Methali 25:1-28

  • Kutunza siri (9)

  • Maneno yaliyochaguliwa vizuri (11)

  • Kuheshimu faragha ya wengine (17)

  • Kukusanya makaa ya mawe juu ya kichwa cha adui (21, 22)

  • Habari njema ni kama maji baridi (25)

25  Hizi pia ni methali za Sulemani+ zilizonakiliwa* na watu wa Hezekia+ mfalme wa Yuda:   Ni utukufu wa Mungu kutunza jambo likiwa siri,+Na utukufu wa wafalme ni kulichunguza jambo kabisa.   Kama mbingu zilivyo juu na kama dunia ilivyo na kina,Ndivyo moyo wa wafalme usivyochunguzika.   Ondoa takataka katika fedha,Nayo itakuwa safi kabisa.+   Mwondoe mtu mwovu mbele ya mfalme,Na kiti chake cha ufalme kitaimarishwa kabisa katika uadilifu.+   Usijiheshimu mwenyewe mbele ya mfalme,+Wala usijiingize miongoni mwa watu mashuhuri,+   Kwa maana ni afadhali yeye akuambie, “Njoo hapa juu,” Kuliko akuaibishe mbele ya mkuu.+   Usiharakishe kupeleka kesi mahakamani,Kwa maana utafanya nini baadaye jirani yako akikuaibisha?+   Suluhisha jambo hilo na jirani yako,+Lakini usifunue uliyoambiwa sirini,*+ 10  Ili anayesikiliza asikuaibisheNawe ueneze habari mbaya ambayo haiwezi* kubatilishwa. 11  Kama matofaa ya dhahabu yaliyonakshiwa kwenye vyombo vya fedhaNdivyo lilivyo neno linalosemwa wakati unaofaa.+ 12  Kama kipuli cha dhahabu na pambo la dhahabu boraNdivyo alivyo mkaripiaji mwenye hekima kwa sikio linalosikia.+ 13  Kama baridi ya theluji siku ya mavunoNdivyo alivyo mjumbe mwaminifu kwa wale wanaomtuma,Kwa maana yeye humburudisha bwana wake.+ 14  Kama mawingu na upepo usioleta mvuaNdivyo alivyo mtu anayejigamba kwamba atatoa zawadi lakini haitoi kamwe.*+ 15  Kwa subira kamanda hushawishiwa,Na ulimi laini* unaweza kuvunja mfupa.+ 16  Ukipata asali, kula kiasi kinachokutosha,Kwa maana ukiila kupita kiasi, huenda ukaitapika.+ 17  Mguu wako na uwe haba katika nyumba ya jirani yako,Ili asikuchoke na kukuchukia. 18  Kama rungu la vita na upanga na mshale mkaliNdivyo alivyo mtu anayetoa ushahidi wa uwongo dhidi ya jirani yake.+ 19  Kama jino lililovunjika au mguu unaochechemeaNdivyo ilivyo kumtumaini mtu asiyetegemeka* nyakati za taabu. 20  Kama mtu anayevua nguo siku ya baridiNa kama siki iliyomwagwa kwenye magadiNdivyo alivyo mtu anayeuimbia nyimbo moyo wenye huzuni.+ 21  Ikiwa adui yako* ana njaa, mpe mkate ale;Ikiwa ana kiu, mpe maji anywe,+ 22  Kwa maana utakuwa unakusanya makaa ya mawe yanayowaka juu ya kichwa chake,*+Na Yehova atakuthawabisha. 23  Upepo wa kaskazini huleta mvua,Na ulimi unaopiga porojo huleta uso wenye hasira.+ 24  Ni afadhali kuishi pembeni juu ya paaKuliko kuishi katika nyumba moja na mke mgomvi.*+ 25  Kama maji baridi kwa nafsi* iliyochokaNdivyo ilivyo habari njema kutoka nchi ya mbali.+ 26  Kama chemchemi yenye matope na kisima kilichochafuliwaNdivyo alivyo mtu mwadilifu anayekubali kumfuata* mtu mwovu. 27  Si vizuri kula asali nyingi mno,+Wala si utukufu kujitafutia utukufu wako mwenyewe.+ 28  Kama jiji lililobomolewa, lisilo na ukuta,Ndivyo alivyo mtu asiyeweza kuidhibiti hasira yake.*+

Maelezo ya Chini

Au “zilizonakiliwa na kukusanywa.”
Au “usifunue siri za wengine.”
Au “uvumi unaodhuru ambao hauwezi.”
Tnn., “kuhusu zawadi ya uwongo.”
Au “mpole.”
Au labda, “mtu mwenye hila.”
Tnn., “anayekuchukia.”
Yaani, kupunguza uadui wake na kuyeyusha ugumu wake.
Au “msumbufu.”
Angalia Kamusi.
Au “anayekubaliana na.” Tnn., “anayepepesuka mbele ya.”
Au “asiyeweza kuizuia roho yake.”