Methali 29:1-27

  • Mtoto aliyeachiliwa huleta aibu (15)

  • Bila maono, watu hutenda wapendavyo (18)

  • Mtu mwenye hasira huchochea ugomvi (22)

  • Mtu mnyenyekevu hupata utukufu (23)

  • Kuwaogopa wanadamu ni mtego (25)

29  Mtu anayeifanya shingo yake kuwa ngumu baada ya kukaripiwa sana+Atavunjwa kwa ghafla, naye hataweza kupona.+   Waadilifu wanapokuwa wengi, watu hushangilia,Lakini mwovu anapotawala, watu hulia kwa maumivu.+   Mtu anayependa hekima humfanya baba yake ashangilie,+Lakini rafiki ya makahaba hutumia vibaya mali yake.+   Kwa haki mfalme huleta uthabiti nchini,+Lakini mtu anayetafuta rushwa huiharibu.   Mtu anayemsifusifu jirani yakeAnautandaza wavu wa kuinasa miguu yake.+   Kosa la mtu mbaya humnasa yeye mwenyewe,+Lakini mwadilifu hupaza sauti kwa shangwe na kufurahi.+   Mwadilifu hujali haki za kisheria za maskini,+Lakini mwovu hajali kamwe.+   Watu wanaojigamba huuwasha moto mji,+Lakini wenye hekima hutuliza hasira.+   Mtu mwenye hekima anapobishana na mpumbavu,Kutakuwa na kelele na dhihaka, lakini hawataridhika.+ 10  Watu wenye kiu ya damu humchukia mtu yeyote asiye na hatia,*+Nao hujaribu kumuua mnyoofu.* 11  Mtu mpumbavu humwaga hisia zake zote,*+Lakini mwenye hekima huzizuia kwa utulivu.+ 12  Mtawala anaposikiliza uwongo,Watumishi wake wote watakuwa waovu.+ 13  Maskini na mkandamizaji wanafanana katika jambo hili:* Yehova huyapa nuru macho ya wote wawili.* 14  Mfalme anapowahukumu maskini kwa haki,+Kiti chake cha ufalme kitakuwa salama daima.+ 15  Fimbo* na karipio hufunza hekima,+Lakini mtoto aliyeachiliwa humwaibisha mama yake. 16  Waovu wanapoongezeka, uovu huongezeka,Lakini waadilifu watawaona wakianguka.+ 17  Mtie nidhamu mwana wako naye atakupumzisha;Atakufurahisha sana.+ 18  Wakati hakuna maono,* watu hufanya wapendavyo,+Lakini wenye furaha ni wale wanaoishika sheria.+ 19  Mtumishi hatakubali kurekebishwa kwa maneno,Kwa maana ingawa anaelewa, hatii.+ 20  Je, umemwona mtu anayeongea bila kufikiri?+ Kuna tumaini zaidi kwa mjinga kuliko yeye.+ 21  Mtumishi akibembelezwa tangu ujana wake,Baadaye atakuwa mtu asiye na shukrani. 22  Mtu anayekasirika upesi huchochea ugomvi;+Yeyote aliye mwepesi wa ghadhabu hufanya makosa mengi.+ 23  Kiburi cha mtu kitamnyenyekeza,+Lakini yeyote aliye mnyenyekevu rohoni atapata utukufu.+ 24  Rafiki ya mwizi hujichukia mwenyewe. Huenda akasikia tangazo la kutoa ushahidi,* lakini hatoi habari yoyote.+ 25  Kuwaogopa* wanadamu ni mtego,+Lakini yule anayemtumaini Yehova atalindwa.+ 26  Watu wengi hutaka kukutana na* mfalme,Lakini mtu hupata haki kutoka kwa Yehova.+ 27  Mtu asiyetenda haki humchukiza mwadilifu,+Lakini yule ambaye njia yake imenyooka humchukiza mwovu.+

Maelezo ya Chini

Au “lawama.”
Au labda, “Lakini mnyoofu hujaribu kuulinda uhai wake.”
Tnn., “roho yake yote.”
Tnn., “hukutana pamoja.”
Yaani, Huwapa uhai.
Au “Nidhamu; Adhabu.”
Au “maono ya kinabii; ufunuo.”
Au “kiapo kinachohusisha laana.”
Au “Kutetemeshwa na.”
Au labda, “kutafuta kibali cha.” Tnn., “kuutafuta uso wa.”