Mika 7:1-20

  • Maadili mapotovu ya Waisraeli (1-6)

    • Adui watakuwa watu wa nyumbani (6)

  • “Nitaonyesha mtazamo wa kumngojea Mungu” (7)

  • Watu wa Mungu watetewa (8-13)

  • Mika asali na kumsifu Mungu (14-20)

    • Jibu la Yehova (15-17)

    • ‘Ni Mungu gani aliye kama Yehova?’ (18)

7  Ole wangu! Mimi ni kama mtu ambaye,Baada ya matunda ya kiangazi kukusanywaNa masalio kuokotwa baada ya mavuno ya zabibu,Hapati kishada chochote cha zabibu za kula,Wala tini inayoiva mapema ninayotamani kula.*   Mtu mshikamanifu ameangamia* duniani;Miongoni mwa wanadamu hakuna yeyote aliye mnyoofu.+ Wote huvizia ili wamwage damu.+ Kila mmoja anamwinda ndugu yake mwenyewe kwa wavu wa kukokotwa.   Mikono yao ni stadi katika kutenda maovu;+Mkuu anadai vitu,Hakimu anaomba zawadi,+Mtu maarufu anasema vitu anavyotamani,*+Nao hupanga njama pamoja.*   Aliye bora zaidi kati yao ni kama miiba,Na mnyoofu zaidi kati yao ni mbaya zaidi kuliko uzio wa miiba. Siku ya walinzi wako na siku utakayowajibishwa itakuja.+ Sasa watashikwa na wasiwasi.+   Usimwamini mwenzakoWala usimtumaini rafiki wa karibu.+ Uwe mwangalifu kuhusu mambo unayomwambia yule unayelala ukiwa umemkumbatia.   Kwa maana mwana anamdharau baba yake,Binti anashindana na mama yake,+Na binti mkwe anampinga mama mkwe wake;+Maadui wa mtu ni watu wa nyumbani mwake.+   Lakini mimi, nitaendelea kumtazamia Yehova.+ Nitaonyesha mtazamo wa kumngojea* Mungu wa wokovu wangu.+ Mungu wangu atanisikia.+   Usishangilie juu yangu, ewe adui yangu.* Ingawa nimeanguka, nitasimama;Ingawa ninakaa gizani, Yehova atakuwa nuru yangu.   Ghadhabu ya Yehova nitaivumilia—Kwa maana nimemtendea dhambi—+Mpaka atakapoitetea kesi yangu na kutekeleza haki kwa ajili yangu. Atanileta nje kwenye nuru; Nitautazama uadilifu wake. 10  Adui yangu pia ataona,Na aibu itamfunika yule aliyeniambia: “Yuko wapi Yehova Mungu wako?”+ Macho yangu yatamtazama adui yangu. Sasa atakanyagwa-kanyagwa kama matope barabarani. 11  Itakuwa siku ya kujenga kuta zako za mawe;Siku hiyo mipaka itapanuliwa.* 12  Siku hiyo watakuja kwako Watatoka mbali kule Ashuru na katika majiji ya Misri,Kutoka Misri hadi kufika Mto Efrati;Kutoka bahari mpaka bahari na kutoka mlima mpaka mlima.+ 13  Na nchi itakuwa katika hali ya ukiwa kwa sababu ya wakaaji wake,Kwa sababu ya mambo waliyotenda.* 14  Wachunge watu wako kwa fimbo yako, kundi la urithi wako,+Yule aliyekuwa akiishi peke yake msituni—katika shamba la matunda. Waache wale Bashani na Gileadi+ kama ilivyokuwa siku za kale. 15  “Kama ilivyokuwa katika siku ulizotoka nchini Misri,Nitamwonyesha yeye mambo ya ajabu.+ 16  Mataifa yataona na kuaibika licha ya nguvu zote walizo nazo.+ Watafunika kinywa chao kwa mkono wao;Masikio yao yatakuwa kiziwi. 17  Wataramba mavumbi kama nyoka;+Kama wanyama wanaotambaa wa duniani watatoka katika ngome zao wakitetemeka. Watakuja kwa Yehova Mungu wetu wakiwa na hofu,Nao watakuogopa wewe.”+ 18  Ni Mungu gani aliye kama wewe,Unayesamehe dhambi na kuachilia makosa+ ya watu waliobaki wa urithi wako?+ Hutaendelea kuwa na hasira milele,Kwa maana unapendezwa na upendo mshikamanifu.+ 19  Utatuonyesha tena rehema;+ utazishinda* dhambi zetu. Utazitupa dhambi zao zote katika vilindi vya bahari.+ 20  Utamtendea Yakobo kwa uaminifu,Na Abrahamu kwa upendo mshikamanifu,Kama ulivyowaapia mababu zetu tangu siku za kale.+

Maelezo ya Chini

Au “ambayo nafsi yangu inatamani.”
Au “ametoweka.”
Tnn., “huisokota pamoja.”
Au “tamaa ya nafsi yake.”
Au “Nitamngojea kwa subira.”
Katika Kiebrania, neno “adui” liko katika jinsia ya kike.
Au labda, “amri itakuwa mbali sana.”
Tnn., “kwa sababu ya matokeo ya matendo yao.”
Au “utazikanyaga-kanyaga chini; utazitiisha.”