Mika 4:1-13

  • Mlima wa Yehova wainuliwa (1-5)

    • Panga zitakuwa majembe (3)

    • “Tutatembea katika jina la Yehova” (5)

  • Sayuni lajengwa upya na kuimarishwa (6-13)

4  Katika siku za mwisho,*Mlima wa nyumba ya Yehova+Utaimarishwa kabisa juu ya vilele vya milima,Nao utainuliwa juu ya vilima,Na mataifa yatamiminika kwenye mlima huo.+   Na mataifa mengi yataenda na kusema: “Njooni, twendeni juu kwenye mlima wa YehovaNa kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo.+ Naye atatufundisha njia zake,Nasi tutatembea katika vijia vyake.” Kwa maana sheria itatoka* Sayuni,Na neno la Yehova litatoka Yerusalemu.   Atatekeleza hukumu miongoni mwa mataifa mengi+Na kunyoosha* mambo kuhusiana na mataifa yenye nguvu yaliyo mbali. Watafua panga zao ziwe majembe ya plauNa mikuki yao iwe miundu.+ Taifa halitainua upanga juu ya taifa lingine,Wala hawatajifunza vita tena kamwe.+   Wataketi,* kila mtu chini ya mzabibu wake na chini ya mtini wake,+Na hakuna yeyote atakayewaogopesha,+Kwa maana kinywa cha Yehova wa majeshi kimesema hayo.   Kwa maana mataifa yote yatatembea, kila taifa katika jina la mungu wake,Lakini sisi tutatembea katika jina la Yehova Mungu wetu+ milele na milele.   “Siku hiyo,” asema Yehova,“Nitamkusanya yule aliyekuwa akichechemea,Na kumkusanya pamoja yule aliyetawanyika,+Pamoja na wale niliowatesa.   Nitamfanya yule aliyekuwa akichechemea abaki,+Na yule aliyepelekwa mbali kuwa taifa lenye nguvu;+Na Yehova atawatawala akiwa mfalme katika Mlima Sayuni,Kuanzia sasa mpaka milele.   Lakini wewe, Ee mnara wa kundi,Kilima cha binti ya Sayuni,+Kwako wewe utakuja, naam, utawala wa kwanza* utakuja,+Ufalme ambao ni wa binti ya Yerusalemu.+   Sasa kwa nini unapiga kelele? Je, huna mfalme,Au je, mshauri wako ameangamia,Hivi kwamba umeshikwa na uchungu kama mwanamke anayezaa?+ 10  Gaagaa na kulia kwa uchungu, Ee binti ya Sayuni,Kama mwanamke anayezaa,Kwa maana sasa utatoka jijini na kuishi shambani. Utaenda mpaka Babiloni,+Na huko utaokolewa;+Huko Yehova atakununua tena kutoka mikononi mwa maadui wako.+ 11  Sasa mataifa mengi yatakusanyika dhidi yako;Yatasema, ‘Acheni achafuliwe,Macho yetu na yaone Sayuni likipatwa na jambo hili.’ 12  Lakini hawajui mawazo ya Yehova,Hawaelewi kusudi* lake;Kwa maana atawakusanya kwenye uwanja wa kupuria kama safu ya miganda ya nafaka iliyotoka kukatwa. 13  Inuka upure, Ee binti ya Sayuni;+Kwa sababu nitabadili pembe zako ziwe chuma,Nami nitabadili kwato zako ziwe shaba,Nawe utapondaponda kabisa mataifa mengi.+ Faida yao isiyo ya haki utamtolea Yehova,Na mali zao utampa Bwana wa kweli wa dunia yote.”+

Maelezo ya Chini

Au “Katika kipindi cha mwisho cha zile siku.”
Au “mafundisho yatatoka.”
Au “kurekebisha.”
Au “Wataishi.”
Au “awali.”
Au “shauri.”