Mhubiri 5:1-20

  • Mkaribie Mungu kwa woga unaofaa (1-7)

  • Walio chini hutazamwa na walio juu zaidi (8, 9)

  • Ubatili wa utajiri (10-20)

    • Wanaopenda pesa hawatosheki kamwe (10)

    • Usingizi wa mfanyakazi ni mtamu (12)

5  Uwe mwangalifu* wakati wowote unapoenda katika nyumba ya Mungu wa kweli;+ ni afadhali ukaribie ili kusikiliza+ badala ya kutoa dhabihu kama wanavyofanya wapumbavu,+ kwa maana hawajui kwamba jambo wanalofanya ni baya.  Usifungue kinywa chako haraka, wala usiruhusu moyo wako uzungumze bila kufikiri mbele za Mungu wa kweli,+ kwa maana Mungu wa kweli yuko mbinguni lakini wewe uko duniani. Ndiyo sababu maneno yako yanapaswa kuwa machache.+  Kwa maana ndoto huja kwa sababu ya shughuli nyingi sana,*+ na mpumbavu huropoka kwa sababu ya kuwa na maneno mengi sana.+  Wakati wowote unapoweka nadhiri kwa Mungu,+ usikawie kuitimiza, kwa maana hapendezwi na wapumbavu.+ Unapoweka nadhiri, itimize.+  Ni afadhali usiweke nadhiri kuliko kuweka nadhiri na kukosa kuitimiza.+  Usiruhusu kinywa chako kikufanye* utende dhambi,+ wala usiseme mbele ya malaika* kwamba nilikosea.+ Kwa nini umkasirishe Mungu wa kweli kwa yale unayosema hivi kwamba alazimike kuiharibu kazi ya mikono yako?+  Kwa maana kama vile shughuli nyingi zinavyomfanya mtu aote ndoto,+ vivyo hivyo, maneno mengi huongoza kwenye ubatili. Lakini mwogope Mungu wa kweli.+  Ukiona maskini wakikandamizwa kwa njia yoyote ile na haki na uadilifu zikikiukwa katika wilaya yenu, usishangazwe na jambo hilo.+ Kwa maana ofisa huyo mkuu anatazamwa na yule aliye juu zaidi yake, na kuna wengine walio juu zaidi yao.  Pia, faida ya nchi hugawanywa miongoni mwao wote; hata mfalme huhudumiwa kutokana na shamba hilo.+ 10  Anayependa fedha hatatosheka na fedha, wala anayependa mali hatatosheka na mapato.+ Hili pia ni ubatili.+ 11  Vitu vizuri vinapoongezeka, walaji huongezeka.+ Na mwenye vitu hivyo hupata faida gani, ila kuviangalia tu kwa macho yake?+ 12  Usingizi wa mtumishi ni mtamu, iwe anakula kidogo au kingi, lakini wingi alionao tajiri haumruhusu kulala usingizi. 13  Kuna msiba mkubwa ambao* nimeona chini ya jua: utajiri uliorundikwa na mtu na kumdhuru yeye mwenyewe. 14  Utajiri huo ulipotea kwa sababu ya mradi ambao haukufanikiwa,* na anapomzaa mwana, habaki na kitu chochote.+ 15  Kama mtu alivyotoka katika tumbo la mama yake akiwa uchi, ndivyo atakavyoenda, kama alivyokuja.+ Naye hawezi kwenda na chochote alichopata kutokana na kazi yake yote ngumu.+ 16  Huu pia ni msiba mkubwa:* Kama tu alivyokuja, ndivyo atakavyoenda; na mtu ambaye anafanya kazi kwa bidii daima kwa ajili ya upepo anapata faida gani?+ 17  Pia, yeye hula gizani kila siku, akiwa amekata tamaa kabisa na akiwa mgonjwa na akiwa amekasirika kabisa.+ 18  Hili ndilo jambo ambalo nimeona ni jema na linafaa: kwamba mtu anapaswa kula na kunywa na kufurahia kazi yote ngumu+ anayofanya kwa jasho chini ya jua katika siku chache za maisha alizopewa na Mungu wa kweli, kwa maana hiyo ndiyo thawabu yake.*+ 19  Pia, Mungu wa kweli anapompa mtu utajiri na mali+ pamoja na uwezo wa kufurahia vitu hivyo, anapaswa kuchukua thawabu yake* na kushangilia katika kazi yake ngumu. Hiyo ndiyo zawadi kutoka kwa Mungu.+ 20  Kwa maana hataona* kwa urahisi jinsi siku za maisha yake zinavyopita, kwa sababu Mungu wa kweli humshughulisha na shangwe ya moyo wake.+

Maelezo ya Chini

Au “Chunga hatua zako.”
Au “mahangaiko mengi sana.”
Tnn., “mwili wako ukufanye.”
Au “mjumbe.”
Au “janga kubwa ambalo.”
Tnn., “kazi ya msiba.”
Au “Hili pia ni janga kubwa.”
Au “hilo ndilo fungu lake.”
Au “fungu lake.”
Au “hatakumbuka.”