Kulingana na Mathayo 11:1-30

  • Yohana Mbatizaji asifiwa (1-15)

  • Kizazi kisicho na imani chashutumiwa (16-24)

  • Yesu amsifu Baba yake kwa kuwafunulia mambo wanyenyekevu (25-27)

  • Nira ya Yesu inaburudisha (28-30)

11  Yesu alipomaliza kuwapa wanafunzi wake 12 maagizo, akaondoka huko na kwenda kufundisha na kuhubiri katika majiji yao.+  Lakini Yohana akiwa jela+ alisikia mambo ambayo Kristo alikuwa akifanya, akawatuma wanafunzi wake+  wamuulize: “Je, wewe ndiye Yule Anayekuja, au tumtarajie mwingine?”+  Yesu akawajibu: “Nendeni mkamwambie Yohana mambo mnayosikia na kuona:+  Vipofu wanaona,+ viwete wanatembea, wenye ukoma+ wanatakaswa, viziwi wanasikia, wafu wanafufuliwa, na maskini wanahubiriwa habari njema.+  Mwenye furaha ni mtu ambaye hapati ndani yangu sababu ya kukwaza.”+  Hao walipoondoka, Yesu akaanza kuuambia umati kumhusu Yohana: “Mlienda nyikani kuona nini?+ Tete likitikiswa na upepo?+  Basi, mlienda kuona nini? Mtu aliyevaa mavazi laini?* Kwa maana wale wanaovaa mavazi laini wamo katika nyumba za wafalme.  Basi kwa kweli, kwa nini mlienda? Kumwona nabii? Ndiyo, ninawaambia, mtu aliye zaidi ya nabii.+ 10  Huyu ndiye ambaye imeandikwa hivi kumhusu: ‘Tazama! Ninamtuma mjumbe wangu mbele yako,* ili akutayarishie njia mbele yako!’+ 11  Kwa kweli ninawaambia, kati ya wale waliozaliwa na wanawake hajatokea mtu mkuu kuliko Yohana Mbatizaji, lakini mtu mdogo zaidi katika Ufalme wa mbinguni ni mkuu kuliko yeye.+ 12  Tangu siku za Yohana Mbatizaji mpaka sasa, Ufalme wa mbinguni ndio mradi ambao watu wanajitahidi kuufikia, na wale wanaojitahidi sana wanaupata.+ 13  Kwa maana, maneno yote ya Manabii na Sheria yalitabiri hadi wakati wa Yohana;+ 14  na mkitaka kukubali, yeye ndiye ‘Eliya anayepaswa kuja.’+ 15  Aliye na masikio na asikilize. 16  “Nitakifananisha kizazi hiki na nani?+ Ni kama watoto walioketi sokoni wakiwapazia wenzao sauti, 17  wakisema: ‘Tuliwapigia filimbi, lakini hamkucheza dansi; tuliomboleza, lakini hamkujipiga-piga kwa huzuni.’ 18  Vivyo hivyo, Yohana hakuja akila wala kunywa, lakini watu wanasema, ‘Ana roho mwovu.’ 19  Mwana wa binadamu alikuja akila na kunywa,+ lakini watu wanasema, ‘Tazama! Yeye ni mlafi na mwenye mazoea ya kunywa divai, rafiki ya wakusanya kodi na watenda dhambi.’+ Hata hivyo, hekima huthibitishwa kuwa yenye uadilifu* kupitia kazi zake.”*+ 20  Kisha Yesu akaanza kuyakemea majiji ambako alifanya matendo mengi yenye nguvu, kwa sababu hawakutubu: 21  “Ole wako, Korazini! Ole wako, Bethsaida! kwa sababu kama matendo yenye nguvu yaliyofanywa kwenu yangefanywa huko Tiro na Sidoni, watu wa majiji hayo wangekuwa wametubu zamani katika nguo za magunia na katika majivu.+ 22  Lakini ninawaambia, katika Siku ya Hukumu, itakuwa afadhali zaidi kwa Tiro na Sidoni kuliko kwenu.+ 23  Nawe Kapernaumu,+ je, utainuliwa mpaka mbinguni? Utashuka mpaka Kaburini;*+ kwa sababu kama matendo yenye nguvu yaliyofanywa ndani yako yangefanywa huko Sodoma, jiji hilo lingekuwepo mpaka leo hii. 24  Lakini ninawaambia, katika Siku ya Hukumu itakuwa afadhali zaidi kwa nchi ya Sodoma kuliko kwenu.”+ 25  Ndipo Yesu akasema: “Ninakusifu hadharani, Baba, Bwana wa mbingu na dunia, kwa sababu umewaficha mambo haya wenye hekima na wenye elimu nawe umeyafunua kwa watoto wadogo.+ 26  Ndiyo, Ee Baba, kwa sababu umekubali iwe hivyo. 27  Baba yangu amenikabidhi vitu vyote,+ na hakuna mtu anayemjua Mwana kikamili isipokuwa Baba;+ wala hakuna anayemjua Baba kikamili isipokuwa Mwana, na yeyote ambaye Mwana anapenda kumfunulia.+ 28  Njooni kwangu, nyote mnaotaabika na kulemewa na mizigo, nami nitawaburudisha. 29  Chukueni nira yangu na mjifunze kutoka kwangu, kwa maana mimi ni mpole na mnyenyekevu moyoni,+ nanyi mtapata burudisho kwa ajili yenu.* 30  Kwa maana nira yangu ni laini,* na mzigo wangu ni mwepesi.”

Maelezo ya Chini

Au “mavazi bora.”
Tnn., “mbele ya uso wako.”
Au “hutetewa.”
Au “kwa matokeo yake.”
Au “Hadesi.” Angalia Kamusi.
Au “kwa ajili ya nafsi zenu.”
Au “rahisi.”