Methali 24:1-34

  • Usiwaonee wivu waovu (1)

  • Nyumba hujengwa kwa hekima (3)

  • Mwadilifu anaweza kuanguka lakini atainuka (16)

  • Usilipize kisasi (29)

  • Kusinzia huleta umaskini (33, 34)

24  Usiwaonee wivu waovu,Wala usitamani kushirikiana nao,+   Kwa maana moyo wao hutafakari ukatili,Na midomo yao huongea kuhusu kuwataabisha wengine.   Nyumba* hujengwa kwa hekima,+Na kwa utambuzi hufanywa iwe salama.   Kwa ujuzi vyumba hujazwaKila aina ya hazina zenye thamani na zinazopendeza.+   Mtu mwenye hekima ana nguvu,+Na kwa ujuzi mtu huzidisha nguvu zake.   Kwa mwelekezo stadi* utapigana vita vyako,+Na kupitia washauri wengi kuna ushindi.*+   Mjinga hawezi kupata hekima ya kweli;+Hana lolote la kusema katika lango la jiji.   Yeyote anayepanga njama ya uovuAtaitwa stadi wa kupanga hila.+   Njama za upumbavu* ni dhambi,Na watu humchukia mwenye dhihaka.+ 10  Ukivunjika moyo siku ya taabu,*Nguvu zako zitakuwa chache. 11  Waokoe wale wanaopelekwa kwenye kifo,Na uwazuie wale wanaopepesuka wakielekea kuchinjwa.+ 12  Ukisema: “Lakini hatukujua jambo hili,” Je, Yule anayeichunguza mioyo* hatatambua hilo?+ Naam, Yule anayekutazama atajuaNaye atamlipa kila mwanadamu kulingana na matendo yake.+ 13  Mwanangu, kula asali, kwa sababu ni njema;Asali ya sega ni tamu kinywani. 14  Vivyo hivyo, jua kwamba hekima ina manufaa kwako.*+ Ukiipata, utakuwa na wakati ujaoNa tumaini lako halitafutiliwa mbali.+ 15  Usivizie kwa uovu karibu na makao ya mtu mwadilifu;Usiharibu mahali pake pa kupumzikia. 16  Kwa maana mwadilifu anaweza kuanguka mara saba, lakini atainuka tena,+Lakini waovu watakwazwa na msiba.+ 17  Adui yako akianguka, usishangilie,Na akijikwaa, usiruhusu moyo wako uwe na shangwe;+ 18  La sivyo, Yehova ataona jambo hilo naye hatafurahi,Naye ataiondoa hasira yake kumwelekea.*+ 19  Usifadhaike* kwa sababu ya waovu;Usiwaonee wivu watu waovu, 20  Kwa maana mtu yeyote mwovu hana wakati ujao;+Taa ya waovu itazimwa.+ 21  Mwanangu, mwogope Yehova na mfalme.+ Nawe usishirikiane na waasi,*+ 22  Kwa maana msiba wao utatokea ghafla.+ Ni nani anayejua jinsi wote wawili* watakavyowaangamiza?+ 23  Haya pia ni maneno ya wenye hekima: Kuonyesha upendeleo katika hukumu si jambo zuri.+ 24  Yeyote anayemwambia mtu mwovu, “Wewe ni mwadilifu,”+ Atalaaniwa na watu na kushutumiwa na mataifa. 25  Lakini mambo yatawaendea vema wale wanaomkaripia;+Watapata baraka ya vitu vyema.+ 26  Watu wataibusu midomo ya mtu anayejibu kwa unyoofu.*+ 27  Tayarisha kazi yako ya nje, na utayarishe kila kitu shambani;Kisha uijenge nyumba* yako. 28  Usitoe ushahidi dhidi ya jirani yako pasipo msingi.+ Usiitumie midomo yako kuwadanganya wengine.+ 29  Usiseme: “Nitamtendea kama tu alivyonitendea;Nitamlipiza kwa sababu ya mambo aliyonitendea.”*+ 30  Nilipita karibu na shamba la mtu mvivu,+Karibu na shamba la mizabibu la mtu asiye na busara.* 31  Niliona limejaa magugu;Ardhi ilifunikwa na miiba,Na ukuta wake wa mawe ulikuwa umebomoka.+ 32  Nilitazama hilo na kulitia moyoni;Nililiona na kujifunza somo hili:* 33  Lala kidogo, sinzia kidogo,Kunja mikono kidogo ili upumzike, 34  Na umaskini wako utakuja kama jambazi,Na uhitaji wako kama mwanamume mwenye silaha.+

Maelezo ya Chini

Au “Familia.”
Au “mwongozo wenye hekima.”
Au “wokovu.”
Au “Njama za mpumbavu.”
Au “nyakati za taabu.”
Au “anayechunguza nia.”
Au “ni tamu kwa nafsi yako.”
Yaani, yule adui.
Au “Usiwake hasira.”
Au “wale wanaotaka mabadiliko.”
Yaani, Yehova na mfalme.
Au labda, “Kujibu kwa unyoofu ni kama kumbusu mtu.”
Au “familia.”
Au “Nitamlipa sawasawa na matendo yake.”
Tnn., “aliyepungukiwa moyoni.”
Tnn., “Nilipokea nidhamu.”