Mhubiri 11:1-10

  • Furahia ujana wako kwa njia inayofaa (9, 10)

11  Tupa* mkate wako juu ya maji,+ kwa maana baada ya siku nyingi utaupata tena.+  Wagawie watu saba au hata wanane,+ kwa maana hujui ni msiba gani utakaotokea* duniani.  Mawingu yakijaa maji, mvua itanyesha duniani; na mti ukianguka kuelekea kusini au kaskazini, utabaki mahali ulipoanguka.  Anayeangalia upepo hatapanda mbegu, na anayetazama mawingu hatavuna.+  Kama usivyojua jinsi roho inavyofanya kazi ndani ya mifupa ya mtoto aliye tumboni mwa mama yake,+ vivyo hivyo hujui kazi ya Mungu wa kweli, anayefanya mambo yote.+  Panda mbegu zako asubuhi na usipumzishe mkono wako mpaka jioni;+ kwa maana hujui ni mbegu gani itakayofanikiwa, hii au ile, au ikiwa zote mbili zitafanikiwa.  Mwangaza ni mtamu, na ni vizuri macho yaone jua.  Kwa maana ikiwa mwanadamu ataishi miaka mingi, na aifurahie yote.+ Lakini anapaswa kukumbuka kwamba huenda siku za giza zikawa nyingi; yote yatakayokuja ni ubatili.+  Shangilia, ewe kijana, wakati ungali kijana, na moyo wako ushangilie siku za ujana wako. Fuata njia za moyo wako na uende mahali ambapo macho yako yanakuongoza; lakini ujue kwamba Mungu wa kweli atakuhukumu* kwa sababu ya mambo hayo yote.+ 10  Kwa hiyo ondoa mahangaiko moyoni mwako, na ujiepushe na mambo yanayodhuru mwili wako, kwa maana ujana na upeo wa maisha ni ubatili.+

Maelezo ya Chini

Au “Sambaza.”
Au “janga gani litakalotokea.”
Au “atakufanya uwajibike.”