Methali 9:1-18

  • Hekima ya kweli inatoa mwaliko (1-12)

    • “Nitafanya siku zako ziwe nyingi” (11)

  • Mwanamke mpumbavu awaalika watu (13-18)

    • “Maji yaliyoibwa ni matamu” (17)

9  Hekima ya kweli imejenga nyumba yake;Imechonga nguzo zake saba.   Imetayarisha kabisa nyama yake;*Imechanganya divai yake;Imepanga pia meza yake.   Imewatuma vijakazi wakeIli waite kwa sauti kutoka vileleni juu ya jiji:+   “Yeyote ambaye ni mjinga, na aje humu.” Humwambia yule asiye na busara:*   “Njoo, ule mkate wanguNa unywe divai niliyochanganya.   Acha ujinga wako* uishi;+Tembea moja kwa moja katika njia ya uelewaji.”+   Anayemrekebisha mtu mwenye dhihaka hualika aibu,+Na yeyote anayemkaripia mtu mwovu ataumia.   Usimkaripie mtu mwenye dhihaka, kwa maana atakuchukia.+ Mkaripie mwenye hekima, naye atakupenda.+   Mfundishe mwenye hekima, naye atazidi kuwa na hekima.+ Mfundishe mwadilifu, naye atazidi kuelimika. 10  Kumwogopa Yehova ndio mwanzo wa hekima,+Na kumjua Aliye Mtakatifu Zaidi+ ni uelewaji. 11  Kwa maana nitafanya siku zako ziwe nyingi,+Na miaka ya maisha yako itaongezwa. 12  Ukipata hekima, unapata hekima kwa faida yako mwenyewe,Lakini ukiwa mwenye dhihaka, utaibeba dhihaka hiyo peke yako. 13  Mwanamke mpumbavu ana kelele.+ Yeye ni mjinga na hajui chochote. 14  Huketi kwenye mlango wa nyumba yakeKwenye kiti sehemu zilizoinuka jijini,+ 15  Akiwaita kwa sauti wale wanaopita karibu naye,Waendao moja kwa moja kwenye njia yao: 16  “Yeyote ambaye ni mjinga, aje hapa.” Huwaambia wale wasio na busara:*+ 17  “Maji yaliyoibwa ni matamu,Na chakula kinacholiwa sirini kinapendeza.”+ 18  Lakini hawajui kwamba wale waliokufa ambao hawana uwezo wako hapo,Na kwamba wageni wake wamo katika vina vya Kaburi.*+

Maelezo ya Chini

Tnn., “Amechinja nyama yake.”
Tnn., “aliyepungukiwa moyoni.”
Au “Waache wajinga.”
Tnn., “waliopungukiwa moyoni.”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.