Mhubiri 10:1-20

  • Upumbavu kidogo huharibu hekima (1)

  • Hatari za upumbavu (2-11)

  • Madhara ya kuwa mjinga (12-15)

  • Upumbavu miongoni mwa watawala (16-20)

    • Huenda ndege akarudia maneno uliyosema (20)

10  Kama nzi waliokufa wanavyofanya mafuta ya mtengenezaji wa marashi yanuke na kutoa povu, ndivyo ujinga kidogo unavyozidi hekima na utukufu.+  Moyo wa mwenye hekima humwongoza katika njia inayofaa,* lakini moyo wa mpumbavu humwongoza katika njia isiyofaa.*+  Katika njia yoyote ambayo mjinga anatembea, hana busara,*+ naye huacha kila mtu ajue kwamba yeye ni mjinga.+  Hasira* ya mtawala ikiwaka dhidi yako, usiondoke mahali pako,+ kwa maana utulivu huzuia dhambi kubwa.+  Kuna jambo linalohuzunisha ambalo nimeona chini ya jua, aina ya kosa linalofanywa na watawala:+  Ujinga huwekwa katika vyeo vingi vya juu, lakini matajiri* hubaki kwenye vyeo vya chini.  Nimeona watumishi wakiwa wamepanda farasi lakini wakuu wakitembea kwa miguu kama watumishi tu.+  Anayechimba shimo huenda akaanguka ndani yake;+ na anayebomoa ukuta wa mawe huenda akaumwa na nyoka.  Anayechimbua mawe huenda yakamuumiza, na yule anayepasua magogo huenda yakamuumiza.* 10  Ikiwa kifaa cha chuma hakina makali na mtu hakinoi, atahitaji kutumia nguvu nyingi. Lakini hekima husaidia kuleta mafanikio. 11  Nyoka akiuma kabla hajachezeshwa, mtu anayemchezesha kwa ustadi* hapati faida yoyote. 12  Maneno yanayotoka kwenye kinywa cha mwenye hekima huleta kibali,+ lakini midomo ya mpumbavu ndiyo inayomwangamiza.+ 13  Maneno ya kwanza yanayotoka katika kinywa chake ni ujinga,+ na maneno yake ya mwisho ni wazimu unaoleta msiba. 14  Lakini mjinga huendelea kuongea.+ Mwanadamu hajui yatakayotukia; ni nani anayeweza kumwambia yatakayotukia baada yake?+ 15  Kazi ngumu ya mpumbavu humchosha kabisa, kwa sababu hata hajui jinsi atakavyofika jijini. 16  Ole kwa nchi ambayo mfalme wake ni mvulana+ na wakuu wake huanza karamu asubuhi! 17  Yenye furaha ni nchi ambayo mfalme wake ni mwana wa watu mashuhuri na wakuu wake hula wakati unaofaa ili wapate nguvu, si walewe!+ 18  Kwa sababu ya uvivu unaopita kiasi paa hubonyea, na kwa sababu ya mikono milegevu nyumba huvuja.+ 19  Mkate umekusudiwa* kuleta kicheko, na divai hufanya maisha yafurahishe;+ lakini pesa ni jawabu la mahitaji yote.+ 20  Usimtukane* mfalme hata katika mawazo yako,*+ na usiwatukane matajiri katika chumba chako cha kulala; kwa sababu huenda ndege* akapeleka habari zako,* au huenda kiumbe mwenye mabawa akarudia lililosemwa.

Maelezo ya Chini

Tnn., “uko kwenye mkono wake wa kulia.”
Tnn., “uko kwenye mkono wake wa kushoto.”
Tnn., “moyo wake umepungukiwa.”
Tnn., “Roho, Pumzi.”
Au “wanaostahili.”
Au labda, “anapaswa kujihadhari nayo.”
Tnn., “stadi wa ulimi.”
Au “Chakula kimekusudiwa.”
Au “Usimlaani.”
Au labda, “kitandani mwako.”
Tnn., “kiumbe anayeruka angani.”
Tnn., “sauti yako.”