Mhubiri 2:1-26

  • Maelezo kuhusu mambo aliyotimiza Sulemani (1-11)

  • Hekima ya wanadamu haina faida kubwa (12-16)

  • Ubatili wa kazi ya jasho (17-23)

  • Ule, unywe, na kufurahia kazi (24-26)

2  Kisha nikasema moyoni mwangu: “Haya, acha nijaribu starehe,* nione ni jambo gani jema litakalokuja.” Lakini tazama! hilo pia lilikuwa ubatili.   Nilisema hivi kuhusu kicheko: “Ni wazimu!” Na kuhusu starehe,* “Ina faida gani?”  Nilijaribu kuufurahisha moyo wangu kwa divai,+ huku nikiendelea kuwa na hekima yangu; hata nilikumbatia ujinga ili nione jambo bora ambalo wanadamu wanapaswa kufanya katika siku chache wanazoishi chini ya mbingu.  Nilianza kufanya mambo makubwa.+ Nikajijengea nyumba;+ Nikajipandia mashamba ya mizabibu.+  Nikajitengenezea mashamba na bustani, na humo nikapanda miti ya matunda ya kila aina.  Nikajichimbia mabwawa ya maji, ili kumwagilia maji msitu wenye miti iliyokuwa ikisitawi.  Nikapata watumishi wa kiume na wa kike,+ na watumishi wengine walizaliwa nyumbani mwangu.* Pia, nilipata mifugo mingi—ng’ombe na kondoo na mbuzi+—kuliko mtu yeyote aliyenitangulia Yerusalemu.  Nikajikusanyia fedha na dhahabu,+ hazina za* wafalme na za mikoa.+ Nikajikusanyia waimbaji wa kiume na wa kike, na pia chanzo cha raha tele kwa wanaume—mwanamke, naam, wanawake wengi.  Basi nikawa mkuu, nikamzidi mtu yeyote aliyenitangulia Yerusalemu.+ Nami nikaendelea kuwa na hekima yangu. 10  Sikujinyima chochote nilichotamani.*+ Sikuunyima moyo wangu raha* yoyote ile, kwa maana moyo wangu ulishangilia kwa sababu ya kazi yangu yote ngumu, na hiyo ndiyo iliyokuwa thawabu yangu* kwa sababu ya kazi yangu yote ngumu.+ 11  Lakini nilipofikiria kazi zote nilizofanya kwa mikono yangu mwenyewe na kazi yangu yote ngumu niliyofanya kwa jasho ili kuitimiza,+ niliona kwamba kila kitu kilikuwa ubatili, kukimbiza upepo;+ hakukuwa na kitu chochote chenye thamani ya kweli* chini ya jua.+ 12  Basi nikaanza kuchunguza hekima na wazimu na ujinga.+ (Kwa maana mtu anayekuja baada ya mfalme anaweza kufanya nini? Anaweza kufanya tu jambo ambalo tayari limefanywa.) 13  Nami nikaona kwamba hekima ina faida kuliko ujinga,+ kama tu nuru ilivyo na faida kuliko giza. 14  Mtu mwenye hekima ana macho kichwani mwake;*+ lakini mpumbavu anatembea gizani.+ Pia nimegundua kwamba wote wana mwisho uleule. *+ 15  Kisha nikasema moyoni mwangu: “Kinachompata mpumbavu ndicho kitakachonipata mimi pia.”+ Sasa, basi, nilipata faida gani kwa kuwa na hekima kupita kiasi? Basi nikasema moyoni mwangu: “Hili pia ni ubatili.” 16  Kwa maana hakuna atakayekumbukwa daima, iwe ni mwenye hekima au mpumbavu.+ Siku zijazo, kila mtu atasahauliwa. Na mwenye hekima atakufa jinsi gani? Pamoja na mpumbavu.+ 17  Basi nikachukia maisha,+ kwa sababu kila jambo linalofanywa chini ya jua lilionekana kwangu kuwa lenye kuhuzunisha, kwa sababu kila jambo lilikuwa ubatili,+ kukimbiza upepo.+ 18  Nikachukia vitu vyote nilivyokuwa nimefanya kazi ngumu chini ya jua ili kuvipata,+ kwa sababu ni lazima nimwachie mtu atakayekuja baada yangu.+ 19  Na ni nani anayejua ikiwa atakuwa mwenye hekima au mjinga?+ Lakini bado atamiliki vitu vyote nilivyotafuta kwa jitihada nyingi na hekima chini ya jua. Hilo pia ni ubatili. 20  Basi nikaanza kukata tamaa moyoni mwangu kwa sababu ya kazi yangu yote ngumu niliyofanya kwa jasho chini ya jua. 21  Kwa maana mtu anaweza kufanya kazi kwa bidii, akiongozwa na hekima na ujuzi na ustadi, lakini ni lazima amwachie fungu lake mtu ambaye hakulifanyia kazi.*+ Hili pia ni ubatili na ni msiba mkubwa.* 22  Kwa kweli mtu hupata faida gani kutokana na kazi yake yote ngumu na tamaa inayomchochea* kufanya kazi kwa bidii chini ya jua?+ 23  Kwa maana siku zake zote, kazi yake humletea maumivu na kumkatisha tamaa,+ na hata usiku moyo wake haupumziki.+ Hili pia ni ubatili. 24  Hakuna jambo bora analoweza kufanya mtu kuliko kula na kunywa na kufurahia* kazi yake ngumu.+ Hili pia nimegundua kwamba linatoka mkononi mwa Mungu wa kweli,+ 25  kwa maana ni nani anayekula na ni nani anayekunywa vizuri kuliko mimi?+ 26  Yeye humpa mtu anayempendeza hekima na ujuzi na shangwe,+ lakini humpa mtenda dhambi kazi ya kukusanya na kurundika tu, ili ampe yule anayempendeza Mungu wa kweli.+ Hili pia ni ubatili, kukimbiza upepo.

Maelezo ya Chini

Au “kushangilia.”
Yaani, kushangilia.
Tnn., “na nilikuwa na wana wa nyumba.”
Au “mali ambazo kwa kawaida ni za.”
Au “na hilo ndilo lililokuwa fungu langu.”
Au “shangwe.”
Tnn., “ambacho macho yangu yaliomba.”
Au “manufaa.”
Au “hatima ileile.”
Au “anafungua macho yake.”
Au “ampe vitu vyote mtu ambaye hakuvifanyia kazi.”
Au “janga kubwa.”
Tnn., “jitihada za moyo wake za.”
Au “kuifanya nafsi yake ione mema kwa sababu ya.”