Kulingana na Mathayo 3:1-17

  • Yohana Mbatizaji ahubiri (1-12)

  • Yesu abatizwa (13-17)

3  Siku hizo Yohana+ Mbatizaji alikuja kuhubiri+ katika nyika ya Yudea,  akisema: “Tubuni, kwa maana Ufalme wa mbinguni umekaribia.”+  Kwa kweli, huyu ndiye anayezungumziwa kupitia nabii Isaya+ kwa maneno haya: “Kuna mtu anayepaza sauti nyikani: ‘Tayarisheni njia ya Yehova!* Nyoosheni barabara zake.’”+  Yohana alivaa mavazi yaliyofumwa kwa manyoya ya ngamia na alijifunga mshipi wa ngozi kiunoni.+ Chakula chake kilikuwa nzige na asali ya mwituni.+  Basi watu kutoka Yerusalemu na Yudea yote na maeneo yote yaliyokuwa karibu na Yordani walikuwa wakimwendea,+  naye akawabatiza* katika Mto Yordani,+ nao wakaungama dhambi zao waziwazi.  Alipoona Mafarisayo na Masadukayo+ wengi wakija kwenye ubatizo, akawaambia: “Enyi uzao wa nyoka,*+ ni nani amewaonya ili mkimbie ghadhabu inayokuja?+  Basi zaeni matunda yanayoonyesha toba.  Msithubutu kujiambia, ‘Abrahamu ndiye baba yetu.’+ Kwa maana ninawaambia, Mungu anaweza kumwinulia Abrahamu watoto kutoka kwenye mawe haya. 10  Tayari shoka limewekwa kwenye mzizi wa miti. Basi, kila mti usiozaa matunda mazuri utakatwa na kutupwa motoni.+ 11  Mimi ninawabatiza kwa maji kwa sababu mmetubu,+ lakini yule anayekuja baada yangu ana nguvu kuliko mimi, nami sistahili kuvivua viatu vyake.+ Yeye atawabatiza ninyi kwa roho takatifu+ na kwa moto.+ 12  Sepetu yake ya kupepetea imo mkononi mwake, naye atausafisha kabisa uwanja wake wa kupuria, na kukusanya ngano yake katika ghala, lakini atayateketeza makapi kwa moto+ usioweza kuzimwa.” 13  Ndipo Yesu akatoka Galilaya na kwenda Yordani ili abatizwe na Yohana.+ 14  Lakini Yohana akajaribu kumzuia, akisema: “Mimi ndiye ninayehitaji kubatizwa na wewe, nawe unakuja kwangu?” 15  Yesu akamjibu: “Acha iwe hivyo wakati huu, kwa maana kwa njia hiyo inafaa tufanye yote yaliyo ya uadilifu.” Ndipo Yohana akaacha kumzuia. 16  Baada ya kubatizwa, mara moja Yesu akainuka kutoka katika maji; na tazama! mbingu zikafunguliwa,+ naye akaona roho ya Mungu ikishuka kama njiwa, ikija juu yake.+ 17  Tazama! Pia, sauti ikasikika kutoka mbinguni+ ikisema: “Huyu ni Mwanangu,+ mpendwa, ambaye nimemkubali.”+

Maelezo ya Chini

Au “akawatumbukiza; akawazamisha.”
Au “nyoka-vipiri.”