Mwanzo 10:1-32

  • Orodha ya mataifa (1-32)

    • Wazao wa Yafethi (2-5)

    • Wazao wa Hamu (6-20)

      • Nimrodi ampinga Yehova (8-12)

    • Wazao wa Shemu (21-31)

10  Hii ndiyo historia ya wana wa Noa, yaani, Shemu,+ Hamu, na Yafethi. Walizaa wana baada ya Gharika.+  Wana wa Yafethi walikuwa Gomeri,+ Magogu,+ Madai, Yavani, Tubali,+ Mesheki,+ na Tirasi.+  Wana wa Gomeri walikuwa Ashkenazi,+ Rifathi, na Togarma.+  Wana wa Yavani walikuwa Elisha,+ Tarshishi,+ Kitimu,+ na Dodanimu.  Kutokana na hawa, wakaaji wa visiwani walienea katika nchi zao, kulingana na lugha zao na koo zao na kulingana na mataifa yao.  Wana wa Hamu walikuwa Kushi, Misraimu,+ Putu,+ na Kanaani.+  Wana wa Kushi walikuwa Seba,+ Havila, Sabta, Raama,+ na Sabteka. Wana wa Raama walikuwa Sheba na Dedani.  Kushi akamzaa Nimrodi. Nimrodi ndiye aliyekuwa shujaa wa kwanza duniani.  Alikuwa mwindaji hodari aliyempinga Yehova. Ndiyo sababu kuna msemo usemao: “Kama Nimrodi, mwindaji hodari aliyempinga Yehova.” 10  Ufalme wake ulianzia* Babeli,+ Ereki,+ Akadi, na Kalne, katika nchi ya Shinari.+ 11  Kutoka katika nchi hiyo alienda Ashuru+ na kujenga Ninawi,+ Rehoboth-Iri, Kala, 12  na Reseni, kati ya Ninawi na Kala: Hilo ndilo lile jiji kubwa.* 13  Misraimu akamzaa Ludimu,+ Anamimu, Lehabimu, Naftuhimu,+ 14  Pathrusimu,+ Kasluhimu (hao ndio waliowazaa Wafilisti),+ na Kaftorimu.+ 15  Kanaani akamzaa Sidoni,+ mzaliwa wake wa kwanza, na Hethi,+ 16  na pia Wayebusi,+ Waamori,+ Wagirgashi, 17  Wahivi,+ Waarkia, Wasini, 18  Waarvadi,+ Wasemari, na Wahamathi.+ Baadaye, koo za Wakanaani zilitawanyika. 19  Basi mpaka wa Wakanaani ulianzia Sidoni mpaka Gerari,+ karibu na Gaza,+ hadi Sodoma, Gomora,+ Adma, na Seboiimu,+ karibu na Lasha. 20  Hao ndio waliokuwa wana wa Hamu kulingana na koo zao, lugha zao, nchi zao, na mataifa yao. 21  Shemu, babu ya wana wote wa Eberi+ na ndugu ya Yafethi mkubwa kuliko wote,* pia alizaa watoto. 22  Wana wa Shemu walikuwa Elamu,+ Asihuru,+ Arpakshadi,+ Ludi, na Aramu.+ 23  Wana wa Aramu walikuwa Usi, Huli, Getheri, na Mashi. 24  Arpakshadi akamzaa Shela,+ naye Shela akamzaa Eberi. 25  Eberi alizaa wana wawili. Mmoja aliitwa Pelegi,*+ kwa sababu katika siku zake dunia ilikuwa imegawanyika.* Ndugu yake aliitwa Yoktani.+ 26  Yoktani akamzaa Almodadi, Shelefu, Hazarmavethi, Yera,+ 27  Hadoramu, Uzali, Dikla, 28  Obali, Abimaeli, Sheba, 29  Ofiri,+ Havila, na Yobabu; wote hao walikuwa wana wa Yoktani. 30  Nchi walimokaa ilianzia Mesha mpaka Sefari, eneo lenye milima la Mashariki. 31  Hao ndio waliokuwa wana wa Shemu kulingana na koo zao, lugha zao, nchi zao, na mataifa yao.+ 32  Hizo ndizo zilizokuwa familia za wana wa Noa kulingana na koo zao na mataifa yao. Kutokana nao, mataifa yalienea duniani kote baada ya Gharika.+

Maelezo ya Chini

Au “Majiji ya kwanza ya ufalme wake yalikuwa.”
Au labda, “Yanafanyiza lile jiji kubwa.”
Au labda, “ndugu mkubwa wa Yafethi.”
Maana yake “Mgawanyiko.”
Au “wakaaji wa dunia walikuwa wamegawanyika.”