Methali 4:1-27

  • Mafundisho ya baba yenye hekima (1-27)

    • Zaidi ya yote, pata hekima (7)

    • Epuka vijia vya uovu (14, 15)

    • Kijia cha waadilifu huzidi kung’aa (18)

    • “Ulinde moyo wako” (23)

4  Wanangu, sikilizeni nidhamu ya baba;+Sikilizeni kwa makini ili mpate uelewaji,   Kwa maana nitawapa mafundisho mema;Msiache mafundisho* yangu.+   Nilikuwa mwana halisi wa baba yangu+Na mama yangu alinipenda sana.+   Baba alinifundisha na kusema: “Moyo wako na ushike kabisa maneno yangu.+ Shika amri zangu, uendelee kuishi.+   Jipatie hekima, jipatie uelewaji.+ Usisahau, wala usiache ninayosema.   Usiiache, nayo itakukinga. Ipende, nayo itakulinda.   Hekima ndilo jambo muhimu zaidi,*+ kwa hiyo jipatie hekima,Pamoja na vyote unavyojipatia, jipatie uelewaji.+   Ithamini sana, nayo itakukweza.+ Itakuheshimu kwa sababu unaikumbatia.+   Itakuvika shada lenye kuvutia kichwani;Itakupamba kwa taji maridadi.” 10  Mwanangu, sikiliza maneno yangu na uyakubali,Na miaka ya maisha yako itakuwa mingi.+ 11  Nitakufundisha katika njia ya hekima;+Nitakuongoza katika vijia vya unyoofu.+ 12  Unapotembea, hatua zako hazitazuiwa;Na ukikimbia, hutajikwaa. 13  Shika kabisa nidhamu; usiiache.+ Ilinde, kwa maana ni uzima wako.+ 14  Usiingie katika kijia cha waovu,Wala usitembee katika njia ya watu wabaya.+ 15  Iepuke, usiifuate;+Jiepushe nayo, pita mbali nayo.+ 16  Kwa maana hawawezi kulala wasipotenda uovu. Hawapati usingizi wasipomwangusha mtu. 17  Wanajilisha mkate wa uovu,Na kunywa divai ya ukatili. 18  Lakini kijia cha waadilifu ni kama nuru nyangavu ya asubuhiInayong’aa zaidi na zaidi mpaka mchana kamili.+ 19  Njia ya waovu ni kama giza;Hawajui ni nini kinachowafanya wajikwae. 20  Mwanangu, sikiliza maneno yangu;Sikiliza kwa makini* ninayokwambia. 21  Yasiondoke machoni pako;Yaweke ndani kabisa moyoni mwako,+ 22  Kwa maana ni uzima kwa wale wanaoyapata+Na afya kwa mwili wao wote. 23  Ulinde moyo wako kuliko vitu vyote unavyolinda,+Kwa maana humo ndimo zinamotoka chemchemi za uzima. 24  Jiepushe kabisa na maneno yaliyopotoka,+Na ujitenge mbali na mazungumzo yenye hila. 25  Macho yako yanapaswa kutazama mbele moja kwa moja,Naam, yakaze macho yako* moja kwa moja mbele yako.+ 26  Lainisha* mapito ya miguu yako,+Na njia zako zote zitakuwa thabiti. 27  Usielekee kulia wala kushoto.+ Iepushe miguu yako na lililo ovu.

Maelezo ya Chini

Au “sheria.”
Au “la msingi.”
Tnn., “Yategee sikio.”
Au “macho yako yanayong’aa.”
Au labda, “Chunguza kwa makini.”