Methali 26:1-28

  • Ufafanuzi kuwahusu watu wavivu (13-16)

  • Epuka ugomvi usiokuhusu (17)

  • Epuka mizaha inayodhuru (18, 19)

  • Pasipo na kuni, moto huzimika (20, 21)

  • Maneno ya mchongezi ni kama matonge matamu (22)

26  Kama theluji wakati wa kiangazi na mvua wakati wa mavuno,Ndivyo heshima isivyomfaa mpumbavu.+   Kama ndege alivyo na sababu ya kukimbia na mbayuwayu kuruka,Ndivyo laana isivyokuja bila sababu nzuri.*   Mjeledi ni wa farasi, lijamu ni ya punda,+Na fimbo ni ya mgongo wa watu wapumbavu.+   Usimjibu mpumbavu kulingana na ujinga wake,Ili usiwe kama yeye.*   Mjibu mpumbavu kulingana na ujinga wake,Ili asifikiri kwamba ana hekima.+   Kama mtu anayeilemaza miguu yake na kujidhuru mwenyewe*Ndivyo alivyo mtu anayemkabidhi mambo mpumbavu.   Kama miguu inayochechemea* ya walemavu,Ndivyo ilivyo methali kinywani mwa watu wapumbavu.+   Kama jiwe linavyofungwa kwenye kombeo,Ndivyo ilivyo kumpa utukufu mtu mpumbavu.+   Kama mmea wa miiba mkononi mwa mlevi,Ndivyo ilivyo methali kinywani mwa watu wapumbavu. 10  Kama mpiga mishale anayemjeruhi yeyote yule,*Ndivyo alivyo mtu anayemwajiri mpumbavu au wapita njia. 11  Kama mbwa anayerudia matapishi yake,Ndivyo mpumbavu anavyorudia ujinga wake.+ 12  Je, umemwona mtu anayefikiri ana hekima?+ Kuna tumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko kwa mtu huyo. 13  Mvivu anasema: “Kuna mwanasimba barabarani,Kuna simba katika uwanja wa jiji!”+ 14  Mlango huzunguka-zunguka katika bawaba zake,*Na mvivu hugeuka-geuka kitandani mwake.+ 15  Mvivu huutumbukiza* mkono wake katika bakuli la karamu,Lakini amechoka sana kuurudisha kinywani mwake.+ 16  Mvivu hufikiri kwamba ana hekima zaidiKuliko watu saba wanaojibu kwa busara. 17  Kama mtu anayemkamata mbwa masikioNdivyo alivyo mpita njia anayekasirishwa na* ugomvi usiomhusu.+ 18  Kama mwenda wazimu anayetupa vishale vinavyowaka moto, mishale, na kifo* 19  Ndivyo alivyo mtu anayemhadaa jirani yake na kusema, “Nilikuwa nikifanya mzaha tu!”+ 20  Pasipo na kuni moto huzimika,Na pasipo na mchongezi, ugomvi hukoma.+ 21  Kama makaa yanavyoongezwa kwenye makaa yanayozimika na kuni zinavyoongezwa motoni,Ndivyo mtu mgomvi anavyochochea ugomvi.+ 22  Maneno ya mchongezi ni kama matonge matamu;*Humezwa na kushuka tumboni moja kwa moja.+ 23  Kama fedha inayopakwa juu ya chombo cha udongoNdivyo yalivyo maneno ya upendo yanayotoka katika* moyo mwovu.+ 24  Anayewachukia wengine huficha chuki hiyo kwa midomo yake,Lakini ndani amesitiri udanganyifu. 25  Ingawa anaongea kwa fadhili, usimwamini,Kwa maana kuna mambo saba yanayochukiza moyoni mwake.* 26  Ingawa chuki yake imefichwa kwa udanganyifu,Uovu wake utafunuliwa kutanikoni. 27  Anayechimba shimo ataanguka ndani yake,Na yeyote anayebingirisha jiwe—litamrudia.+ 28  Ulimi unaosema uwongo huwachukia watu uliowaponda,Na kinywa kinachosifusifu huleta uharibifu.+

Maelezo ya Chini

Au labda, “Ndivyo laana isiyostahiliwa isivyompata mtu.”
Au “Ili usilingane naye.”
Tnn., “kunywa ukatili.”
Au “inayoning’inia.”
Au “anayemjeruhi kila mtu.”
Au “maegemeo yake.”
Tnn., “huuzika.”
Au labda, “anayejiingiza katika.”
Au “mishale inayoua.”
Au “vitu vinavyomezwa kwa pupa.”
Tnn., “Ndivyo ilivyo midomo yenye shauku pamoja na.”
Au “Kwa maana moyo wake unachukiza kabisa.”