Mika 6:1-16

  • Mungu ana kesi dhidi ya Waisraeli (1-5)

  • Yehova anataka nini? (6-8)

    • Haki, ushikamanifu, kiasi (8)

  • Hatia na adhabu ya Waisraeli (9-16)

6  Sikieni, tafadhali, jambo analosema Yehova. Simameni, pelekeni kesi mbele ya milima,Vilima na visikie sauti yenu.+   Sikieni kesi ya Yehova, enyi milima,Enyi misingi imara ya dunia,+Kwa maana Yehova ana kesi dhidi ya watu wake;Atateta dhidi ya Israeli:+   “Watu wangu, nimewafanya nini? Nimewachoshaje?+ Toeni ushahidi dhidi yangu.   Kwa maana niliwapandisha kutoka nchini Misri,+Kutoka katika nyumba ya utumwa niliwakomboa;+Nilimtuma Musa, Haruni, na Miriamu mbele yenu.+   Watu wangu, tafadhali, kumbukeni pendekezo la Mfalme Balaki wa Moabu,+Na jibu ambalo Balaamu mwana wa Beori alimpa+—Kile kilichotukia kuanzia Shitimu+ mpaka Gilgali+Ili mjue matendo ya uadilifu ya Yehova.”   Nitakuja mbele za Yehova nikiwa na nini? Nitainama mbele za Mungu aliye juu nikiwa na nini? Je, nitakuja mbele zake nikiwa na dhabihu nzima za kuteketezwa,Nikiwa na ndama wenye umri wa mwaka mmoja?+   Je, Yehova atapendezwa na maelfu ya kondoo dume,Na makumi ya maelfu ya mito ya mafuta?+ Je, nitamtoa mwanangu mzaliwa wa kwanza kwa ajili ya uasi wangu,Uzao wa mwili wangu kwa ajili ya dhambi yangu?*+   Ee mwanadamu, amekuambia yaliyo mema. Na Yehova anataka* nini kutoka kwako? Anataka tu utekeleze haki,*+ uthamini sana ushikamanifu,*+Na utembee kwa kiasi+ na Mungu wako!+   Sauti ya Yehova inaliita jiji;Wale walio na hekima inayotumika wataliogopa jina lako. Isikilizeni fimbo na yule aliyeichagua.+ 10  Je, bado kuna hazina za uovu katika nyumba ya mwovuNa kipimo kilichopunguka cha efa* kinachochukiza? 11  Je, ninaweza kuwa safi kimaadili* nikiwa na mizani ya uovu,Nikiwa na mfuko wenye mawe ya kupimia ya udanganyifu?+ 12  Kwa maana matajiri wake wamejaa ukatili,Na wakaaji wake husema uwongo;+Ulimi wao ni mdanganyifu kinywani mwao.+ 13  “Kwa hiyo, nitakupiga na kukujeruhi,+Na kukuacha katika hali ya ukiwa kwa sababu ya dhambi zako. 14  Utakula lakini hutashiba;Utahisi njaa.+ Vitu utakavyotoa, hutaenda navyo kwa usalama,Na utakavyoenda navyo, nitaviharibu kwa upanga. 15  Utapanda mbegu, lakini hutavuna. Utakanyaga-kanyaga zeituni, lakini hutatumia mafuta yake;Nawe utatengeneza divai mpya, lakini hutakunywa divai hata kidogo.+ 16  Kwa maana unashika sheria za Omri na matendo yote ya nyumba ya Ahabu,+Nawe unafuata ushauri wao. Ndiyo sababu nitakufanya kuwa kitu cha kutishaNa wakaaji wake kuwa kitu cha kupigiwa mluzi;+Nawe utabeba dharau za mataifa.”+

Maelezo ya Chini

Au “dhambi ya nafsi yangu?”
Au “uwe mwenye fadhili na mshikamanifu katika upendo wako.” Tnn., “upende upendo mshikamanifu.”
Au “uwe mwenye haki; bila upendeleo.”
Au “anadai.”
Au “bila hatia.”