Matendo ya Mitume 6:1-15

  • Wanaume saba wachaguliwa kuhudumu (1-7)

  • Stefano ashtakiwa kwamba amekufuru (8-15)

6  Basi katika siku hizo, wanafunzi walipokuwa wakiongezeka, Wayahudi waliozungumza Kigiriki walianza kulalamika kuhusu Wayahudi waliozungumza Kiebrania, kwa sababu wajane wao walikuwa wakipuuzwa katika ugawaji wa kila siku.+  Basi wale 12 wakauita umati wa wanafunzi na kuwaambia: “Si vema* sisi tuache neno la Mungu ili kugawa chakula mezani.+  Basi akina ndugu, jichagulieni kati yenu wanaume saba wenye sifa nzuri,+ waliojaa roho na hekima,+ ili tuwaweke rasmi wafanye kazi hii muhimu;+  lakini sisi tutajitoa kwa sala na huduma ya neno.”  Wanafunzi wote wakakubaliana na jambo walilosema, nao wakamchagua Stefano, mwanamume aliyejaa imani na roho takatifu, vilevile Filipo,+ Prokoro, Nikanori, Timoni, Parmena, na Nikolao, mgeuzwa-imani wa Antiokia.  Wakawaleta kwa mitume, na baada ya kusali, wakaweka mikono juu yao.+  Kwa hiyo, neno la Mungu likazidi kuenea,+ na idadi ya wanafunzi ikazidi kuongezeka sana+ huko Yerusalemu; na umati mkubwa wa makuhani wakawa waamini.+  Sasa Stefano, akiwa amejaa kibali cha Mungu na nguvu, alikuwa akifanya mambo makubwa ya ajabu* na ishara kati ya watu.  Lakini watu fulani wa Sinagogi la Watu Waliowekwa Huru wakaja mbele, pamoja na Wakirene na Waaleksandria, na wengine kutoka Kilikia na Asia, ili kubishana na Stefano. 10  Lakini hawakuweza kumshinda kwa sababu ya hekima yake na roho iliyomwongoza kusema.+ 11  Ndipo wakawashawishi watu kwa siri waseme: “Tumemsikia akisema maneno ya kumkufuru Musa na Mungu.” 12  Nao wakawachochea watu, wazee, na waandishi, wakamjia ghafla, wakamkamata kwa nguvu na kumpeleka kwenye Sanhedrini. 13  Wakawaleta mbele mashahidi wa uwongo, waliosema: “Mtu huyu haachi kusema mambo yasiyofaa kuhusu mahali hapa patakatifu na kuhusu Sheria. 14  Kwa mfano, tumemsikia akisema kwamba huyu Yesu Mnazareti atapaangusha mahali hapa na kuzibadili desturi ambazo Musa alitukabidhi.” 15  Wote waliokuwa wameketi katika Sanhedrini wakamkazia macho, nao wakaona uso wake ukiwa kama uso wa malaika.

Maelezo ya Chini

Tnn., “Haipendezi.”
Au “miujiza.”