Mika 1:1-16

  • Hukumu dhidi ya Samaria na Yuda (1-16)

    • Matatizo yasababishwa na dhambi na uasi (5)

1  Neno la Yehova lililomjia Mika*+ wa Moreshethi, katika siku za utawala wa Yothamu,+ Ahazi,+ na Hezekia,+ wafalme wa Yuda,+ na ambalo alilipokea katika maono kuhusu Samaria na Yerusalemu:   “Sikieni, enyi mataifa yote! Sikiliza, Ee dunia na vitu vyote vinavyokujaza,Acha Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova awe shahidi dhidi yako+—Yehova kutoka katika hekalu lake takatifu.   Kwa maana tazama! Yehova anatoka mahali pake;Atashuka chini na kukanyaga sehemu za juu za dunia.   Milima itayeyuka chini yake,+Na mabonde yatagawanyika*Kama nta mbele ya moto,Kama maji yanayomwagwa kwenye mteremko mkali.   Hayo yote kwa sababu ya uasi wa Yakobo,Kwa sababu ya dhambi za nyumba ya Israeli.+ Uasi wa Yakobo ni nini? Je, si Samaria?+ Na mahali pa juu pa Yuda ni nini?+ Je, si Yerusalemu?   Nitafanya Samaria kuwa rundo la magofu la shambani,Mahali pa kupanda mizabibu;Nitayatupa* mawe yake chini bondeni,Nami nitaichimbua misingi yake.   Sanamu zake zote za kuchongwa zitavunjwa vipandevipande,+Na zawadi zote alizopewa kwa sababu ya ukahaba wake zitateketezwa motoni.*+ Nitaharibu kabisa sanamu zake zote. Kwa sababu alizikusanya kwa kutumia malipo ya ukahaba,Nazo zitakuwa tena malipo ya makahaba.”   Kwa sababu hiyo nitalia kwa sauti na kupiga mayowe;+Nitatembea bila viatu nikiwa uchi.+ Nitalia kwa sauti kama mbwamwitu wanavyolia,Na kuomboleza kama mbuni wanavyoomboleza.   Kwa sababu jeraha lake haliwezi kuponywa;+Limefika mpaka Yuda.+ Pigo limeenea mpaka kwenye lango la watu wangu, mpaka Yerusalemu.+ 10  “Msitangaze hilo kule Gathi;Msilie hata kidogo. Kule Beth-afra* mgaegae mavumbini. 11  Vukeni mkiwa uchi na wenye aibu, enyi wakaaji* wa Shafiri. Wakaaji wa Saanani hawajatoka nje. Kutakuwa na kilio kikubwa kule Beth-ezeli, nacho hakitawasaidia. 12  Kwa maana wakaaji wa Marothi wamengojea mema,Lakini mabaya yameshuka kutoka kwa Yehova mpaka kwenye lango la Yerusalemu. 13  Fungeni kundi la farasi kwenye gari la vita, enyi wakaaji wa Lakishi.+ Mlikuwa chanzo cha dhambi kwa binti ya Sayuni,Kwa maana maasi ya Israeli yalipatikana ndani yako.+ 14  Kwa hiyo mtampa Moresheth-gathi zawadi za kumuaga.* Nyumba za Akzibu+ zilikuwa kitu cha udanganyifu kwa wafalme wa Israeli. 15  Bado nitawaletea mshindi,*+ enyi wakaaji wa Maresha.+ Utukufu wa Israeli utafika mpaka Adulamu.+ 16  Nyoeni upara na kuzikata kabisa nywele zenu kwa ajili ya watoto wenu wapendwa. Nyoeni upara kama wa tai,Kwa maana wamechukuliwa kutoka kwenu na kupelekwa uhamishoni.”+

Maelezo ya Chini

Ufupisho wa jina Mikaeli au Mikaya linalomaanisha “Ni Nani Aliye Kama Yehova?”
Au “nchi tambarare za chini zitagawanyika.”
Tnn., “Nitayamwaga.”
Au “malipo yote ya ukahaba wake yatateketezwa motoni.”
Au “Katika nyumba ya Afra.”
Tnn., “ewe mkaaji wa kike.”
Au “za kwaheri.”
Au “mnyang’anyi.”