Methali 27:1-27

  • Karipio kutoka kwa rafiki hunufaisha (5, 6)

  • Mwanangu, ufanye moyo wangu ushangilie (11)

  • Chuma hunoa chuma (17)

  • Lijue kundi lako (23)

  • Mali haidumu milele (24)

27  Usijigambe kuhusu kesho,Kwa maana hujui siku italeta nini.*+   Acha mtu mwingine* akusifu, wala si kinywa chako mwenyewe;Wengine,* wala si midomo yako mwenyewe.+   Jiwe ni zito na mchanga ni mzito sana,Lakini usumbufu unaosababishwa na mjinga ni mzito kuliko vyote viwili.+   Kuna ukatili wa ghadhabu na mafuriko ya hasira,Lakini ni nani anayeweza kustahimili wivu?+   Karipio la wazi ni afadhali kuliko upendo uliofichwa.+   Majeraha yanayosababishwa na rafiki ni ya uaminifu,+Lakini mabusu ya adui ni mengi.*   Yule aliyetosheleza hamu yake hukataa* asali ya sega,Lakini kwa mwenye njaa, hata kilicho kichungu ni kitamu.   Kama ndege anayeenda* mbali kutoka kwenye kiota chakeNdivyo alivyo mtu anayetangatanga mbali kutoka nyumbani kwake.   Mafuta na uvumba huufanya moyo ushangilie;Ndivyo ulivyo urafiki mtamu unaochipuka kutokana na shauri la unyoofu.*+ 10  Usimwache rafiki yako au rafiki ya baba yako,Wala usiingie katika nyumba ya ndugu yako siku ya msiba wako;Ni afadhali jirani aliye karibu kuliko ndugu aliye mbali.+ 11  Uwe na hekima, mwanangu, na kuufanya moyo wangu ushangilie,+Ili niweze kumjibu yule anayenidhihaki.+ 12  Mtu mwerevu huona hatari na kujificha,+Lakini wajinga husonga mbele na kupata madhara.* 13  Chukua vazi la mtu ikiwa amemdhamini mtu asiyemjua;Chukua dhamana kutoka kwake ikiwa alimfanyia hivyo mwanamke mgeni.*+ 14  Mtu akimbariki jirani yake kwa sauti kubwa asubuhi na mapema,Itaonwa kuwa laana. 15  Mke mgomvi* ni kama paa linalovuja maji mfululizo siku ya mvua.+ 16  Yeyote anayeweza kumzuia anaweza kuuzuia upepoNaye anaweza kuyakamata mafuta kwa mkono wake wa kulia. 17  Kama chuma kinavyonoa chuma,Ndivyo mtu anavyomnoa* rafiki yake.+ 18  Anayeutunza mtini atakula matunda yake,+Na anayemtunza bwana wake ataheshimiwa.+ 19  Kama maji yanavyoonyesha* uso wa mtu,Ndivyo moyo wa mtu unavyoonyesha* moyo wa mwingine. 20  Kaburi na mahali pa maangamizi* havitosheki kamwe,+Wala macho ya mwanadamu hayatosheki kamwe. 21  Chungu cha kusafishia ni kwa ajili ya fedha na tanuru ni kwa ajili ya dhahabu,+Vivyo hivyo mtu hupimwa kwa sifa anayopokea.* 22  Hata ukimtwanga mpumbavu kwa mchi*Kama nafaka iliyopondwa katika kinu,Upumbavu wake hautamtoka. 23  Unapaswa kujua vizuri hali ya kundi lako. Watunze vizuri* kondoo wako,+ 24  Kwa maana mali haidumu milele,+Wala taji halidumu vizazi vyote. 25  Majani mabichi hutoweka, na majani mapya huchipuka,Na majani ya milimani yanakusanywa. 26  Wanakondoo dume hukupatia mavazi yako,Na mbuzi dume hukupatia malipo ya shamba. 27  Nawe utakuwa na maziwa ya mbuzi yanayotosha kukulisha wewe,Kuilisha familia yako, na kuwategemeza vijakazi wako.

Maelezo ya Chini

Tnn., “itazaa nini.”
Tnn., “mtu asiyekujua.”
Tnn., “Wageni.”
Au labda, “si ya unyoofu; ni ya kulazimishwa.”
Tnn., “huikanyagia chini.”
Au “anayekimbia.”
Au “shauri la nafsi.”
Au “adhabu.”
Au “mgeni.”
Au “msumbufu.”
Tnn., “anavyounoa uso wa.”
Au “yanavyoakisi.”
Au “unavyoakisi.”
Au “Sheoli na Abadoni.”
Au “Vivyo hivyo mtu hulingana na sifa yake.”
Au “mtwangio.”
Au “Uweke moyo kwa; Wakazie uangalifu.”