Methali 30:1-33

  • MANENO YA AGURI (1-33)

    • Usinipe umaskini wala utajiri (8)

    • Vitu visivyotosheka kamwe (15, 16)

    • Vitu visivyoacha alama (18, 19)

    • Mwanamke mzinzi (20)

    • Wanyama wenye hekima ya kisilika (24)

30  Ujumbe mzito wa Aguri mwana wa Yake, aliomwambia Ithieli, naam, Ithieli na Ukali.   Mimi ni mjinga kuliko mtu yeyote yule,+Nami sina uelewaji ambao mwanadamu anapaswa kuwa nao.   Sijajifunza hekima,Nami sina ujuzi kumhusu Aliye Mtakatifu Zaidi.   Ni nani amepanda mbinguni kisha akashuka?+ Ni nani ameukusanya upepo katika viganja vyake viwili? Ni nani ameyafunga maji katika vazi lake?+ Ni nani ameimarisha* miisho yote ya dunia?+ Jina lake ni nani nalo jina la mwana wake ni nani—ikiwa unajua?   Kila neno la Mungu ni safi.+ Yeye ni ngao kwa wale wanaomkimbilia.+   Usiongeze chochote katika maneno yake,+La sivyo atakukaripia,Nawe utathibitika kuwa mwongo.   Ninakuomba mambo mawili. Usininyime mambo hayo kabla sijafa.   Yaondolee mbali nami mambo yasiyo ya kweli na ya uwongo.+ Usinipe umaskini wala utajiri. Acha nile tu fungu langu la chakula,+   Ili nisishibe na kukukana na kusema, “Yehova ni nani?”+ Wala usiruhusu niwe maskini, niibe na kuliaibisha* jina la Mungu wangu. 10  Usimchongee mtumishi kwa bwana wake,La sivyo atakulaani, nawe utapatikana na hatia.+ 11  Kuna kizazi kinachomtukana baba yaoNacho hakimbariki mama yao.+ 12  Kuna kizazi kinachojiona kuwa safi+Lakini hakijasafishwa uchafu wake.* 13  Kuna kizazi chenye macho yaliyojaa kiburiNa ambacho macho yake yanatazama kwa majivuno mengi!+ 14  Kuna kizazi ambacho meno yake ni mapangaNa ambacho mataya yake ni visu vya kuchinjia;Wanawanyafua watu wa hali ya chini dunianiNa maskini kutoka miongoni mwa wanadamu.+ 15  Ruba wana mabinti wawili wanaolia, “Nipe! Nipe!” Kuna vitu vitatu visivyotosheka,Vinne ambavyo havisemi kamwe, “Inatosha!” 16  —Kaburi*+ na tumbo lisiloweza kuzaa,Nchi iliyonyimwa maji,Na moto ambao kamwe hausemi, “Inatosha!” 17  Jicho linalomdhihaki baba na kudharau kumtii mama+—Kunguru wa bondeni* wataling’oa,Na tai wachanga watalila.+ 18  Kuna mambo matatu yanayozidi ufahamu wangu,*Na manne ambayo siyaelewi: 19  Njia ya tai angani,Njia ya nyoka juu ya mwamba,Njia ya meli baharini,Na njia ya mwanamume pamoja na mwanamwali. 20  Hii ndiyo njia ya mwanamke mzinzi: Anakula, anajipangusa kinywa;Kisha anasema, “Sijafanya kosa lolote.”+ 21  Kuna mambo matatu yanayoitetemesha duniaNa mambo manne ambayo haiwezi kuvumilia: 22  Mtumwa anapotawala akiwa mfalme,+Mjinga anaposhiba kupita kiasi, 23  Mwanamke anayechukiwa* anapoolewa,Na kijakazi anapochukua nafasi ya bimkubwa wake.+ 24  Kuna vitu vinne duniani ambavyo ni miongoni mwa vitu vidogo zaidi,Lakini vina hekima ya kisilika:*+ 25  Chungu si viumbe wenye nguvu,*Lakini wanatayarisha chakula chao wakati wa kiangazi.+ 26  Wibari*+ si viumbe wenye nguvu,*Lakini wanajenga nyumba zao kwenye majabali.+ 27  Nzige+ hawana mfalme,Lakini wote husonga mbele kwa mpangilio.*+ 28  Mjusi+ hushika kwa miguu yake,Naye huingia katika jumba la mfalme. 29  Kuna viumbe watatu wenye mwendo unaovutia,Wanne wenye mwendo wa madaha: 30  Simba, mnyama mwenye nguvu zaidi kuliko wanyama wote,Ambaye hamkimbii yeyote;+ 31  Mbwa mwindaji; mbuzi dume;Na mfalme aliye pamoja na jeshi lake. 32  Ikiwa umejikweza kwa ujinga+Au ikiwa umepanga kufanya hivyo,Funika kinywa chako kwa mkono wako.+ 33  Kwa maana kama vile kusukasuka maziwa kunavyotokeza siagiNa kufinya pua kunavyofanya damu itoke,Ndivyo kuchochea hasira kunavyotokeza ugomvi.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “ameinua.”
Au “kulishambulia.”
Tnn., “kinyesi chake.”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Au “korongoni.”
Au “ambayo ni ya ajabu sana kwangu.”
Au “ambaye hapendwi.”
Au “hekima kupindukia.”
Tnn., “si taifa lenye nguvu.”
Tnn., “si taifa lenye nguvu.”
Au “Pelele.”
Au “vikundi-vikundi.”