Mika 3:1-12

  • Viongozi na manabii washutumiwa (1-12)

    • Mika apata nguvu nyingi kwa sababu ya roho ya Yehova (8)

    • Makuhani wafundisha ili wapate pesa (11)

    • Yerusalemu litabaki marundo ya magofu (12)

3  Nilisema: “Sikieni, tafadhali, enyi viongozi wa YakoboNanyi makamanda wa nyumba ya Israeli.+ Je, hampaswi kujua jambo lililo la haki?   Lakini mnachukia mema+ na kupenda maovu;+Mnawachuna ngozi watu wangu na kuondoa nyama kutoka kwenye mifupa yao.+   Pia mnakula nyama ya watu wangu+Na kuwachuna ngozi,Mnapasua mifupa yao, na kuivunja vipandevipande,+Kama kitu kinachopikwa ndani ya chungu,* kama nyama ndani ya chungu cha kupikia.   Wakati huo watamlilia Yehova awasaidie,Lakini hatawajibu. Atauficha uso wake kutoka kwao wakati huo,+Kwa sababu ya matendo yao maovu.+   Yehova anasema hivi kuhusu manabii wanaowapotosha watu wake,+Wanaotangaza ‘Amani!’+ huku wakitafuna* kwa meno yao+Lakini wanaotangaza* vita dhidi ya yule asiyeweka kitu vinywani mwao:   ‘Mtakuwa na usiku;+ hakutakuwa na maono;+Mtakuwa na giza tu, hakutakuwa na uaguzi.* Jua litatua kwa manabii,Na mchana utageuka kuwa giza kwao.+   Watu wanaoona maono wataaibishwa,+Na wabashiri watakata tamaa. Wote watalazimika kufunika masharubu,*Kwa maana hakuna jibu kutoka kwa Mungu.’”   Lakini mimi, nimejazwa nguvu kwa roho ya Yehova,Nimejazwa haki na uwezo, Ili nimwambie Yakobo uasi wake na Israeli dhambi yake.   Sikieni jambo hili, tafadhali, enyi viongozi wa nyumba ya YakoboNanyi makamanda wa nyumba ya Israeli,+Mnaochukia haki na kupotosha mambo yote yaliyonyooka,+ 10  Mnaojenga Sayuni kwa umwagaji wa damu na Yerusalemu kwa ukosefu wa uadilifu.+ 11  Viongozi* wake huhukumu ili wapate rushwa,+Makuhani wake hufundisha ili wapate malipo,+Na manabii wake hufanya uaguzi* ili wapate pesa.*+ Na bado wanamwegemea Yehova,* wakisema: “Je, Yehova hayuko pamoja nasi?+ Hakuna msiba utakaotupata.”+ 12  Basi kwa sababu yenu,Sayuni litalimwa kama shamba,Yerusalemu litakuwa marundo ya magofu,+Na mlima wa Nyumba* utakuwa kama vilima msituni.*+

Maelezo ya Chini

Au “chungu cha kupikia chenye mdomo mpana.”
Au labda, “wanapokuwa na kitu cha kutafuna.”
Tnn., “wanaotakasa.”
Au “ubashiri.”
Au “watafumba vinywa vyao.”
Au “wanadai wanamwegemea Yehova.”
Au “fedha.”
Au “hubashiri.”
Tnn., “Vichwa.”
Au “mlima wa hekalu.”
Au “kilima chenye msitu.”