Mika 2:1-13

  • Ole kwa wakandamizaji! (1-11)

  • Waisraeli wakusanywa na kuunganishwa (12, 13)

    • Nchi itakuwa na kelele za watu (12)

2  “Ole wao wanaopanga njama yenye kudhuru,Wanaotunga maovu vitandani mwao! Kunapopambazuka wanayatekeleza,Kwa sababu wana uwezo wa kuyatekeleza.+   Wanatamani mashamba na kuyanyakua;+Pia nyumba, na kuzichukua;Wanamlaghai mtu na kuchukua nyumba yake,+Wanachukua urithi wa mtu.   Kwa hiyo Yehova anasema hivi: ‘Sasa basi nakusudia kuiletea familia hii msiba+ ambao hamtaweza kuuepuka.*+ Hamtatembea tena kwa kiburi,+ kwa sababu utakuwa wakati wa msiba.+   Siku hiyo watu watatunga methali kuwahusu,Nao watawaombolezea kwa uchungu.+ Watasema: “Tumeangamizwa kabisa!+ Alisababisha fungu la watu wangu lichukuliwe na wengine—Lo! Amenipokonya!+ Amemgawia yule asiye mwaminifu mashamba yetu.”   Kwa hiyo hamtakuwa na mtu wa kunyoosha kamba ya kupimia,Wa kuigawa ardhi katika kutaniko la Yehova.   Wanahubiri wakisema, “Acheni kuhubiri!” “Hawapaswi kuhubiri mambo haya;Hatutapatwa na aibu!”   Je, inasemwa, Ee nyumba ya Yakobo, kwamba“Roho ya Yehova imekosa subira? Je, haya ndiyo matendo yake?” Je, maneno yangu mwenyewe hayawanufaishi wale wanaotembea kwa unyoofu?   Lakini hivi karibuni watu wangu mwenyewe wameinuka kama adui. Mnalivua hadharani pambo la kifahari pamoja na* vaziKutoka kwa watu wanaopita bila wasiwasi, kama watu wanaorudi kutoka vitani.   Mnawafukuza wanawake wa watu wangu kutoka katika nyumba zao zenye kupendeza;Mnaondoa fahari yangu milele kutoka kwa watoto wao. 10  Inukeni mwende zenu, kwa sababu hapa si mahali pa kupumzika. Kwa sababu ya uchafu,+ kuna maangamizi, maangamizi makubwa.+ 11  Mtu akifuata upepo na udanganyifu na kusema uwongo huu: “Nitawahubiria kuhusu divai na pombe,” Basi atakuwa mhubiri anayewafaa kabisa watu hawa!+ 12  Kwa hakika nitawakusanya ninyi nyote, enyi watu wa Yakobo;Kwa kweli nitawakusanya pamoja wale wanaobaki wa Israeli.+ Kwa umoja nitawaweka kama kondoo zizini,Kama kundi la kondoo katika malisho yake;+Litakuwa na kelele za watu.’+ 13  Yule anayevunja lango na kutoka atawatangulia;Nao watavunja lango na kupitia langoni kwenda nje.+ Mfalme wao atapitia humo akiwatangulia,Huku Yehova akiwaongoza.”+

Maelezo ya Chini

Tnn., “hamtauondoa kwenye shingo zenu.”
Au labda, “kutoka kwenye.”