Methali 5:1-23

  • Onyo dhidi ya wanawake waasherati (1-14)

  • Shangilia pamoja na mke wako (15-23)

5  Mwanangu, sikiliza hekima yangu. Sikiliza kwa makini* utambuzi wangu,+   Ili uweze kuulinda uwezo wako wa kufikiriNa kuulinda ujuzi kwa midomo yako.+   Kwa maana midomo ya mwanamke aliyepotoka* inadondoka kama sega la asali,+Na kinywa chake ni laini kuliko mafuta.+   Lakini mwishowe ni mchungu kama pakanga+Na mwenye makali kama upanga unaokata kwa pande zote mbili.+   Miguu yake hushuka kwenye kifo. Hatua zake huongoza moja kwa moja Kaburini.*   Hakazii fikira kijia cha uzima. Huyumbayumba katika njia yake, lakini hajui inakoelekea.   Sasa, wanangu, nisikilizeniNanyi msiache ninayosema.   Kaeni mbali naye;Msiukaribie mlango wa nyumba yake,+   Ili msiwape wengine heshima yenu+Wala kuvuna miaka ya ukatili;+ 10  Ili wageni wasimalize mali* zenu+Na vitu mlivyopata kwa jasho viende katika nyumba ya mgeni. 11  La sivyo, mtalia kwa uchungu mwishoni mwa maisha yenuNyama na mwili wenu vitakapodhoofika+ 12  Nanyi mseme: “Jinsi nilivyochukia nidhamu! Jinsi moyo wangu ulivyodharau karipio! 13  Sikusikiliza sauti ya wakufunzi wanguWala kuwasikiliza kwa makini walimu wangu. 14  Nimefika ukingoni mwa maangamizi kamiliKatikati ya kutaniko lote.”*+ 15  Kunywa maji ya tangi lako mwenyeweNa maji yanayotiririka* kutoka katika kisima chako mwenyewe.+ 16  Je, chemchemi zako zitawanywe nje,Na vijito vyako vya maji katika viwanja vya jiji?+ 17  Na yawe yako peke yako,Wala si ya wageni pamoja nawe.+ 18  Chemchemi yako na ibarikiwe,*Na ushangilie pamoja na mke wa ujana wako,+ 19  Paa jike anayependeza, mbuzi wa mlimani* anayevutia.+ Matiti yake na yakuridhishe* nyakati zote. Upendo wake na ukusisimue daima.+ 20  Basi mwanangu, kwa nini usisimuliwe na mwanamke aliyepotoka*Au kukikumbatia kifua cha mwanamke mwasherati?*+ 21  Kwa maana njia za mwanadamu ziko mbele ya macho ya Yehova;Yeye huvichunguza vijia vyake vyote.+ 22  Mwovu hunaswa na makosa yake mwenyewe,Naye atashikwa na kamba za dhambi yake mwenyewe.+ 23  Atakufa kwa sababu ya utovu wa nidhamuNa kupotea njia kwa sababu ya upumbavu wake uliopita kiasi.

Maelezo ya Chini

Tnn., “Utegee sikio.”
Tnn., “mgeni.” Angalia Met 2:16.
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Au “nguvu.”
Tnn., “Katikati ya kusanyiko na kutaniko.”
Au “baridi.”
Au “Chanzo chako cha maji na kibarikiwe.”
Au “mbuzi mwitu.”
Au “yakuleweshe.”
Tnn., “mgeni.” Angalia Met 2:16.
Tnn., “mgeni.” Angalia Met 2:16.