata hivyo, Petro akasema: “Sina fedha wala dhahabu, lakini kile nilicho nacho ndicho ninachokupa. Katika jina la Yesu Kristo Mnazareti, tembea!”+  Ndipo akamshika mkono wa kulia na kumwinua.+ Papo hapo miguu yake na vifundo vya miguu yake vikafanywa imara;+  akasimama mara moja,+ akaanza kutembea na kuingia nao hekaluni, akitembea na kurukaruka akimsifu Mungu.  Watu wote wakamwona akitembea huku akimsifu Mungu. 10  Wakaanza kutambua kwamba huyu ndiye mtu aliyekuwa akiketi kwenye Lango Zuri la hekalu+ akisubiri zawadi za rehema, nao wakashangaa sana na kushangilia kuhusu jambo lililotokea. 11  Mtu huyo akiwa bado amewashika Petro na Yohana, watu wote wakawakimbilia pamoja kwenye sehemu iliyoitwa Safu ya Nguzo za Sulemani,+ wakiwa wameshangaa sana. 12  Petro alipoona jambo hilo, akawaambia watu hao: “Watu wa Israeli, kwa nini mnastaajabishwa na jambo hili, na kwa nini mnatutazama kana kwamba tumemfanya atembee kwa nguvu zetu au kwa sababu ya ujitoaji-kimungu?* 13  Mungu wa Abrahamu na wa Isaka na wa Yakobo,+ Mungu wa mababu zetu, amemtukuza Mtumishi wake,+ Yesu,+ ambaye ninyi mlimkabidhi+ na kumkana mbele ya Pilato, ingawa alikuwa ameamua kumfungua. 14  Ndiyo, mlimkana huyo aliye mtakatifu na mwadilifu, nanyi mkaomba mpewe mwanamume aliyekuwa muuaji,+ 15  lakini mkamuua Wakili Mkuu wa uzima.+ Hata hivyo, Mungu alimfufua kutoka kwa wafu, nasi ni mashahidi wa jambo hilo.+ 16  Kupitia jina lake, na kwa imani yetu katika jina lake, mtu huyu mnayemwona na kumfahamu amefanywa awe mwenye nguvu. Imani kupitia kwake imemfanya mtu huyu awe mwenye afya kamili, mbele yenu nyote. 17  Na sasa, akina ndugu, ninajua kwamba mlitenda kwa kutojua,+ kama vile watawala wenu pia walivyotenda.+ 18  Lakini kwa njia hiyo Mungu ametimiza mambo aliyotangaza mapema kupitia kinywa cha manabii wote, kwamba Kristo wake angeteseka.+ 19  “Kwa hiyo, tubuni+ na mgeuke+ ili dhambi zenu zifutwe,+ ili majira yenye kuburudisha yaje kutoka kwa Yehova mwenyewe,* 20  naye amtume Kristo aliyewekwa rasmi kwa ajili yenu, yaani, Yesu. 21  Naye lazima abaki mbinguni mpaka nyakati za kurudishwa kwa mambo yote ambayo Mungu alisema kupitia kinywa cha manabii wake watakatifu walioishi zamani. 22  Kwa kweli, Musa alisema: ‘Yehova* Mungu wenu atawainulia nabii kama mimi kutoka kati ya ndugu zenu.+ Ni lazima msikilize kile atakachowaambia.+ 23  Kwa kweli, yeyote* ambaye hatamsikiliza Nabii huyo ataangamizwa kutoka kati ya watu.’+ 24  Manabii wote kuanzia Samweli na wale waliofuata, wengi ambao wamesema, wametangaza waziwazi pia kuhusu siku hizi.+ 25  Ninyi ndio wana wa manabii na wa agano ambalo Mungu alifanya na mababu zenu,+ alipomwambia Abrahamu: ‘Kupitia uzao wako,* familia zote za dunia zitabarikiwa.’+ 26  Baada ya Mungu kumwinua Mtumishi wake, alimtuma kwenu kwanza+ ili awabariki ninyi kwa kumgeuza kila mmoja wenu aache matendo yake maovu.”

Maelezo ya Chini

Yaani, karibu saa 9 alasiri.
Angalia Kamusi.
Tnn., “kutoka kwa uso wa Yehova.” Angalia Nyongeza A5.
Au “nafsi yoyote.”
Tnn., “mbegu yako.”