Methali 23:1-35

  • Uwe na busara unapokubali mwaliko (2)

  • Usifuatie utajiri (4)

  • Utajiri unaweza kuruka mbali nawe (5)

  • Usiwe miongoni mwa walevi (20)

  • Kileo huuma kama nyoka (32)

23  Ukiketi kula pamoja na mfalme,Chunguza kwa makini kilicho mbele yako;   Tia kisu kwenye koo lako*Ikiwa una hamu kubwa ya chakula.*   Usivitamani vyakula vyake vitamu,Kwa maana ni vyakula vya udanganyifu.   Usijichoshe kupata utajiri.+ Acha, na uonyeshe uelewaji.*   Ukiutupia jicho, haupo,+Kwa maana hakika utaota mabawa kama ya tai na kuruka mbali angani.+   Usile chakula cha mtu mchoyo;*Usivitamani vyakula vyake vitamu,   Kwa maana yeye ni kama mtu anayeweka hesabu.* “Kula na kunywa,” anakuambia, lakini sivyo anavyomaanisha.*   Utatapika matonge uliyokulaNawe utakuwa umepoteza maneno yako ya kumsifu.   Usiongee masikioni mwa mpumbavu,+Kwa maana ataidharau hekima ya maneno yako.+ 10  Usiisogeze alama ya kale ya mpaka+Wala kuingia katika shamba la mayatima. 11  Kwa maana Mtetezi* wao ana nguvu;Atawatetea dhidi yako.+ 12  Ufanye moyo wako uzingatie nidhamuNa sikio lako maneno ya ujuzi. 13  Usimnyime mvulana* nidhamu.+ Ukimpiga kwa fimbo, hatakufa. 14  Unapaswa kumpiga kwa fimbo,Ili umwokoe asiingie Kaburini.* 15  Mwanangu, ikiwa moyo wako utakuwa na hekima,Basi moyo wangu mimi utashangilia.+ 16  Utu wangu wa ndani utashangiliaMidomo yako inaposema mambo yaliyo sawa. 17  Moyo wako usiwaonee wivu watenda dhambi,+Bali mwogope Yehova mchana kutwa,+ 18  Kwa maana ndipo utakapokuwa na wakati ujao+Na tumaini lako halitafutiliwa mbali. 19  Mwanangu, sikiliza uwe na hekima,Na uuelekeze moyo wako katika njia inayofaa. 20  Usiwe miongoni mwa watu wanaokunywa divai nyingi mno,+Miongoni mwa wale wanaokula nyama kwa pupa,+ 21  Kwa maana mlevi na mlafi watakuwa maskini,+Na kusinzia kutamvika mtu matambara. 22  Msikilize baba yako aliyekuzaa,Wala usimdharau mama yako kwa sababu tu amezeeka.+ 23  Inunue* kweli wala usiiuze kamwe,+Pia hekima na nidhamu na uelewaji.+ 24  Baba ya mtu mwadilifu hakika atakuwa na shangwe;Na baba anayemzaa mwana mwenye hekima atamfurahia. 25  Baba yako na mama yako watafurahi,Na mama aliyekuzaa atakuwa na shangwe. 26  Mwanangu, nipe moyo wako,Na macho yako yapendezwe na njia zangu.+ 27  Kwa maana kahaba ni shimo refu,Na mwanamke mwasherati* ni kisima chembamba.+ 28  Hunyemelea kama mnyang’anyi;+Huongeza idadi ya wanaume wasio waaminifu. 29  Ni nani mwenye ole? Ni nani aliye na wasiwasi? Ni nani mwenye ugomvi? Ni nani anayelalamika? Ni nani aliye na majeraha bila sababu? Ni nani aliye na macho mazito?* 30  Ni wale wanaoshinda kwenye divai;+Wale wanaotafuta* divai iliyochanganywa. 31  Usiitazame rangi nyekundu ya divaiInapong’aa katika kikombe na kushuka taratibu, 32  Kwa maana mwishowe huuma kama nyoka,Nayo hutoa sumu kama nyoka kipiri. 33  Macho yako yataona mambo ya ajabu,Na moyo wako utasema mambo yaliyopotoka.+ 34  Nawe utakuwa kama mtu anayelala katikati ya bahari,Kama mtu anayelala juu ya mlingoti wa meli. 35  Utasema: “Wamenipiga, lakini sikuhisi chochote.* Walinipiga, lakini sikujua. Nitaamka lini?+ Nahitaji kinywaji kingine.”*

Maelezo ya Chini

Au “Jizuie.”
Au “una nafsi iliyojaa tamaa.”
Au labda, “Acha kufuata uelewaji wako mwenyewe.”
Au “cha yeyote mwenye jicho ovu.”
Au “anayehesabu katika nafsi yake.”
Tnn., “moyo wake hauko pamoja nawe.”
Tnn., “Mkombozi.”
Au “mtoto; kijana.”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Au “Jipatie.”
Tnn., “mgeni.” Angalia Met 2:16.
Au “macho yaliyochoka.”
Au “wanaokusanyika ili kuonjaonja.”
Au “sikuhisi uchungu.”
Au “Nitaitafuta divai tena.”