Methali 22:1-29

  • Jina jema ni bora kuliko mali nyingi (1)

  • Mazoezi ya mapema ya mtoto yatadumu maisha yake yote (6)

  • Mvivu huogopa kwamba simba yuko nje (13)

  • Nidhamu huondoa ujinga (15)

  • Mfanyakazi stadi huwatumikia wafalme (29)

22  Ni afadhali kuchagua jina jema* kuliko mali nyingi;+Kuheshimiwa* ni bora kuliko fedha na dhahabu.   Matajiri na maskini wanafanana katika jambo hili:* Yehova aliwaumba wote.+   Mtu mwerevu huona hatari na kujificha,Lakini wajinga husonga mbele na kupata madhara.*   Unyenyekevu na kumwogopa Yehova huletaUtajiri na utukufu na uzima.+   Miiba na mitego iko kwenye njia ya mtu aliyepotoka,Lakini yeyote anayethamini uhai wake* hukaa mbali nayo.+   Mzoeze mvulana* njia anayopaswa kuifuata;+Hata atakapozeeka hataiacha.+   Tajiri humtawala maskini,Na mkopaji ni mtumwa wa mkopeshaji.+   Yeyote anayepanda uovu atavuna msiba,+Na fimbo ya ghadhabu yake itaangamia.+   Mtu mkarimu* atabarikiwa,Kwa maana chakula chake humgawia maskini.+ 10  Mfukuze mtu mwenye dhihaka,Na ugomvi utatoweka;Mizozo* na matusi yatakoma. 11  Mtu anayependa moyo safi na ambaye husema maneno yenye fadhiliAtakuwa rafiki ya mfalme.+ 12  Macho ya Yehova huulinda ujuzi,Lakini Yeye huyapindua maneno ya wenye hila.+ 13  Mvivu anasema: “Kuna simba nje! Nitauawa katikati ya uwanja wa jiji!”+ 14  Kinywa cha wanawake waliopotoka* ni shimo refu.+ Anayeshutumiwa na Yehova ataanguka ndani yake. 15  Ujinga umefungwa katika moyo wa mvulana,*+Lakini fimbo ya nidhamu ndiyo itakayouondolea mbali.+ 16  Anayempunja maskini ili aongeze mali yake+Na yule anayewapa zawadi matajiriMwishowe watakuwa maskini. 17  Tega sikio lako usikie maneno ya wenye hekima,+Ili uufanye moyo wako uzingatie ujuzi wangu,+ 18  Kwa maana inapendeza kuyahifadhi ndani yako kabisa,+Ili yote yawe midomoni mwako daima.+ 19  Ili umtegemee Yehova,Ninakupa ujuzi leo. 20  Je, tayari sijakuandikia,Na kukupa mashauri na ujuzi, 21  Ili nikufundishe maneno ya kweli yanayotegemeka,Uweze kumpelekea habari sahihi yule aliyekutuma? 22  Usimwibie mtu maskini kwa kuwa ni maskini,+Wala usimkandamize mtu wa hali ya chini katika lango la jiji,+ 23  Kwa maana Yehova mwenyewe atawatetea+Naye atawaangamiza wanaowapunja. 24  Usiwe na urafiki na mtu mwenye hasira kaliWala kushirikiana na mtu anayekasirika upesi, 25  Ili usijifunze kamwe njia zakeNa kujitia mtegoni.+ 26  Usiwe miongoni mwa wale wanaopeana mikono wanapotoa dhamana,Wanaoweka dhamana kwa ajili ya mikopo.+ 27  Ikiwa huna kitu cha kulipa,Kitanda chako kitavutwa na kuchukuliwa ukiwa umekilalia! 28  Usiisogeze alama ya kale ya mpakaIliyowekwa na mababu zako.+ 29  Je, umemwona mtu aliye stadi katika kazi yake? Atasimama mbele ya wafalme;+Hatasimama mbele ya watu wa kawaida.

Maelezo ya Chini

Tnn., “Kibali.”
Au “sifa njema.” Tnn., “jina.”
Tnn., “hukutana.”
Au “adhabu.”
Au “nafsi yake.”
Au “mtoto; kijana.”
Tnn., “Aliye na jicho zuri.”
Au “Kesi.”
Tnn., “wageni.”
Au “mtoto; kijana.”