Methali 11:1-31

  • Wenye kiasi wana hekima (2)

  • Mwasi imani huwaangamiza wengine (9)

  • “Washauri wengi huleta mafanikio” (14)

  • Mtu mkarimu atapata ufanisi (25)

  • Anayeutumaini utajiri wake ataanguka (28)

11  Mizani ya uwongo* humchukiza Yehova,Lakini kipimo sahihi* humfurahisha.+   Kimbelembele kinapokuja, aibu itafuata,+Lakini wenye kiasi wana hekima.+   Utimilifu wa wanyoofu ndio unaowaongoza,+Lakini ujanja wa wenye hila utawaangamiza.+   Mali haitakuwa* na faida yoyote siku ya ghadhabu,+Lakini uadilifu ndio utakaookoa kutoka katika kifo.+   Uadilifu wa mtu asiye na lawama hukinyoosha kijia chake,Lakini mwovu ataanguka kwa sababu ya uovu wake mwenyewe.+   Uadilifu wa wanyoofu utawaokoa,+Lakini wenye hila watanaswa na tamaa zao wenyewe.+   Mtu mwovu anapokufa, tumaini lake hutokomea;Na matarajio aliyokuwa nayo kwa kutegemea nguvu zake hutokomea pia.+   Mwadilifu huokolewa kutoka katika taabu,Na mwovu huingia humo badala yake.+   Kwa kinywa chake mwasi imani* humwangamiza jirani yake,Lakini kwa ujuzi waadilifu huokolewa.+ 10  Wema wa watu waadilifu hulifanya jiji lishangilie,Na waovu wanapoangamia, kunakuwa na kelele za shangwe.+ 11  Jiji hukwezwa kwa sababu ya baraka ya mtu mnyoofu,+Lakini kinywa cha waovu hulibomoa.+ 12  Mtu yeyote asiye na busara* humdharau jirani yake,Lakini mtu mwenye utambuzi wa kweli hukaa kimya.+ 13  Mchongezi huzurura-zurura akifunua mazungumzo ya siri,+Lakini mtu anayeaminika* hutunza siri.* 14  Mwelekezo stadi* unapokosekana, watu huanguka,Lakini washauri wengi huleta mafanikio.*+ 15  Yeyote anayemwekea dhamana ya mkopo* mtu asiyemjua hakika ataumia,+Lakini yeyote anayeepuka* kumpa mkono ili kumdhamini atakuwa salama. 16  Mwanamke mwenye fadhili* hupata utukufu,+Lakini watu wasio na huruma hujitwalia utajiri. 17  Mtu mwenye fadhili* hujinufaisha,*+Lakini mtu mkatili hujiletea shida.*+ 18  Mtu mwovu hupata mshahara wa udanganyifu,+Lakini mtu anayepanda uadilifu hupata thawabu ya kweli.+ 19  Anayetetea uadilifu kwa uthabiti atapata uzima,+Lakini anayefuatia uovu anaelekea kwenye kifo. 20  Waliopotoka moyoni wanamchukiza Yehova,+Lakini wale ambao njia yao haina lawama humfurahisha.+ 21  Uwe na hakika kuhusu hili:* Mtu mwovu hatakosa kuadhibiwa,+Lakini watoto wa mwadilifu wataponyoka. 22  Kama pete ya dhahabu katika pua ya nguruweNdivyo alivyo mwanamke mrembo anayekataa busara. 23  Tamaa ya waadilifu huongoza kwenye mema,+Lakini tumaini la waovu huongoza kwenye ghadhabu. 24  Mtu mmoja hutoa kwa ukarimu* na kupata vitu vingi zaidi;+Mtu mwingine huwanyima wengine wanachostahili, lakini anakuwa maskini.+ 25  Mtu mkarimu atapata ufanisi,*+Na yule anayewaburudisha wengine* yeye mwenyewe ataburudishwa.+ 26  Watu watamlaani anayeficha nafaka,Lakini watambariki anayeiuza. 27  Anayetafuta kwa bidii kutenda mema hutafuta kibali,+Lakini anayetafuta uovu—kwa hakika atapatwa na uovu.+ 28  Anayeutumaini utajiri wake ataanguka,+Lakini waadilifu watasitawi kama majani.+ 29  Yeyote anayewaletea taabu* watu wa nyumbani mwake atarithi upepo,+Na mpumbavu atakuwa mtumishi wa mtu mwenye hekima moyoni. 30  Tunda la mwadilifu ni mti wa uzima,+Na yule anayeziteka* nafsi* ni mwenye hekima.+ 31  Ikiwa, kwa hakika, mtu mwadilifu duniani huthawabishwa,Sembuse mwovu na mtenda dhambi!+

Maelezo ya Chini

Au “jiwe kamili la kupimia.”
Au “udanganyifu.”
Au “Vitu vyenye thamani havitakuwa.”
Au “mtu anayemkataa Mungu.”
Tnn., “aliyepungukiwa moyoni.”
Tnn., “mwaminifu rohoni.”
Tnn., “hufunika jambo.”
Au “Mwongozo wenye hekima.”
Au “wokovu.”
Au “rehani.”
Tnn., “anayechukia.”
Au “anayevutia.”
Au “Mtu mwenye upendo mshikamanifu.”
Au “huitendea mema nafsi yake.”
Au “aibu.”
Tnn., “Mkono kwa mkono.”
Tnn., “hutawanya.”
Tnn., “atanenepeshwa.”
Tnn., “anayewanywesha wengine kwa ukarimu.”
Au “aibu.”
Au “anayezishawishi.”
Angalia Kamusi.