Methali 28:1-28

  • Sala ya mtu asiyesikiliza inachukiza (9)

  • Anayeungama huonyeshwa rehema (13)

  • Anayeharakisha kupata utajiri hatakosa hatia (20)

  • Karipio ni bora kuliko kusifusifu (23)

  • Mtu mkarimu hakosi chochote (27)

28  Waovu hukimbia ingawa hakuna yeyote anayewakimbiza,Lakini waadilifu wana ujasiri kama simba.*+   Kunapokuwa na uovu* nchini, nchi inakuwa na kiongozi mmoja baada ya mwingine,+Lakini kwa msaada wa mtu mwenye utambuzi na ujuzi, kiongozi atadumu kwa muda mrefu.+   Mtu maskini anayempunja mtu wa hali ya chini+Ni kama mvua inayofagilia mbali chakula chote.   Wale wanaoiacha sheria humsifu mtu mwovu,Lakini wale wanaoishika sheria huwakasirikia.+   Waovu hawawezi kuelewa haki,Lakini wale wanaomtafuta Yehova wanaweza kuelewa mambo yote.+   Ni afadhali maskini anayetembea kwa utimilifu wakeKuliko tajiri ambaye njia zake zimepotoka.+   Mwana mwenye uelewaji hushika sheria,Lakini rafiki ya walafi humwaibisha baba yake.+   Anayezidisha mali zake kwa faida+ na ribaHumkusanyia yule anayemtendea maskini kwa fadhili.+   Anayekataa kusikiliza sheria—Hata sala yake inachukiza.+ 10  Anayempotosha mnyoofu afuate njia ya uovu ataanguka katika shimo lake mwenyewe,+Lakini wasio na lawama watarithi kilicho chema.+ 11  Tajiri hujiona mwenyewe kuwa mwenye hekima,+Lakini mtu maskini aliye na utambuzi anaweza kumchunguza kabisa.+ 12  Waadilifu wanaposhinda, kuna utukufu mwingi,Lakini waovu wanapopata mamlaka, watu hujificha.+ 13  Anayefunika makosa yake hatafanikiwa,+Lakini yeyote anayeyaungama na kuyaacha ataonyeshwa rehema.+ 14  Mwenye furaha ni mtu aliye chonjo sikuzote,*Lakini yeyote anayeufanya moyo wake kuwa mgumu ataanguka katika msiba.+ 15  Kama simba anayenguruma na dubu anayeshambuliaNdivyo alivyo mtawala mwovu anayewatawala watu wasio na uwezo.+ 16  Kiongozi asiye na utambuzi hutumia vibaya mamlaka yake,+Lakini mtu anayechukia faida isiyo ya haki atarefusha maisha yake.+ 17  Mtu aliyelemewa na hatia ya damu kwa sababu ya kumuua mwingine* ataendelea kukimbia mpaka kaburini.*+ Mtu yeyote asimsaidie. 18  Anayetembea bila kosa ataokolewa,+Lakini yule ambaye njia zake zimepotoka ataanguka ghafla.+ 19  Anayelima ardhi yake atakuwa na chakula kingi,*Lakini anayefuatia vitu visivyo na thamani atakuwa na umaskini wa kutosha.+ 20  Mtu mwaminifu atapata baraka nyingi,+Lakini anayeharakisha kupata utajiri hatabaki bila hatia.+ 21  Si vema kuonyesha upendeleo;+Lakini mtu anaweza kukosea kwa sababu ya kipande cha mkate. 22  Mtu mwenye wivu* hujitahidi sana kupata mali,Lakini hajui kwamba umaskini utamkumba. 23  Yeyote anayemkaripia mwingine+ hatimaye atapata kibali zaidi+Kuliko mtu anayesifusifu kwa ulimi wake. 24  Yeyote anayemwibia baba yake na mama yake na kusema, “Si kosa,”+ Ni rafiki ya mtu anayesababisha uharibifu.+ 25  Mtu mwenye pupa* huchochea mgawanyiko,Lakini yeyote anayemtegemea Yehova atapata ufanisi.*+ 26  Yeyote anayeutumaini moyo wake mwenyewe ni mpumbavu,+Lakini anayetembea kwa hekima ataponyoka.+ 27  Yeyote anayewapa maskini hatakosa chochote,+Lakini yule anayewafumbia macho atapata laana nyingi. 28  Waovu wanapopata mamlaka, mtu hujificha,Lakini wanapoangamia, waadilifu huongezeka.+

Maelezo ya Chini

Au “mwanasimba.”
Au “uasi.”
Au “anayeogopa nyakati zote.”
Au “aliyelemewa na damu ya nafsi.”
Au “shimoni.”
Tnn., “mkate mwingi.”
Au “pupa.”
Au labda, “Nafsi yenye kiburi.”
Tnn., “atanenepeshwa.”