Methali 26:1-28
26 Kama theluji wakati wa kiangazi na mvua wakati wa mavuno,Ndivyo heshima isivyomfaa mpumbavu.+
2 Kama ndege alivyo na sababu ya kukimbia na mbayuwayu kuruka,Ndivyo laana isivyokuja bila sababu nzuri.*
3 Mjeledi ni wa farasi, lijamu ni ya punda,+Na fimbo ni ya mgongo wa watu wapumbavu.+
4 Usimjibu mpumbavu kulingana na ujinga wake,Ili usiwe kama yeye.*
5 Mjibu mpumbavu kulingana na ujinga wake,Ili asifikiri kwamba ana hekima.+
6 Kama mtu anayeilemaza miguu yake na kujidhuru mwenyewe*Ndivyo alivyo mtu anayemkabidhi mambo mpumbavu.
7 Kama miguu inayochechemea* ya walemavu,Ndivyo ilivyo methali kinywani mwa watu wapumbavu.+
8 Kama jiwe linavyofungwa kwenye kombeo,Ndivyo ilivyo kumpa utukufu mtu mpumbavu.+
9 Kama mmea wa miiba mkononi mwa mlevi,Ndivyo ilivyo methali kinywani mwa watu wapumbavu.
10 Kama mpiga mishale anayemjeruhi yeyote yule,*Ndivyo alivyo mtu anayemwajiri mpumbavu au wapita njia.
11 Kama mbwa anayerudia matapishi yake,Ndivyo mpumbavu anavyorudia ujinga wake.+
12 Je, umemwona mtu anayefikiri ana hekima?+
Kuna tumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko kwa mtu huyo.
13 Mvivu anasema: “Kuna mwanasimba barabarani,Kuna simba katika uwanja wa jiji!”+
14 Mlango huzunguka-zunguka katika bawaba zake,*Na mvivu hugeuka-geuka kitandani mwake.+
15 Mvivu huutumbukiza* mkono wake katika bakuli la karamu,Lakini amechoka sana kuurudisha kinywani mwake.+
16 Mvivu hufikiri kwamba ana hekima zaidiKuliko watu saba wanaojibu kwa busara.
17 Kama mtu anayemkamata mbwa masikioNdivyo alivyo mpita njia anayekasirishwa na* ugomvi usiomhusu.+
18 Kama mwenda wazimu anayetupa vishale vinavyowaka moto, mishale, na kifo*
19 Ndivyo alivyo mtu anayemhadaa jirani yake na kusema, “Nilikuwa nikifanya mzaha tu!”+
20 Pasipo na kuni moto huzimika,Na pasipo na mchongezi, ugomvi hukoma.+
21 Kama makaa yanavyoongezwa kwenye makaa yanayozimika na kuni zinavyoongezwa motoni,Ndivyo mtu mgomvi anavyochochea ugomvi.+
22 Maneno ya mchongezi ni kama matonge matamu;*Humezwa na kushuka tumboni moja kwa moja.+
23 Kama fedha inayopakwa juu ya chombo cha udongoNdivyo yalivyo maneno ya upendo yanayotoka katika* moyo mwovu.+
24 Anayewachukia wengine huficha chuki hiyo kwa midomo yake,Lakini ndani amesitiri udanganyifu.
25 Ingawa anaongea kwa fadhili, usimwamini,Kwa maana kuna mambo saba yanayochukiza moyoni mwake.*
26 Ingawa chuki yake imefichwa kwa udanganyifu,Uovu wake utafunuliwa kutanikoni.
27 Anayechimba shimo ataanguka ndani yake,Na yeyote anayebingirisha jiwe—litamrudia.+
28 Ulimi unaosema uwongo huwachukia watu uliowaponda,Na kinywa kinachosifusifu huleta uharibifu.+
Maelezo ya Chini
^ Au labda, “Ndivyo laana isiyostahiliwa isivyompata mtu.”
^ Au “Ili usilingane naye.”
^ Tnn., “kunywa ukatili.”
^ Au “inayoning’inia.”
^ Au “anayemjeruhi kila mtu.”
^ Au “maegemeo yake.”
^ Tnn., “huuzika.”
^ Au labda, “anayejiingiza katika.”
^ Au “mishale inayoua.”
^ Au “vitu vinavyomezwa kwa pupa.”
^ Tnn., “Ndivyo ilivyo midomo yenye shauku pamoja na.”
^ Au “Kwa maana moyo wake unachukiza kabisa.”