Methali 8:1-36

  • Hekima yaongea kama mtu (1-36)

    • ‘Mimi ni mwanzo kabisa wa kazi za Mungu’ (22)

    • ‘Nilikuwa kando ya Mungu nikiwa mfanyakazi stadi’ (30)

    • “Niliwapenda sana wanadamu” (31)

8  Je, hekima haipazi sauti? Je, utambuzi hauinui sauti yake?+   Kwenye sehemu zilizoinuka+ pembeni mwa barabara,Husimama kwenye makutano ya barabara.   Karibu na malango yanayoelekea jijini,Kwenye njia zinazoelekea milangoni,Huendelea kulia kwa sauti kubwa:+   “Ninawaita, enyi watu, ninawaita;Ninampazia sauti kila mtu.*   Enyi wajinga, jifunzeni werevu;+Enyi wapumbavu, jipatieni moyo wenye uelewaji.*   Sikilizeni, kwa maana ninayosema ni muhimu,Midomo yangu husema yaliyo sawa;   Kwa maana kinywa changu husema ukweli kwa sauti ya chini,Na midomo yangu huchukia jambo ovu.   Maneno yote ya kinywa changu ni ya uadilifu. Hakuna neno hata moja lililopinda wala kupotoka.   Yote yako wazi kabisa kwa mtu mwenye utambuziNayo ni sawa kwa wale ambao wamepata ujuzi. 10  Chukueni nidhamu yangu badala ya fedha,Na ujuzi badala ya dhahabu bora zaidi,+ 11  Kwa maana hekima ni bora kuliko marijani;*Vitu vingine vyote vinavyotamanika haviwezi kulinganishwa nayo. 12  Mimi, hekima, ninakaa pamoja na werevu;Nimepata ujuzi na uwezo wa kufikiri.+ 13  Kumwogopa Yehova humaanisha kuchukia uovu.+ Ninachukia kujikweza na kiburi+ na njia ya uovu na maneno mapotovu.+ 14  Nina ushauri mzuri na hekima inayotumika;+Uelewaji+ na nguvu+ ni vyangu. 15  Kwa msaada wangu wafalme huendelea kutawala,Na maofisa wakuu hutunga sheria za uadilifu.+ 16  Kwa msaada wangu wakuu huendelea kutawala,Na viongozi huhukumu kwa uadilifu. 17  Ninawapenda wale wanaonipenda,Na wale wanaonitafuta watanipata.+ 18  Nina utajiri na utukufu,Mali inayodumu* na uadilifu. 19  Tunda langu ni bora kuliko dhahabu, hata kuliko dhahabu safi,Na mazao yangu ni bora kuliko fedha bora kabisa.+ 20  Mimi hutembea katika kijia cha uadilifu,Katikati ya vijia vya haki; 21  Mimi huwapa urithi mwingi wale wanaonipenda,Nami huyajaza maghala yao. 22  Yehova aliniumba mwanzoni mwa njia yake,+Mwanzo kabisa wa kazi zake za zamani za kale.+ 23  Niliimarishwa tangu nyakati za kale,*+Tangu mwanzoni, nyakati za mapema kabla ya dunia kuwepo.+ 24  Wakati ambapo hakukuwa na vilindi vya maji,+ nilizaliwa,*Wakati ambapo hakukuwa na chemchemi zilizofurika maji. 25  Kabla milima haijawekwa mahali pake,Kabla ya vilima, nilizaliwa, 26  Wakati ambapo hakuwa ameiumba dunia na mashamba yakeWala mabonge ya kwanza ya udongo. 27  Alipozitayarisha mbingu,+ nilikuwepo;Alipouweka upeo* juu ya maji,+ 28  Alipoyafanya imara mawingu yaliyo juu,Alipojenga msingi wa chemchemi za vilindini, 29  Alipoiwekea bahari sheriaKwamba maji yake yasipite agizo lake,+Alipoiweka* misingi ya dunia, 30  Wakati huo nilikuwa kando yake nikiwa mfanyakazi stadi.+ Mimi ndiye aliyenipenda sana+ siku baada ya siku;Nilishangilia mbele zake wakati wote;+ 31  Nilishangilia dunia yake inayokaliwa,Nami niliwapenda sana wanadamu. 32  Na sasa, wanangu, nisikilizeni;Naam, wenye furaha ni wale wanaoshika njia zangu. 33  Sikilizeni nidhamu+ muwe na hekima,Msiipuuze kamwe. 34  Mwenye furaha ni mtu anayenisikilizaKwa kuja mapema* milangoni pangu siku baada ya siku,Kwa kusubiri karibu na miimo ya milango yangu; 35  Kwa maana anayenipata mimi atapata uzima,+Naye hupata kibali kutoka kwa Yehova. 36  Lakini anayenipuuza anajidhuru mwenyewe,*Na wale wanaonichukia wanapenda kifo.”+

Maelezo ya Chini

Au “kila mwanadamu.”
Tnn., “eleweni moyo.”
Angalia Kamusi.
Au “Kanuni zilizorithiwa.”
Au “zamani za kale.”
Au “nilizaliwa kana kwamba kwa uchungu wa kuzaa.”
Tnn., “Alipopiga duara.”
Au “Alipotunga sheria kuhusu.”
Au “Kwa kukesha.”
Au “anaidhuru nafsi yake.”