Kulingana na Mathayo 1:1-25

  • Ukoo wa Yesu Kristo (1-17)

  • Yesu azaliwa (18-25)

1  Kitabu cha historia ya* Yesu Kristo,* mwana wa Daudi,+ mwana wa Abrahamu:+   Abrahamu akawa baba ya Isaka;+ Isaka akawa baba ya Yakobo;+ Yakobo akawa baba ya Yuda+ na ndugu zake;   Yuda akawa baba ya Perezi na Zera+ kupitia Tamari; Perezi akawa baba ya Hezroni;+ Hezroni akawa baba ya Ramu;+   Ramu akawa baba ya Aminadabu; Aminadabu akawa baba ya Nashoni;+ Nashoni akawa baba ya Salmoni;   Salmoni akawa baba ya Boazi kupitia Rahabu;+ Boazi akawa baba ya Obedi kupitia Ruthu;+ Obedi akawa baba ya Yese;+   Yese akawa baba ya Mfalme Daudi.+ Daudi akawa baba ya Sulemani+ kupitia mke wa Uria;   Sulemani akawa baba ya Rehoboamu;+ Rehoboamu akawa baba ya Abiya; Abiya akawa baba ya Asa;+   Asa akawa baba ya Yehoshafati;+ Yehoshafati akawa baba ya Yehoramu;+ Yehoramu akawa baba ya Uzia;   Uzia akawa baba ya Yothamu;+ Yothamu akawa baba ya Ahazi;+ Ahazi akawa baba ya Hezekia;+ 10  Hezekia akawa baba ya Manase;+ Manase akawa baba ya Amoni;+ Amoni akawa baba ya Yosia;+ 11  Yosia+ akawa baba ya Yekonia+ na ndugu zake, wakati wa kupelekwa uhamishoni Babiloni.+ 12  Baada ya kupelekwa uhamishoni Babiloni, Yekonia akawa baba ya Shealtieli; Shealtieli akawa baba ya Zerubabeli;+ 13  Zerubabeli akawa baba ya Abiudi; Abiudi akawa baba ya Eliakimu; Eliakimu akawa baba ya Azori; 14  Azori akawa baba ya Sadoki; Sadoki akawa baba ya Akimu; Akimu akawa baba ya Eliudi; 15  Eliudi akawa baba ya Eleazari; Eleazari akawa baba ya Mathani; Mathani akawa baba ya Yakobo; 16  Yakobo akawa baba ya Yosefu mume wa Maria, aliyemzaa Yesu,+ aitwaye Kristo.+ 17  Kuanzia Abrahamu mpaka Daudi kulikuwa na vizazi 14; kuanzia Daudi mpaka wakati wa kupelekwa uhamishoni Babiloni, vizazi 14; kuanzia wakati wa kupelekwa uhamishoni Babiloni mpaka Kristo, vizazi 14. 18  Basi kuzaliwa kwa Yesu Kristo kulikuwa hivi: Maria mama ya Yesu alichumbiwa na Yosefu, lakini kabla hawajafunga ndoa akapata mimba kupitia roho takatifu.*+ 19  Hata hivyo, kwa sababu Yosefu mume wake alikuwa mwadilifu na hakutaka kumwaibisha hadharani, alikusudia kumtaliki kisiri.+ 20  Lakini baada ya kufikiria mambo hayo, tazama! malaika wa Yehova* alimtokea katika ndoto na kumwambia: “Yosefu, mwana wa Daudi, usiogope kumpeleka Maria mke wako nyumbani, kwa sababu amepata mimba kupitia roho takatifu.+ 21  Atamzaa mwana, nawe utamwita jina Yesu,*+ kwa maana atawaokoa watu wake kutoka katika dhambi zao.”+ 22  Kwa kweli, yote hayo yalitukia ili kutimiza maneno haya yaliyosemwa na Yehova* kupitia nabii wake: 23  “Tazama! Bikira atapata mimba naye atazaa mwana, nao watamwita jina Imanueli,”+ ambalo linapotafsiriwa linamaanisha, “Mungu Yuko Pamoja Nasi.”+ 24  Ndipo Yosefu akaamka kutoka usingizini na kufanya kama alivyoambiwa na malaika wa Yehova,* akampeleka mke wake nyumbani. 25  Lakini hakufanya ngono naye mpaka alipozaa mwana,+ kisha Yosefu akamwita jina Yesu.+

Maelezo ya Chini

Au “Masihi; Mtiwa-mafuta.”
Au “ukoo wa.”
Au “nguvu ya utendaji.”
Hii ndiyo mara ya kwanza, kati ya mara 237 katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo ambapo jina la Mungu, Yehova, linapatikana katika toleo hili. Angalia Nyongeza A5.
Linafanana na jina la Kiebrania Yeshua, au Yoshua, linalomaanisha “Yehova Ni Wokovu.”