Methali 7:1-27

  • Zishike amri za Mungu uishi (1-5)

  • Kijana mjinga atongozwa (6-27)

    • “Kama ng’ombe dume anayeenda machinjioni” (22)

7  Mwanangu, shika maneno yangu,Na uzihifadhi amri zangu kama hazina.+   Shika amri zangu uishi;+Linda mafundisho* yangu kama mboni ya jicho lako.   Zifunge juu ya vidole vyako;Ziandike kwenye kibao cha moyo wako.+   Iambie hekima, “Wewe ni dada yangu,” Na uuite uelewaji “mtu wangu wa ukoo,”   Ili vikulinde dhidi ya mwanamke aliyepotoka,*+Dhidi ya mwanamke mwasherati* na maneno yake laini.*+   Kutoka kwenye dirisha la nyumba yangu,Nilitazama chini kupitia viunzi vya dirisha langu,   Na nilipokuwa nikiwachunguza wajinga,*Nilitambua miongoni mwa vijana, kijana fulani mwanamume asiye na busara.*+   Alipita barabarani karibu na njia panda anapoishi mwanamke huyo,Naye akashika njia inayoelekea nyumbani kwa mwanamke huyo   Jioni wakati wa gizagiza,+Usiku na giza linapoingia. 10  Kisha nikamwona mwanamke akija kukutana naye,Akiwa amevaa kama* kahaba,+ mwenye moyo mjanja. 11  Mwanamke mwenye kelele na mkaidi.+ Hakai* kamwe nyumbani mwake. 12  Mara yuko nje, mara yuko katika viwanja vya jiji,Ananyemelea karibu na kila njia panda.+ 13  Kisha anamkamata kwa nguvu kijana huyo na kumpiga busu;Bila aibu, mwanamke huyo anamwambia: 14  “Nililazimika kutoa dhabihu za ushirika.+ Leo nilitimiza nadhiri zangu. 15  Ndiyo sababu nimekuja kukupokea,Kukutafuta, nami nimekupata! 16  Nimetandika matandiko bora kitandani mwangu,Kitani cha Misri chenye rangi mbalimbali.+ 17  Nimenyunyiza manemane, udi, na mdalasini kitandani mwangu.+ 18  Njoo, tunywe na kushiba upendo mpaka asubuhi;Na tujifurahishe kwa mahaba, 19  Kwa maana mume wangu hayuko nyumbani;Amesafiri mbali. 20  Alibeba mfuko wa pesa,Naye hatarudi mpaka siku ya mwezi mpevu.” 21  Anampotosha kwa ushawishi mkubwa.+ Anamtongoza kwa maneno laini. 22  Ghafla kijana huyo anamfuata, kama ng’ombe dume anayeenda machinjioni,Kama mjinga anayeenda kuadhibiwa katika mikatale,*+ 23  Mpaka mshale unapochoma ini lake;Kama ndege anayekimbia kuingia mtegoni, hajui kwamba hilo litamgharimu uhai wake.*+ 24  Na sasa, wanangu, nisikilizeni;Sikilizeni kwa makini maneno ninayosema. 25  Msiruhusu moyo wenu ugeuke na kufuata njia zake. Msipotee njia na kufuata vijia vyake,+ 26  Kwa maana amewaangamiza wengi,+Na wale aliowaua ni wengi sana.+ 27  Nyumba yake huongoza Kaburini;*Hushuka chini kwenye vyumba vya ndani vya kifo.

Maelezo ya Chini

Au “sheria.”
Tnn., “mgeni.” Angalia Met 2:16.
Tnn., “mgeni.” Angalia Met 2:16.
Au “yenye ushawishi.”
Au “wasio na uzoefu.”
Tnn., “aliyepungukiwa moyoni.”
Au “Akiwa na mavazi ya.”
Tnn., “Miguu yake haikai.”
Au “pingu.”
Au “nafsi yake.”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.