Mhubiri 3:1-22

  • Kila jambo lina wakati wake (1-8)

  • Kufurahia maisha ni zawadi kutoka kwa Mungu (9-15)

    • Umilele umo ndani ya mioyo ya wanadamu (11)

  • Mungu huwahukumu wote kwa haki (16, 17)

  • Wanadamu na wanyama wote hufa (18-22)

    • Wote watarudi mavumbini (20)

3  Kuna wakati uliowekwa wa kila jambo,Wakati wa kila shughuli chini ya mbingu:   Wakati wa kuzaliwa na wakati wa kufa;Wakati wa kupanda na wakati wa kung’oa kilichopandwa;   Wakati wa kuua na wakati wa kuponya;Wakati wa kubomoa na wakati wa kujenga;   Wakati wa kulia na wakati wa kucheka;Wakati wa kuomboleza kwa sauti na wakati wa kucheza dansi;*   Wakati wa kutupa mawe na wakati wa kukusanya mawe;Wakati wa kukumbatia na wakati wa kuacha kukumbatia;   Wakati wa kutafuta na wakati wa kuacha kutafuta kilichopotea;Wakati wa kuhifadhi na wakati wa kutupa;   Wakati wa kurarua+ na wakati wa kushona,Wakati wa kunyamaza+ na wakati wa kuongea;+   Wakati wa kupenda na wakati wa kuchukia;+Wakati wa vita na wakati wa amani.  Mfanyakazi hupata faida gani kutokana na jitihada zake zote?+ 10  Nimeona kazi ambayo Mungu amewapa wanadamu wajishughulishe nayo. 11  Amefanya kila kitu kipendeze* kwa wakati wake.+ Hata ameweka umilele katika moyo wao; lakini bado wanadamu hawatajua kamwe kazi ambayo Mungu wa kweli amefanya tangu mwanzo mpaka mwisho. 12  Nimefikia mkataa kwamba hakuna jambo bora wanaloweza kufanya kuliko kushangilia na kufanya mema maishani mwao,+ 13  na kwamba kila mtu anapaswa kula na kunywa na kufurahia kazi yake yote ngumu. Ni zawadi kutoka kwa Mungu.+ 14  Sasa nimejua kwamba kazi zote za Mungu wa kweli zitadumu milele. Hakuna chochote kinachoweza kuongezwa wala chochote kinachoweza kupunguzwa kwenye kazi zake. Mungu wa kweli amezifanya ziwe hivyo, ili watu wamwogope.+ 15  Jambo lolote linalotukia limewahi kutukia, na litakalokuja limewahi kuwepo;+ lakini Mungu wa kweli hutafuta kilichofuatiwa.* 16  Pia nimeona jambo hili chini ya jua: Badala ya haki kulikuwa na uovu, na badala ya uadilifu kulikuwa na uovu.+ 17  Basi nikasema moyoni mwangu: “Mungu wa kweli atawahukumu waadilifu na waovu,+ kwa maana kuna wakati kwa ajili ya kila kazi na kila tendo.” 18  Pia nikasema moyoni mwangu kwamba Mungu wa kweli atawajaribu wanadamu na kuwaonyesha kwamba wao ni kama wanyama, 19  kwa maana kuna mwisho wa* wanadamu na mwisho wa wanyama; wote wana mwisho uleule.+ Anavyokufa huyu, ndivyo anavyokufa huyu; na wote wana roho ileile.+ Kwa hiyo mwanadamu si bora kuliko wanyama, kwa maana kila kitu ni ubatili. 20  Wote wanaenda mahali palepale.+ Wote wanatoka mavumbini,+ na wote wanarudi mavumbini.+ 21  Kwa kweli ni nani anayejua ikiwa roho ya wanadamu hupanda kwenda juu, na ikiwa roho ya wanyama hushuka chini ardhini?+ 22  Nami nikaona kwamba hakuna jambo bora kwa mwanadamu kuliko kufurahia kazi yake,+ kwa sababu hiyo ndiyo zawadi yake;* kwa maana ni nani anayeweza kumwezesha aone yatakayotukia baada ya kifo chake?+

Maelezo ya Chini

Tnn., “kuruka; kurukaruka.”
Au “kiwe na mpangilio mzuri; kifae.”
Au labda, “kilichopitilia mbali.”
Au “hatima ya.”
Au “hilo ndilo fungu lake.”