Mhubiri 4:1-16

  • Ukandamizaji ni mbaya kuliko kifo (1-3)

  • Maoni yanayofaa kuhusu kazi (4-6)

  • Faida ya rafiki (7-12)

    • Wawili ni bora (9)

  • Maisha ya mtawala yanaweza kuwa ya ubatili (13-16)

4  Tena, nikakazia uangalifu matendo yote ya ukandamizaji yanayofanywa chini ya jua. Nikaona machozi ya wanaokandamizwa, na hakukuwa na mtu yeyote wa kuwafariji.+ Na wale waliowakandamiza walikuwa na nguvu, lakini waliokandamizwa hawakuwa na mtu yeyote wa kuwafariji.  Nami nikawapongeza wafu ambao tayari walikuwa wamekufa badala ya walio hai ambao bado walikuwa hai.+  Na yule ambaye hajazaliwa ni afadhali kuliko hao wawili,+ kwa kuwa hajaona mambo yenye kuhuzunisha yanayofanywa chini ya jua.+  Nami nimeona jinsi ambavyo ushindani kati ya watu unavyowafanya wajitahidi sana* na kufanya kazi kwa ustadi;+ hili pia ni ubatili, kukimbiza upepo.  Mpumbavu hukunja mikono yake huku mwili wake ukiendelea kudhoofika.*+  Ni afadhali konzi moja ya pumziko kuliko konzi mbili za kazi ngumu na kukimbiza upepo.+  Nilikazia uangalifu mfano mwingine wa ubatili chini ya jua:  Kuna mtu aliye peke yake, asiye na rafiki yeyote; hana mwana wala ndugu, lakini kazi yake yote ngumu haina mwisho. Macho yake hayatosheki kamwe na utajiri.+ Lakini je, yeye hujiuliza, ‘Ninafanya kazi kwa bidii na kujinyima* vitu vyema kwa ajili ya nani’?+ Hili pia ni ubatili na ni kazi inayosikitisha.+  Wawili ni afadhali kuliko mmoja+ kwa sababu wanapata thawabu njema* kwa kazi yao ngumu. 10  Kwa maana mmoja wao akianguka, mwenzake anaweza kumwinua. Lakini itakuwaje kwa yule atakayeanguka naye hana mtu wa kumwinua? 11  Tena, wawili wakilala pamoja, watapata joto, lakini mtu mmoja tu atapataje joto? 12  Na mtu anaweza kumzidi nguvu aliye peke yake, lakini wawili walio pamoja wanaweza kukabiliana naye. Na kamba ya nyuzi tatu haikatiki upesi.* 13  Ni afadhali mtoto maskini lakini mwenye hekima kuliko mfalme mzee lakini mpumbavu,+ ambaye hana tena ufahamu wa kutosha wa kutii onyo.+ 14  Kwa maana alitoka* gerezani ili awe mfalme,+ ingawa alizaliwa maskini katika utawala wa mfalme huyo.+ 15  Niliwafikiria wote walio hai wanaotembeatembea chini ya jua, na pia hali ya yule mtawala kijana anayechukua mahali pa yule mfalme. 16  Ingawa idadi ya wafuasi wake wote haina mwisho, wale watakaokuja baadaye hawatafurahishwa naye.+ Hili pia ni ubatili, kukimbiza upepo.

Maelezo ya Chini

Au “wajitahidi kufanya kazi ya jasho.”
Tnn., “naye anakula mwili wake mwenyewe.”
Au “kuinyima nafsi yangu.”
Au “faida kubwa zaidi.”
Au “kwa urahisi.”
Labda ni yule mtoto mwenye hekima.