Methali 2:1-22

  • Thamani ya hekima (1-22)

    • Tafuta hekima kama hazina zilizofichika (4)

    • Uwezo wa kufikiri ni ulinzi (11)

    • Uasherati huleta msiba (16-19)

2  Mwanangu, ukiyakubali maneno yanguNa kuhifadhi amri zangu kama hazina,+   Kwa kutega sikio lako usikilize hekima+Na kuuelekeza moyo wako upate utambuzi;+   Pia, ukiuita uelewaji kwa sauti+Na kupaza sauti yako upate utambuzi;+   Ukiendelea kuutafuta kama fedha,*+Na kuendelea kuutafuta sana kama hazina zilizofichika;+   Ndipo utakapoelewa kumwogopa Yehova,+Nawe utapata ujuzi kumhusu Mungu.+   Kwa maana Yehova mwenyewe hutoa hekima;+Na kinywani mwake hutoka ujuzi na utambuzi.   Huwahifadhia wanyoofu hekima inayotumika;Yeye ni ngao kwa wanaotembea kwa utimilifu.+   Huvilinda vijia vya haki,Naye atailinda njia ya washikamanifu wake.+   Ndipo utakapoelewa lililo la uadilifu na la haki na lililo sawa,Njia yote ya lililo jema.+ 10  Hekima inapoingia moyoni mwako+Na ujuzi kupendeza nafsi* yako,+ 11  Uwezo wa kufikiri utakukinga,+Na utambuzi utakulinda, 12  Ili kukuokoa kutoka kwenye njia mbaya,Kutoka kwa mtu anayesema mambo mapotovu,+ 13  Kutoka kwa wale wanaoviacha vijia vya unyoofuIli watembee katika njia za giza,+ 14  Kutoka kwa wale wanaoshangilia kutenda mabaya,Wanaofurahia upotovu wa uovu, 15  Wale ambao vijia vyao vimepindaNa ambao mwenendo wao wote ni wenye hila. 16  Utakuokoa kutoka kwa mwanamke aliyepotoka,*Kutoka kwa maneno laini* ya mwanamke mwasherati,*+ 17  Anayemwacha rafiki wa karibu* wa ujana wake+Na kusahau agano la Mungu wake; 18  Kwa maana nyumba yake huzama katika kifo,Na vijia vyake* huongoza kwa wale waliokufa ambao hawana uwezo.+ 19  Hakuna yeyote anayelala naye* atakayerudi,Wala hawatarudi kwenye vijia vya uzima.+ 20  Basi fuata njia ya watu wemaNa ubaki kwenye vijia vya waadilifu,+ 21  Kwa maana ni wanyoofu tu watakaokaa duniani,Na wasio na lawama* ndio watakaobaki ndani yake.+ 22  Lakini waovu, wataangamizwa kutoka duniani,+Na wenye hila watang’olewa kutoka ndani yake.+

Maelezo ya Chini

Yaani, madini ya fedha.
Angalia Kamusi.
Tnn., “mgeni.” Ni wazi kwamba ni mgeni machoni pa Mungu kwa sababu ya upotovu wa maadili.
Au “maneno yenye ushawishi.”
Tnn., “mgeni.” Ni wazi kwamba ni mgeni machoni pa Mungu kwa sababu ya upotovu wa maadili.
Au “mume.”
Tnn., “mapito yake.”
Tnn., “anayeingia kwake.”
Au “wanaoshika utimilifu.”